• Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
HALMASHAURI YA MJI WA MAKAMBAKO
HALMASHAURI YA MJI WA MAKAMBAKO

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA HALMASHAURI YA MJI WA MAKAMBAKO

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Ardhi na maliasili
      • Raslimali watu na Utawala
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Usafi na mazingira
      • Elimu ya Msingi
      • Ujenzi na Uokoaji
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Elimu ya Sekondari
      • Kilimo, Ushirika na umwagiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maji
    • Vitengo
      • Sheria
      • ICT and Public relations
      • Ugavi na Manunuzi
      • Mkaguzi wa ndani
      • Ufugaji Nyuki
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma ya Afya
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Huduma za Jamii
      • Kamati ya Maadili
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Mipango Miji na Mazingira
    • Ratiba
      • Ratiba ya kumwona Mwenyekiti wa Halmashauri
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
  • Miradi
    • Miradi iliyo kwenye Mpango
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Ripoti mbalimbali
    • Mikataba
    • Mpango Mkakati
    • Hatua
    • Fomu za maombi
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Hotuba
    • Habari Mpya
    • Matukio
    • jarida la mji

Bil. 42 za mradi wa maji zatolewa Serikali kwa Halmashauri ya Mji Makambako

Tarehe iliyowekwa: July 18th, 2022

Na. Lina Sanga

Halmashauri ya Mji Makambako katika bajeti ya Serikali kwa mwaka wa fedha 2022/2023 imepata jumla ya shilingi Bil. 42 kwa ajili ya utekelezaji wa miradi ya Maji na mkataba tayari umesainiwa na mkandarasi.

Hayo yameelezwa na Mbunge wa jimbo la Makambako,Mhe. Deo Kasenyenda Sanga katika mkutano wa hadhara  katika  Kijiji cha Mawande, Utengule na Ikelu leo,ikiwa ni sehemu ya ziara ya Mbunge ya kutembelea wananchi na kusikiliza kero zao.

Mhe. Sanga amesema kuwa katika awamu zote za Serikali zilizopita halmashauri ya Mji Makambako haijawahi kupata fedha nyingi kama awamu hii ya Sita chini ya Rais Samia Suluhu Hassan kwa ajili ya miundombinu ya elimu na Maji.

“Juzi tulikuwa ikulu kushuhudia utiaji saini mikataba ya maji ambapo nimeshuhudia Mkandarasi akisaini Mkataba wa mradi wa Maji wa Halmashauri ya Mji Makambako wenye jumla ya Bil. 42,na hiyo ni sababu inayotufanya sisi kumpongeza Mhe. Samia Suluhu Hassan,Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kutuona Sisi na kutupatia fedha nyingi kwani haijawai kutokea kupata fedha nyingi kiasi hiki”,alisema Mhe. Sanga.

Ameongeza kuwa jumla ya miji 28 pekee Nchini imepata fedha za utekelezaji wa miradi mikubwa ya maji,Halmashauri ya Mji Makambako ikiwa ni miongoni mwa Miji hiyo,hivyo kupitia miradi hiyo vijana wetu watapata ajira ya kuchimba mitaro na kazi mbalimbali wakati wa ujenzi wa miradi ya maji katika Halmashauri.

 Amesema kwa upande wa elimu,ametoa fedha zake binafsi kwa ajili ya kujenga madarasa zaidi ya tisa pamoja na ofisi ili kuunga juhudi za Serikali na wananchi katika kujenga na kuboresha miundombinu ya elimu,hivyo kwa kila mwananchi hana budi kuchangia ujenzi wa madarasa kwani hata kijana ambaye ana mtoto mdogo sasa, anatakiwa kuchangia ujenzi wa madarasa na bweni kwani mtoto wake akikua atatumia madarasa hayo na bweni.

Ameongeza kuwa Serikali imekuwa ikileta fedha kwa ajili ya ujenzi wa majengo mbalimbali katika sekta ya afya na elimu,lakini pia wananchi wanatakiwa kuchangia ili kuona thamani ya majengo hayo kupitia michango mbalimbali.

