• Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
HALMASHAURI YA MJI WA MAKAMBAKO
HALMASHAURI YA MJI WA MAKAMBAKO

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA HALMASHAURI YA MJI WA MAKAMBAKO

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Ardhi na maliasili
      • Raslimali watu na Utawala
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Usafi na mazingira
      • Elimu ya Msingi
      • Ujenzi na Uokoaji
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Elimu ya Sekondari
      • Kilimo, Ushirika na umwagiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maji
    • Vitengo
      • Sheria
      • ICT and Public relations
      • Ugavi na Manunuzi
      • Mkaguzi wa ndani
      • Ufugaji Nyuki
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma ya Afya
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Huduma za Jamii
      • Kamati ya Maadili
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Mipango Miji na Mazingira
    • Ratiba
      • Ratiba ya kumwona Mwenyekiti wa Halmashauri
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
  • Miradi
    • Miradi iliyo kwenye Mpango
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Ripoti mbalimbali
    • Mikataba
    • Mpango Mkakati
    • Hatua
    • Fomu za maombi
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Hotuba
    • Habari Mpya
    • Matukio
    • jarida la mji

Chama cha Skauti Makambako,chaadhimisha kumbukizi ya muasisi wa Skauti duniani kwa kupanda miti ya parachichi.

Tarehe iliyowekwa: February 22nd, 2023

Na. Lina Sanga

Chama cha Skauti Halmashauri ya Mji Makambako leo,kimeadhimisha kumbukumbu ya kuzaliwa kwa muasisi wa skauti duniani, Baden Powell raia wa Uingereza  kwa kupanda miti ya parachichi shule ya Msingi Mwembetogwa, iliyotolewa na Serikali kwa ajili ya kukuza kipato cha shule na lishe kwa wanafunzi.

Akizungumza baada ya kukamilika kwa zoezi la upandaji miti ,Mwl. Diana Nyemele ambaye ni mwanzilish na mlezi wa skauti Wilaya ya Njombe, ameishukuru Serikali kwa kutoa miche ya parachichi mashuleni na kuwataka wanachama wa Skauti kudumisha amani,upendo na uzalendo kwani lengo kuu la kuanzishwa kwa chama cha skauti ni kujenga vijana wenye  ukakamavu,mshikamano na uzalendo kwa manufaa ya jamii na nchi kwa ujumla.

Amesema kuwa,chama cha skauti kilianzishwa mnamo mwaka 2004 katika shule ya Msingi Azimio ,Njombe ikiwa Wilaya chini ya Mkoa wa Iringa ,na baadaye ilienea shule mbalimbali na hadi sasa chama hicho kipo imara na kutoa wito kwa wanafunzi kujiunga na chama cha skauti ,ili waweze kujifunza stadi za maisha na masuala mbalimbali ya ulinzi binafsi na taifa kwa ujumla.

Naye Mwl.Emmanuel Lugongo,Kamishina wa skauti Wilaya ya Njombe ametoa wito kwa vijana ambao wamehitimu masomo na hawana ajira, kujiunga na chama cha skauti na kukiendeleza kiwanda cha utengenezaji chaki,kilichoanzishwa na wanachama wa skauti wa Makambako.

Ametoa wito kwa Walimu wakuu na wamiliki wa shule kuunga mkono juhudi za chama cha skauti kwa kununua chaki, zinazotengenezwa katika kiwanda hicho ili vijana wasio na ajira waendelee kujiajiri.

Tusiwene Mahenge,ambaye ni muasisi wa Chama cha Skauti Mkoa wa Iringa 2004 na Mlezi wa skauti Mkoa wa Njombe kwa sasa,ametoa wito kwa wanafunzi wote ambao ni wanachama wa chama cha skauti kuzingatia masomo na kuhakikisha wanafaulu vizuri,ili kukijengea sifa nzuri chama hicho kwani wengi waliopitia mafunzo ya skauti wamefanikiwa kupata ajira katika kada mbalimbali ikiwa ni pamoja na  jeshi.

Chama cha Skauti kilianza rasmi Mwaka 1912 Zanzibar na Mwaka 1917  Tanganyika na Mkoani Njombe mwaka 2004 ikiwa ni Wilaya iliyokuwa chini ya Mkoa wa Iringa.

Maadhimisho ya kumbukizi ya kuzaliwa kwa muasisi wa skauti hufanyika februari 22,kila mwaka ambapo kwa mwaka huu  kitaifa maadhimisho hayo yanafanyika jijini Tanga.

Matangazo

  • Ujio wa Mwenge wa Uhuru 2025, bado siku 13 April 19, 2025
  • Ujio wa Mwenge wa Uhuru 2025, bado siku 12. April 20, 2025
  • Ujio wa Mwenge wa Uhuru 2025, bado siku 11. April 21, 2025
  • Ujio wa Mwenge wa Uhuru 2025, bado siku 10. April 22, 2025
  • Fungua

Habari Mpya

  • Wataalamu na viongozi watakiwa kusimamia upatikanaji na utoaji wa huduma za chanjo.

    April 25, 2025
  • Makambako yang'ara katika tuzo za Afya ya Usafi wa Mazingira ngazi ya Halmashauri za Miji.

    April 09, 2025
  • Jumla ya Miti 15,000 kupandwa Halmashauri ya Mji Makambako kuelekea siku ya Miti duniani mwaka 2025.

    March 15, 2025
  • Maadhimisho ya siku ya wanawake duniani 2025 Mkoa wa Njombe, Mila kandamizi zaelezwa kuwa kikwazo cha ustawi na uwezeshaji

    March 09, 2025
  • Fungua

Video

Shule mpya ya Mbugani Kitandililo sekondari kupitia mradi wa SEQUIP
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Fursa za Usafirishaji
  • Orodha ya Madiwani
  • Uzalishaji wa Umeme wa Upepo
  • Organisation Structure
  • Fursa za Biashara
  • By Laws
  • Permanent Committee

Tovuti Mashuhuri

  • Tovuti ya Ikulu ya Rais
  • Tovuti ya Ofisi ya Utumishi
  • Tovuti ya TAMISEMI
  • Tovuti ya Ofisi ya Takwimu ya Taifa (NBS)
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Open Data Tanzania

Wasomaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Makambako Town Council

    Anuani ya Posta: P.O.BOX 405 Makambako

    Simu ya mezani: 026-2730044

    Simu ya Kiganjani: 0785635383

    Barua pepe: td@makambakotc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Haki miliki ©2017 Halmashauri ya Mji Makambako. Haki zote zimehifadhiwa