• Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
HALMASHAURI YA MJI WA MAKAMBAKO
HALMASHAURI YA MJI WA MAKAMBAKO

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA HALMASHAURI YA MJI WA MAKAMBAKO

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Ardhi na maliasili
      • Raslimali watu na Utawala
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Usafi na mazingira
      • Elimu ya Msingi
      • Ujenzi na Uokoaji
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Elimu ya Sekondari
      • Kilimo, Ushirika na umwagiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maji
    • Vitengo
      • Sheria
      • ICT and Public relations
      • Ugavi na Manunuzi
      • Mkaguzi wa ndani
      • Ufugaji Nyuki
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma ya Afya
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Huduma za Jamii
      • Kamati ya Maadili
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Mipango Miji na Mazingira
    • Ratiba
      • Ratiba ya kumwona Mwenyekiti wa Halmashauri
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
  • Miradi
    • Miradi iliyo kwenye Mpango
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Ripoti mbalimbali
    • Mikataba
    • Mpango Mkakati
    • Hatua
    • Fomu za maombi
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Hotuba
    • Habari Mpya
    • Matukio
    • jarida la mji

Bil. 429.1 Zatumika kuboresha bandari ya Tanga

Tarehe iliyowekwa: May 10th, 2022



Jumla ya bil.429.1 zimetolewa na Serikali kwa ajili ya kufanya maboresho ya bandari ya Tanga,ili kupunguza gharama za kushusha mizigo baharini na uendeshaji wa operesheni,ambapo jumla ya bil.256.8 zimetolewa na serikali  awamu ya pili ili kufanya  upanuzi wa bandari  kwa  kujenga gati mbili zenye upana wa mita 150 na urefu wa mita 450 ,na bil.172.3 zilitolewa awamu ya kwanza kwa ajili ya kuongeza kina cha bahari na lango la kuingilia bahari.

Taarifa hiyo imetolewa na Mhandisi wa bandari ya Tanga,Mhandisi Khamis Omary Kipalo wakati akizungumza na Mkurugenzi wa Idara ya habari Maelezo na Msemaji Mkuu wa Serikali, Gerson Msigwa katika ziara ya Maafisa habari,Mawasiliano na Uhusiano  wa Serikali iliyofanyika leo katika bandari hiyo ili kutembelea mradi wa ujenzi wa gati za kushushia mizigo zinajengwa  na kampuni ya China Urban Co.Ltd.

Mhandisi  Kipalo amesema kuwa maboresho ya  bandari ya Tanga yamefanyika kwa awamu mbili ambapo katika awamu ya kwanza  kazi zilizofanyika ni kuongeza kina kwenye lango la bahari na kuchimba eneo la kuingilia bahari na kugharimu jumla ya shilingi Mil. 172.8 na mradi umekamilika kwa asilimia 98.

"Serikali imeamua kutoa fedha hizo ili kupunguza umbali wa kufuata mizigo baharini kutokana na kukosekana kwa gati za kushushia mizigo katika bandari hii,na gharama za utekelezaji wa operesheni zilikua kubwa sana tofauti na sasa baada ya umbali wa kushusha mizigo kupungua",alisema Kipalo

Amesema kuwa zamani meli ilipowasili  mzigo ulifuatwa kwa umbali wa kilomita 1.7 kutoka bandarini,lakini baada ya Serikali kuamua kuongeza kina cha kuingia kwenye lango la  bahari umbali kufuata mizigo umepungua na kufika mita 200 kutoka bandarini na gharama za uendeshaji wa operesheni zimepungua.

Naye Mkurugenzi wa idara ya Habari Maelezo na Msemaji Mkuu Wa Seriikali, Gerson Msigwa amesema kuwa endapo mradi huo ukikamilika utapunguza gharama za kushusha mizigo na wananchi watanufaika kupitia bandari hiyo na kupunguza msongamano wa mizigo katika bandari ya Dar es salaam kwani nchi jirani kama Rwanda,Burundi,Uganda na Kongo zinaweza kutumia bandari ya Tanga.

Amebainisha kuwa bandari ya Dar es salaam jumla ya trilioni moja inatumika kupanua njia ya kupita meli kubwa,lakini pia bandari mbalimbali ikiwemo bandari ya Kalema imefikia asilimia  90,bandari ya mtwara maboresho yamefanyika  na sasa imekamilika na ina uwezo wa kuhudumia tani milioni moja kwa mwaka,na serikali inafanya jitihada ya kuunganisha kutoka Mtwara,Mbamba bay na kuhudumia Nchi ya Malawi.

Matangazo

  • Ujio wa Mwenge wa Uhuru 2025, bado siku 13 April 19, 2025
  • Ujio wa Mwenge wa Uhuru 2025, bado siku 12. April 20, 2025
  • Ujio wa Mwenge wa Uhuru 2025, bado siku 11. April 21, 2025
  • Ujio wa Mwenge wa Uhuru 2025, bado siku 10. April 22, 2025
  • Fungua

Habari Mpya

  • Wataalamu na viongozi watakiwa kusimamia upatikanaji na utoaji wa huduma za chanjo.

    April 25, 2025
  • Makambako yang'ara katika tuzo za Afya ya Usafi wa Mazingira ngazi ya Halmashauri za Miji.

    April 09, 2025
  • Jumla ya Miti 15,000 kupandwa Halmashauri ya Mji Makambako kuelekea siku ya Miti duniani mwaka 2025.

    March 15, 2025
  • Maadhimisho ya siku ya wanawake duniani 2025 Mkoa wa Njombe, Mila kandamizi zaelezwa kuwa kikwazo cha ustawi na uwezeshaji

    March 09, 2025
  • Fungua

Video

Shule mpya ya Mbugani Kitandililo sekondari kupitia mradi wa SEQUIP
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Fursa za Usafirishaji
  • Orodha ya Madiwani
  • Uzalishaji wa Umeme wa Upepo
  • Organisation Structure
  • Fursa za Biashara
  • By Laws
  • Permanent Committee

Tovuti Mashuhuri

  • Tovuti ya Ikulu ya Rais
  • Tovuti ya Ofisi ya Utumishi
  • Tovuti ya TAMISEMI
  • Tovuti ya Ofisi ya Takwimu ya Taifa (NBS)
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Open Data Tanzania

Wasomaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Makambako Town Council

    Anuani ya Posta: P.O.BOX 405 Makambako

    Simu ya mezani: 026-2730044

    Simu ya Kiganjani: 0785635383

    Barua pepe: td@makambakotc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Haki miliki ©2017 Halmashauri ya Mji Makambako. Haki zote zimehifadhiwa