• Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
HALMASHAURI YA MJI WA MAKAMBAKO
HALMASHAURI YA MJI WA MAKAMBAKO

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA HALMASHAURI YA MJI WA MAKAMBAKO

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Ardhi na maliasili
      • Raslimali watu na Utawala
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Usafi na mazingira
      • Elimu ya Msingi
      • Ujenzi na Uokoaji
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Elimu ya Sekondari
      • Kilimo, Ushirika na umwagiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maji
    • Vitengo
      • Sheria
      • ICT and Public relations
      • Ugavi na Manunuzi
      • Mkaguzi wa ndani
      • Ufugaji Nyuki
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma ya Afya
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Huduma za Jamii
      • Kamati ya Maadili
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Mipango Miji na Mazingira
    • Ratiba
      • Ratiba ya kumwona Mwenyekiti wa Halmashauri
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
  • Miradi
    • Miradi iliyo kwenye Mpango
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Ripoti mbalimbali
    • Mikataba
    • Mpango Mkakati
    • Hatua
    • Fomu za maombi
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Hotuba
    • Habari Mpya
    • Matukio
    • jarida la mji

Halmashauri ya Mji Makambako imezindua Miongozo ya elimu leo,Madiwani wasema wanataka Makambako kuwa namba moja kila idara ya elimu

Tarehe iliyowekwa: September 28th, 2022

Na. Lina Sanga

Mhe. Imani Fute kwa niaba ya Mwenyekiti wa Halmashauri ya Mji Makambako na Madiwani wote,ametoa kauli hiyo leo  Katika hafla ya uzinduzi wa Miongozo ya elimu ngazi ya Halmashauri, uliofanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Halmashauri ya Mji Makambako.

Akizungumza na Wajumbe wa Kamati ya fedha na Uongozi,Maafisa elimu idara ya Msingi na Sekondari,Wakuu wa shule na Walimu wakuu wote pamoja na wanafunzi ,Mhe. Fute amesema kuwa ipo haja ya walimu  kuwashirikisha madiwani ili kufikia lengo la kukuza taaluma katika Kata zote za Halmashauri ya Mji Makambako.

Mhe. Fute amesema kuwa,Serikali chini ya Mhe. Samia Suluhu Hassan,Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imefanya vizuri katika eneo la elimu hasa kwenye uandaaji wa miongozo ya uboreshaji elimumsingi na sekondari pamoja na mkakati wa kuimarisha ufundishaji na ujifunzaji ngazi ya elimumsingi.


Ameongeza kuwa,ipo haja ya Walimu kuwashirikisha Madiwani  katika utekelezaji wa jambo lolote linalofaa ili kukuza taaluma,kwani Madiwani pia wana nia njema ya kuhakikisha taaluma katika Halmashauri hiyo inapewa kipaumbele na inaendelea kukua kila siku.


Amesema ili taaluma iendelee kukua ipo haja ya kila mtu kusimama vizuri katika nafasi yake, kuanzia wananchi,madiwani na walimu, na diwani ni kiungo muhimu kati ya wananchi na walimu kwani wanatoka miongoni mwa wananchi wa Kata husika.


Ametoa wito kwa walimu kuendelea kutekeleza majukumu yao kwa weledi,kwa kutambua madiwani wote wana nia njema na wanawapenda kwani wanatambua kazi kubwa na jitihada zao wanazozifanya katika kuhakikisha taaluma inakua.

Vitabu vya miongozo vilikabidhiwa kwa Afisa elimu taaluma Halmashauri ya Mji Makambako na Mratibu elimu Kata kwa ajili ya kuuanza utekelezaji.

 

Matangazo

  • Ujio wa Mwenge wa Uhuru 2025, bado siku 13 April 19, 2025
  • Ujio wa Mwenge wa Uhuru 2025, bado siku 12. April 20, 2025
  • Ujio wa Mwenge wa Uhuru 2025, bado siku 11. April 21, 2025
  • Ujio wa Mwenge wa Uhuru 2025, bado siku 10. April 22, 2025
  • Fungua

Habari Mpya

  • Wataalamu na viongozi watakiwa kusimamia upatikanaji na utoaji wa huduma za chanjo.

    April 25, 2025
  • Makambako yang'ara katika tuzo za Afya ya Usafi wa Mazingira ngazi ya Halmashauri za Miji.

    April 09, 2025
  • Jumla ya Miti 15,000 kupandwa Halmashauri ya Mji Makambako kuelekea siku ya Miti duniani mwaka 2025.

    March 15, 2025
  • Maadhimisho ya siku ya wanawake duniani 2025 Mkoa wa Njombe, Mila kandamizi zaelezwa kuwa kikwazo cha ustawi na uwezeshaji

    March 09, 2025
  • Fungua

Video

Shule mpya ya Mbugani Kitandililo sekondari kupitia mradi wa SEQUIP
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Fursa za Usafirishaji
  • Orodha ya Madiwani
  • Uzalishaji wa Umeme wa Upepo
  • Organisation Structure
  • Fursa za Biashara
  • By Laws
  • Permanent Committee

Tovuti Mashuhuri

  • Tovuti ya Ikulu ya Rais
  • Tovuti ya Ofisi ya Utumishi
  • Tovuti ya TAMISEMI
  • Tovuti ya Ofisi ya Takwimu ya Taifa (NBS)
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Open Data Tanzania

Wasomaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Makambako Town Council

    Anuani ya Posta: P.O.BOX 405 Makambako

    Simu ya mezani: 026-2730044

    Simu ya Kiganjani: 0785635383

    Barua pepe: td@makambakotc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Haki miliki ©2017 Halmashauri ya Mji Makambako. Haki zote zimehifadhiwa