• Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
HALMASHAURI YA MJI WA MAKAMBAKO
HALMASHAURI YA MJI WA MAKAMBAKO

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA HALMASHAURI YA MJI WA MAKAMBAKO

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Ardhi na maliasili
      • Raslimali watu na Utawala
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Usafi na mazingira
      • Elimu ya Msingi
      • Ujenzi na Uokoaji
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Elimu ya Sekondari
      • Kilimo, Ushirika na umwagiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maji
    • Vitengo
      • Sheria
      • ICT and Public relations
      • Ugavi na Manunuzi
      • Mkaguzi wa ndani
      • Ufugaji Nyuki
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma ya Afya
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Huduma za Jamii
      • Kamati ya Maadili
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Mipango Miji na Mazingira
    • Ratiba
      • Ratiba ya kumwona Mwenyekiti wa Halmashauri
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
  • Miradi
    • Miradi iliyo kwenye Mpango
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Ripoti mbalimbali
    • Mikataba
    • Mpango Mkakati
    • Hatua
    • Fomu za maombi
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Hotuba
    • Habari Mpya
    • Matukio
    • jarida la mji

DC Sweda asisitiza zoezi la uhamisho wa muda wa wafanyabiashara wa Soko kuu na Stendi ya zamani kuwa shirikishi.

Tarehe iliyowekwa: February 20th, 2025


Na. Tanessa Lyimo

Mkuu wa Wilaya ya Njombe,Mhe. Juma Sweda ameutaka uongozi wa  Halmashauri ya Mji Makambako kushirikiana na wafanyabiashara wa Soko kuu na  Stendi ya zamani, katika harakati za kuwahamishia kwa muda wafanyabiashara hao katika eneo  la kuoshea magari mkabala na A one lodge,  lililopo katika Mtaa wa Kahawa, Kata ya  Kitisi  ili kupisha ujenzi wa Soko la kisasa unaotarajiwa kuanza mwaka ujao wa fedha 2025/2026,kupitia mradi wa uboreshaji miji wa TACTIC.

 

Mhe. Sweda ametoa rai hiyo leo katika Mkutano wa hadhara na wafanyabiashara wa Soko kuu na Stendi  ya zamani , na kumuagiza Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji Makambako, kuzingatia suala la Miundombinu wakati wa ujenzi wa soko hilo hasa miundombinu ya vyoo.

Aidha,ameuagiza uongozi wa  Halmashauri kupitia divisheni ya Biashara,Viwanda na Uwekezaji kuendelea kuboresha mazingira ya wafanyabiashara kwa  kutekeleza majukumu yao, ili kusaidia kuongeza mapato na kuleta taswira nzuri ya uwekezaji katika Mji wa Makambako.

Wakati huo huo, Mbunge wa jimbo la Makambako, Mhe. Deo Kasenyenda Sanga amemkaribisha  Mhe. Sweda katika jimbo la Makambako baada ya kufanyika kwa mabadiliko ya wakuu wa Wilaya na kumshukuru Dkt.Samia Suluhu Hassan ,kwa kutambua umuhimu wa sekta ya Afya  kwa kutoa vifaa mbalimbali, ikiwa ni pamoja na  magari mawili ya kubebea wagonjwa aliyokabidhi leo.

Ndg. Kenneth Haule, Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji Makambako , amewataka wananchi kupuuza taarifa za upotoshaji kuhusu  eneo la muda lililotengwa kwa matumizi ya soko wakati wa ujenzi wa soko jipya, na kuwahakikishia kuwa kila mfanyabiashara  anayetambulika na uongozi wa soko hilo atapata nafasi ya kufanya biashara bila kubaguliwa wala  kusumbuliwa katika eneo hilo.

Naye, Mwenyekiti wa Jumuiya ya wafanyabiashara Mkoa wa Njombe na Nyanda za juu Kusini,Ndg. Sifael Msigala amemshukuru Mkurugenzi kwa ushirikiano baina ya wafanyabiashara na watendaji wa Serikali, katika mchakato mzima wa maandalizi ya awali katika mageuzi ya soko hilo na katika masuala mbalimbali yanayohusu maendeleo na changamoto zinazowakabili wafanyabiashara.

Matangazo

  • Ujio wa Mwenge wa Uhuru 2025, bado siku 13 April 19, 2025
  • Ujio wa Mwenge wa Uhuru 2025, bado siku 12. April 20, 2025
  • Ujio wa Mwenge wa Uhuru 2025, bado siku 11. April 21, 2025
  • Ujio wa Mwenge wa Uhuru 2025, bado siku 10. April 22, 2025
  • Fungua

Habari Mpya

  • Wataalamu na viongozi watakiwa kusimamia upatikanaji na utoaji wa huduma za chanjo.

    April 25, 2025
  • Makambako yang'ara katika tuzo za Afya ya Usafi wa Mazingira ngazi ya Halmashauri za Miji.

    April 09, 2025
  • Jumla ya Miti 15,000 kupandwa Halmashauri ya Mji Makambako kuelekea siku ya Miti duniani mwaka 2025.

    March 15, 2025
  • Maadhimisho ya siku ya wanawake duniani 2025 Mkoa wa Njombe, Mila kandamizi zaelezwa kuwa kikwazo cha ustawi na uwezeshaji

    March 09, 2025
  • Fungua

Video

Shule mpya ya Mbugani Kitandililo sekondari kupitia mradi wa SEQUIP
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Fursa za Usafirishaji
  • Orodha ya Madiwani
  • Uzalishaji wa Umeme wa Upepo
  • Organisation Structure
  • Fursa za Biashara
  • By Laws
  • Permanent Committee

Tovuti Mashuhuri

  • Tovuti ya Ikulu ya Rais
  • Tovuti ya Ofisi ya Utumishi
  • Tovuti ya TAMISEMI
  • Tovuti ya Ofisi ya Takwimu ya Taifa (NBS)
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Open Data Tanzania

Wasomaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Makambako Town Council

    Anuani ya Posta: P.O.BOX 405 Makambako

    Simu ya mezani: 026-2730044

    Simu ya Kiganjani: 0785635383

    Barua pepe: td@makambakotc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Haki miliki ©2017 Halmashauri ya Mji Makambako. Haki zote zimehifadhiwa