• Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
HALMASHAURI YA MJI WA MAKAMBAKO
HALMASHAURI YA MJI WA MAKAMBAKO

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA HALMASHAURI YA MJI WA MAKAMBAKO

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Ardhi na maliasili
      • Raslimali watu na Utawala
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Usafi na mazingira
      • Elimu ya Msingi
      • Ujenzi na Uokoaji
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Elimu ya Sekondari
      • Kilimo, Ushirika na umwagiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maji
    • Vitengo
      • Sheria
      • ICT and Public relations
      • Ugavi na Manunuzi
      • Mkaguzi wa ndani
      • Ufugaji Nyuki
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma ya Afya
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Huduma za Jamii
      • Kamati ya Maadili
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Mipango Miji na Mazingira
    • Ratiba
      • Ratiba ya kumwona Mwenyekiti wa Halmashauri
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
  • Miradi
    • Miradi iliyo kwenye Mpango
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Ripoti mbalimbali
    • Mikataba
    • Mpango Mkakati
    • Hatua
    • Fomu za maombi
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Hotuba
    • Habari Mpya
    • Matukio
    • jarida la mji

Mbunge viti Maalum Mkoa Wa Njombe Dk Pindi Chana Katika Mahafali shule ya Msingi Manga-Makambako.

Tarehe iliyowekwa: September 15th, 2021

Katika Picha ni Mbunge wa viti maalumu Mkoa wa Njombe Dk Pindi Chana, mgeni Rasmi katika mahafali ya arobaini na sita(46) shule ya msingi Manga Halmashauri ya Mji Makambako,Hafla ambayo imehudhuriwa na Diwani kata ya Mahongole Ndg Mario Kihombo,Diwani viti maalum na mlezi wa kata ya Mahongole Angelina Kimbawala,Mwakilishi kutoka ofisi ya Mkurugenzi Halmshauri ya Mji Makambako Yusto Nyamle,Walimu,Wazazi,walezi na wahitimu wa shule hiyo.

Akizungumza katika hafla hiyo Dk Pindi Chana amewashukuru walimu na wazazi kwa ushirikano wao kwa kufanikisha wanafunzi hao kuhitimu miaka saba(7) ya elimu ya msingi kwa ushirikiano mkubwa ,mshikimano upendo  na mwamko wa   kusukuma gurudumu la elimu hapa nchini kwa ngazi ya Halmashauri ,Mkoa mpaka Taifa.

"Niwaombe wazazi na walezi tushirikiane kuwalea watoto wetu hawa na kuwatunza kwa ukaribu mkubwa hasa kipindi hiki wanaposubiri matokeo yao ya kujiunga na elimu ya sekondari ,kwani huko mtaani watoto hawa wanasubiliwa kama simba aliye na njaa kali mawindoni hivyo basi tuache mipango ya kuwasafirisha wanafunzi hawa kwenda mijini kufanya kazi za ndani kwani bado wadogo sana kikubwa wazazi jiandaeni kuwapeleka watoto elimu ya sekondari ,amesema Dk Pindi.

Ameongeza pia elimu ndio kila kitu na ni urithi wa pekee kwa mtoto elimu ya darasa la saba ni sawa na mbegu ya mche inayoaanza kumea  safari ya elimu bado ni ndefu kwao  hivyo serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ipo pamoja na walimu ,wazazi na walezi pia hususani katika kuendelea kutatua changamoto zinazoikumba sekta ya elimu nchini ndio maana kwa mwaka wa fedha 2021-2022 serikali ya Mama Samia Suluhu Hasan imeshatoa fedha kwaajili ya kutatua changomoto kwa shule mbalimbali za msingi nchini hasa vyumba vya madarasa na shule ya Msingi Manga ni moja wapo.