“Serikali imekuwa na taratibu za kuleta fedha mara kwa mara kwa ajili ya miradi ya ujenzi wa vituo vya afya,zahanati na madarasa,lakini ili kuonyesha uhuitaji wa majengo hayo Serikali inamtaka kila mwananchi kuchangia ili kuonyesha thamani ya jengo linalojengwa iwe kwa kubeba mawe,kusafisha eneo na kazi zingine katika eneo la mradi”,alisema Mhe. Sanga.

Katika kijiji cha Mawande Mhe. Sanga ameahidi kuchangia ujenzi wa shule shikizi katika kitongoji cha Mjimwema ili kuwapunguzia umbali wanafunzi wa kutembea,ambapo jumla ya tofali elfu mbili zitatolewa na mifuko 50 ya saruji kwa ajili ya ujenzi wa madarasa mawili ya kuanzia.

Katika kuunga juhudi za Serikali na wananchi  za ujenzi wa madarasa kwa shule mbalimbali zilizopo Halmashauri ya Mji Makmbako,Mhe. Deo Kasenyenda Sanga kwa mwaka huu amejenga jumla ya madarasa tisa na ofisi mbili ambapo shule ya Kitisi Sekondari madarasa mawili,Shule ya Msingi Mwembetogwa madarasa mawili na ofisi moja, Shule ya Msingi uhuru madarasa mawili,shule ya msingi ilangamoto darasa moja,shule ya msingi shikizi kifumbe madarasa mawili na Ofisi moja.

Pia kupitia wadau ambao ni Asas jumla ya madarasa mawili yamejengwa katika shule ya msingi Magegele na madarasa hayo yapo katika hatua za ukamilishaji na darasa moja katika shule ya Msingi Majengo lilijengwa na aliyekuwa Mbunge wa Mbarali kutokana na ushawishi wa Mhe. Sanga.

Matangazo

  • Ujio wa Mwenge wa Uhuru 2025, bado siku 13 April 19, 2025
  • Ujio wa Mwenge wa Uhuru 2025, bado siku 12. April 20, 2025
  • Ujio wa Mwenge wa Uhuru 2025, bado siku 11. April 21, 2025
  • Ujio wa Mwenge wa Uhuru 2025, bado siku 10. April 22, 2025
  • Fungua

Habari Mpya

  • Wataalamu na viongozi watakiwa kusimamia upatikanaji na utoaji wa huduma za chanjo.

    April 25, 2025
  • Makambako yang'ara katika tuzo za Afya ya Usafi wa Mazingira ngazi ya Halmashauri za Miji.

    April 09, 2025
  • Jumla ya Miti 15,000 kupandwa Halmashauri ya Mji Makambako kuelekea siku ya Miti duniani mwaka 2025.

    March 15, 2025
  • Maadhimisho ya siku ya wanawake duniani 2025 Mkoa wa Njombe, Mila kandamizi zaelezwa kuwa kikwazo cha ustawi na uwezeshaji

    March 09, 2025
  • Fungua

Video

Shule mpya ya Mbugani Kitandililo sekondari kupitia mradi wa SEQUIP
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Fursa za Usafirishaji
  • Orodha ya Madiwani
  • Uzalishaji wa Umeme wa Upepo
  • Organisation Structure
  • Fursa za Biashara
  • By Laws
  • Permanent Committee

Tovuti Mashuhuri

  • Tovuti ya Ikulu ya Rais
  • Tovuti ya Ofisi ya Utumishi
  • Tovuti ya TAMISEMI
  • Tovuti ya Ofisi ya Takwimu ya Taifa (NBS)
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Open Data Tanzania

Wasomaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Makambako Town Council

    Anuani ya Posta: P.O.BOX 405 Makambako

    Simu ya mezani: 026-2730044

    Simu ya Kiganjani: 0785635383

    Barua pepe: td@makambakotc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Haki miliki ©2017 Halmashauri ya Mji Makambako. Haki zote zimehifadhiwa