• Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
HALMASHAURI YA MJI WA MAKAMBAKO
HALMASHAURI YA MJI WA MAKAMBAKO

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA HALMASHAURI YA MJI WA MAKAMBAKO

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Ardhi na maliasili
      • Raslimali watu na Utawala
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Usafi na mazingira
      • Elimu ya Msingi
      • Ujenzi na Uokoaji
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Elimu ya Sekondari
      • Kilimo, Ushirika na umwagiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maji
    • Vitengo
      • Sheria
      • ICT and Public relations
      • Ugavi na Manunuzi
      • Mkaguzi wa ndani
      • Ufugaji Nyuki
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma ya Afya
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Huduma za Jamii
      • Kamati ya Maadili
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Mipango Miji na Mazingira
    • Ratiba
      • Ratiba ya kumwona Mwenyekiti wa Halmashauri
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
  • Miradi
    • Miradi iliyo kwenye Mpango
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Ripoti mbalimbali
    • Mikataba
    • Mpango Mkakati
    • Hatua
    • Fomu za maombi
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Hotuba
    • Habari Mpya
    • Matukio
    • jarida la mji

Jukwaa la wadau wa ustawi wa Mtoto Halmashauri ya Mji Makambako lazinduliwa rasmi leo.

Tarehe iliyowekwa: December 4th, 2023

Na. Lina Sanga

Jukwaa la wadau wa ustawi wa mtoto limezinduliwa rasmi leo katika Halmashauri ya Mji Makambako,ili kuwawezesha wadau mbalimbali kuchangia mahitaji ya watoto wanaoishi kwenye mazingira hatarishi.

Akizungumza na wadau wa ustawi wa mtoto katika Halmashauri ya Mji Makambako leo,Bw. Erick Haule kwa niaba ya Afisa ustawi wa jamii Mkoa wa Njombe, amesema kuwa lengo kuu la jukwaa hilo ni kutekeleza Mpango wa taifa wa kuhudumia watoto wanaoishi katika mazingira hatarishi wa mwaka 2017  , wenye malengo mbalimbali ikiwa ni pamoja na kuongeza na kuimarisha uwezo wa kaya na jamii kuhudumia watoto waliopo katika mazingira yao.

Amesema kuwa,lengo lingine la jukwaa hilo ni kuongeza upatikanaji na matumizi ya huduma zinazozuia na kuitikia masuala yote yanayohusiana na ukatili wa Kijinsia na ukatili dhidi ya watoto,na  kuboresha uwezo wa  watoto waliopo katika  mazingira hatarishi kuweza kutumia na kupata huduma za elimu,Afya na maendeleo na makuzi yao.

Ametoa rai kwa wadau wa ustawi wa mtoto kuratibu huduma wanazotoa kwa watoto ,ili kujua huduma zinazotolewa kwa watoto hao na kuhakikisha huduma hizo zinawafikia watoto wote wenye uhitaji, na kutambua mazingira wanayoishi watoto kwani ni chanzo kikubwa cha kuongezeka kwa watoto wanaoishi mazingira hatarishi kutokana na kaya zao kukithiri vitendo vya ukatili.

Pia ametoa wito kwa wadau wenye nia ya kutoa huduma kwa watoto kutoa huduma zinazoendana na umri wao,kama viatu,mavazi na kutowapa vyakula vilivyoharibika na visivyofaa kwa matumizi ya binadamu kwa kigezo cha kutoa msaada.

Bi. Appia Mayemba,Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji Makambako ametoa wito kwa wadau mbalimbali wa ustawi wa mtoto, katika Halmashauri ya Mji Makambako kujitoa katika kuchangia mahitaji ya watoto wanaoishi katika mazingira hatarishi,ili kuwawezesha watoto hao kufikia malengo yao na kuweza kujitegemea.

Jukwaa la wadau la ustawi wa mtoto Mkoa wa Njombe,lilizinduliwa rasmi septemba 29,2023 na Mhe. Anthony Mtaka,Mkuu wa Mkoa wa Njombe kwa kukutanisha wadau mbalimbali ndani ya Mkoa wa Njombe ili kutoa fursa ya uchangiaji na uwezeshaji wa watoto wenye mahitaji mbalimbali.

Matangazo

  • Ujio wa Mwenge wa Uhuru 2025, bado siku 13 April 19, 2025
  • Ujio wa Mwenge wa Uhuru 2025, bado siku 12. April 20, 2025
  • Ujio wa Mwenge wa Uhuru 2025, bado siku 11. April 21, 2025
  • Ujio wa Mwenge wa Uhuru 2025, bado siku 10. April 22, 2025
  • Fungua

Habari Mpya

  • Wataalamu na viongozi watakiwa kusimamia upatikanaji na utoaji wa huduma za chanjo.

    April 25, 2025
  • Makambako yang'ara katika tuzo za Afya ya Usafi wa Mazingira ngazi ya Halmashauri za Miji.

    April 09, 2025
  • Jumla ya Miti 15,000 kupandwa Halmashauri ya Mji Makambako kuelekea siku ya Miti duniani mwaka 2025.

    March 15, 2025
  • Maadhimisho ya siku ya wanawake duniani 2025 Mkoa wa Njombe, Mila kandamizi zaelezwa kuwa kikwazo cha ustawi na uwezeshaji

    March 09, 2025
  • Fungua

Video

Shule mpya ya Mbugani Kitandililo sekondari kupitia mradi wa SEQUIP
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Fursa za Usafirishaji
  • Orodha ya Madiwani
  • Uzalishaji wa Umeme wa Upepo
  • Organisation Structure
  • Fursa za Biashara
  • By Laws
  • Permanent Committee

Tovuti Mashuhuri

  • Tovuti ya Ikulu ya Rais
  • Tovuti ya Ofisi ya Utumishi
  • Tovuti ya TAMISEMI
  • Tovuti ya Ofisi ya Takwimu ya Taifa (NBS)
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Open Data Tanzania

Wasomaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Makambako Town Council

    Anuani ya Posta: P.O.BOX 405 Makambako

    Simu ya mezani: 026-2730044

    Simu ya Kiganjani: 0785635383

    Barua pepe: td@makambakotc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Haki miliki ©2017 Halmashauri ya Mji Makambako. Haki zote zimehifadhiwa