 Akitoa salamu za Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji Makambako Mwakilishi wa Mkurugenzi,Yusto Nyamle amesema katika suala la elimu kwa Halmashauri ya Mji wa Makambako kimkoa si haba kwani tangu Mkoa wa Njombe kuanzishwa Halmashauri ya Mji Makambako imekua ikifanya vizuri kielimu na michezo pia.

Katika suala zima la changamoto katika shule za msingi Halmashauri ya Mji Makambako amesema kwa kila shule tayari ofisi ya Mkurugenzi inaendelea kufanyia kazi changamoto mbalimbali hususani vyumba vya madarasa  hivyo ushirikiano mkubwa unahitajika kwakuwa umoja ni nguvu na utengano ni udhaifu hasa katika kusukuma gurudumu la elimu kwa ngazi ya Halmashauri, Mkoa na taifa.

Mwisho Mbunge viti maalumu Dk pindi Chana amesema kwa niaba ya wananchi wa Mkoa wa Njombe anaishukuru serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kuwasaidia wakulima katika soko la Mahindi kwani wakulima wengi wa zao hilo walikuwa wamekata tamaa sana hususani katika Mikoa inayozalisha mahindi kwa wingi ikiwemo Mkoa wa Njombe. 

Serikali yetu ni sikivu sana wakulima sasa mahindi yao yatauzwa kwa bei nzuri ,niwaombe wana Njombe tushirikiane tudumishe amani upendo kwani amani tuliyo nayo yapo mataifa yanaitamani ,wapo watu hawana muda hata wa kukaa pamoja na kuzungumza masuala ya maendeleo kwahiyo tuitunze Lulu hii,na Katika changamoto ambayo imesomwa katika risala ya shule hiyo hususani ukosefu wa vifaa vya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEHAMA) amesema ameipokea changamoto hiyo na ataifanyia kazi kwani kwa ulimwengu wa sasa TEHAMA ndio Msingi wa Taifa lolote endelevu.

kazi iendelee.

 





Matangazo

  • Ujio wa Mwenge wa Uhuru 2025, bado siku 13 April 19, 2025
  • Ujio wa Mwenge wa Uhuru 2025, bado siku 12. April 20, 2025
  • Ujio wa Mwenge wa Uhuru 2025, bado siku 11. April 21, 2025
  • Ujio wa Mwenge wa Uhuru 2025, bado siku 10. April 22, 2025
  • Fungua

Habari Mpya

  • Wataalamu na viongozi watakiwa kusimamia upatikanaji na utoaji wa huduma za chanjo.

    April 25, 2025
  • Makambako yang'ara katika tuzo za Afya ya Usafi wa Mazingira ngazi ya Halmashauri za Miji.

    April 09, 2025
  • Jumla ya Miti 15,000 kupandwa Halmashauri ya Mji Makambako kuelekea siku ya Miti duniani mwaka 2025.

    March 15, 2025
  • Maadhimisho ya siku ya wanawake duniani 2025 Mkoa wa Njombe, Mila kandamizi zaelezwa kuwa kikwazo cha ustawi na uwezeshaji

    March 09, 2025
  • Fungua

Video

Shule mpya ya Mbugani Kitandililo sekondari kupitia mradi wa SEQUIP
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Fursa za Usafirishaji
  • Orodha ya Madiwani
  • Uzalishaji wa Umeme wa Upepo
  • Organisation Structure
  • Fursa za Biashara
  • By Laws
  • Permanent Committee

Tovuti Mashuhuri

  • Tovuti ya Ikulu ya Rais
  • Tovuti ya Ofisi ya Utumishi
  • Tovuti ya TAMISEMI
  • Tovuti ya Ofisi ya Takwimu ya Taifa (NBS)
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Open Data Tanzania

Wasomaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Makambako Town Council

    Anuani ya Posta: P.O.BOX 405 Makambako

    Simu ya mezani: 026-2730044

    Simu ya Kiganjani: 0785635383

    Barua pepe: td@makambakotc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Haki miliki ©2017 Halmashauri ya Mji Makambako. Haki zote zimehifadhiwa