• Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
HALMASHAURI YA MJI WA MAKAMBAKO
HALMASHAURI YA MJI WA MAKAMBAKO

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA HALMASHAURI YA MJI WA MAKAMBAKO

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Ardhi na maliasili
      • Raslimali watu na Utawala
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Usafi na mazingira
      • Elimu ya Msingi
      • Ujenzi na Uokoaji
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Elimu ya Sekondari
      • Kilimo, Ushirika na umwagiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maji
    • Vitengo
      • Sheria
      • ICT and Public relations
      • Ugavi na Manunuzi
      • Mkaguzi wa ndani
      • Ufugaji Nyuki
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma ya Afya
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Huduma za Jamii
      • Kamati ya Maadili
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Mipango Miji na Mazingira
    • Ratiba
      • Ratiba ya kumwona Mwenyekiti wa Halmashauri
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
  • Miradi
    • Miradi iliyo kwenye Mpango
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Ripoti mbalimbali
    • Mikataba
    • Mpango Mkakati
    • Hatua
    • Fomu za maombi
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Hotuba
    • Habari Mpya
    • Matukio
    • jarida la mji

Chuo cha VETA kujengwa Halmashauri ya Mji Makambako

Tarehe iliyowekwa: July 19th, 2022

Na. Lina Sanga

Ili kukabiliana na changamoto ya ukosefu wa ajira kwa vijana,Halmashauri ya Mji Makambako inatarajia kujenga chuo cha ufundi stadi(VETA),ili vijana waweze kujiendeleza na baadaye kujiajiri na eneo la ujenzi wa chuo hicho limeshapatikana.

Hayo yameelezwa na Mbunge wa Jimbo la Makambako, Mhe. Deo Sanga katika mkutano wa hadhara uliofanyika leo katika kitongoji cha Nyambogo,Luhota na Kijiji cha Ngamanga,Kata ya Utengule  ikiwa ni ziara ya Mbunge ya kijiji kwa kijiji,Mtaa kwa Mtaa ili kuongea na wananchi,kusikiliza kero zao na kutoa jumbe mbalimbali za Serikali ikiwa ni pamoja na Ujumbe wa Sensa ya watu na Makazi 2022,Mbolea ya ruzuku na bajeti ya Serikali ya mwaka 2022/2023.

Amesema kuwa kutokana na changamoto ya ajira nchini,chuo cha VETA kitawawezesha vijana wanapohitimu elimu ya msingi,kidato cha nne na kuendelea,kujiunga na chuo hicho kujifunza kazi mbalimbali ili waweze kujiajiri badala ya kusubiri kuajiriwa,kwani Serikali imeshaweka utaratibu wa utoaji mikopo ya wanawake,vijana na watu wenye ulemavu ili kuwawezesha vijana kupata mtaji wa kuanza biashara au kilimo na shughuli nyingine.

Pia,amempongeza uongozi wa kijiji cha Ikelu kwa kujitoa kuchangia ujenzi wa Kituo cha Afya,nyumba ya watumishi pamoja na shule ya msingi shikizi Ikelu B,yenye maboma matano na ofisi Moja na darasa moja limekamilika kwa fedha ya ruzuku kutoka Serikali Kuu shilingi Mil. 12.5 na darasa hilo linaweza tumika ili kuwapunguzia wanafunzi umbali wa kutembea hadi shule ya Msingi Ikelu.

Aidha,ametoa wito kwa viongozi wa dini kumuombea Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Mhe. Samia Suluhu Hassan kwa kazi kubwa anayoifanya ya kuhakikisha Tanzania inapata maendeleo,na Halmashauri ya Mji Makambako pia kwa kutoa fedha za miradi na maendeleo.

Pia,ametoa wito kwa wazee vijiji kuwaombea Mhe. Samia pamoja na Viongozi wote wa Mji wa Makambako,kwa sababu mila zipo na Serikali inawaamini.

Matangazo

  • Ujio wa Mwenge wa Uhuru 2025, bado siku 13 April 19, 2025
  • Ujio wa Mwenge wa Uhuru 2025, bado siku 12. April 20, 2025
  • Ujio wa Mwenge wa Uhuru 2025, bado siku 11. April 21, 2025
  • Ujio wa Mwenge wa Uhuru 2025, bado siku 10. April 22, 2025
  • Fungua

Habari Mpya

  • Mil. 350.8 za Mikopo ya 10% zimetolewa kwa vikundi 30 Halmashauri ya Mji Makambako,DC aagiza mikopo hiyo kuwa chanzo cha utajiri.

    August 14, 2025
  • MIL 350.8 ZA MIKOPO YA 10% ZATOLEWA KWA AWAMU YA PILI KWA MWAKA 2024/2025.

    August 01, 2025
  • Wataalamu na viongozi watakiwa kusimamia upatikanaji na utoaji wa huduma za chanjo.

    April 25, 2025
  • Makambako yang'ara katika tuzo za Afya ya Usafi wa Mazingira ngazi ya Halmashauri za Miji.

    April 09, 2025
  • Fungua

Video

Shule mpya ya Mbugani Kitandililo sekondari kupitia mradi wa SEQUIP
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Fursa za Usafirishaji
  • Orodha ya Madiwani
  • Uzalishaji wa Umeme wa Upepo
  • Organisation Structure
  • Fursa za Biashara
  • By Laws
  • Permanent Committee

Tovuti Mashuhuri

  • Tovuti ya Ikulu ya Rais
  • Tovuti ya Ofisi ya Utumishi
  • Tovuti ya TAMISEMI
  • Tovuti ya Ofisi ya Takwimu ya Taifa (NBS)
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Open Data Tanzania

Wasomaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Makambako Town Council

    Anuani ya Posta: P.O.BOX 405 Makambako

    Simu ya mezani: 026-2730044

    Simu ya Kiganjani: 0785635383

    Barua pepe: td@makambakotc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Haki miliki ©2017 Halmashauri ya Mji Makambako. Haki zote zimehifadhiwa