• Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
HALMASHAURI YA MJI WA MAKAMBAKO
HALMASHAURI YA MJI WA MAKAMBAKO

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA HALMASHAURI YA MJI WA MAKAMBAKO

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Ardhi na maliasili
      • Raslimali watu na Utawala
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Usafi na mazingira
      • Elimu ya Msingi
      • Ujenzi na Uokoaji
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Elimu ya Sekondari
      • Kilimo, Ushirika na umwagiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maji
    • Vitengo
      • Sheria
      • ICT and Public relations
      • Ugavi na Manunuzi
      • Mkaguzi wa ndani
      • Ufugaji Nyuki
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma ya Afya
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Huduma za Jamii
      • Kamati ya Maadili
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Mipango Miji na Mazingira
    • Ratiba
      • Ratiba ya kumwona Mwenyekiti wa Halmashauri
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
  • Miradi
    • Miradi iliyo kwenye Mpango
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Ripoti mbalimbali
    • Mikataba
    • Mpango Mkakati
    • Hatua
    • Fomu za maombi
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Hotuba
    • Habari Mpya
    • Matukio
    • jarida la mji

KAMATI YA FEDHA NA UONGOZI YAAGIZA UTHAMINISHAJI WA NGUVU ZA WANANCHI KATIKA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAENDELEO.

Tarehe iliyowekwa: October 9th, 2022

Kamati ya Fedha na Uongozi imeziagiza kamati za ujenzi kuthaminisha nguvu za wananchi zinazotumika katika utekelezaji wa miradi ya Maendeleo na kuziainisha kwenye taarifa za miradi ili kupata gharama halisi ya mradi.

Agizo hilo limetolewa leo katika ziara ya ukaguzi,usimamizi na ufuatiliaji wa utekelezaji wa miradi ya maendeleo kwa kipindi cha robo ya kwanza kwa mwaka wa fedha 2022/2023,katika Kata ya Makambako,Utengule na Kitisi katika  Halmashauri ya Mji Makambako.

Akizungumza na wajumbe wa Kamati ya Ujenzi wa Zahanati ya Kijiji cha Ikelu,Kamati ya Ujenzi ya Shule ya Sekondari Mtimbwe na Kamati ya ujenzi ya Shule ya Msingi Magongo,Mwenyekiti wa Kamati ya Fedha na Uongozi, Mhe. Hanana Mfikwa amesema kuwa,sababu kuu ya baadhi ya miradi inayotekelezwa kwa fedha kutoka Serikali Kuu kushindwa kukamilika kwa fedha zilizoletwa ni kukosekana kwa thamani ya nguvu za wananchi kulingana na soko.

“Miradi inajengwa kwa nguvu za wananchi na fedha kutoka Serikali kuu,gharama za nguvu za wananchi hazihesabiki siku nyingine unapewa fedha zile zile ujenge bila nguvu za wananchi unashindwa kukamilisha mradi, kila siku tunasikia kwenye redio Njombe wamejenga  kwa Mil.50 Iringa wamejenga kwa Mil 20 hawakuandika nguvu za wananchi,wakiletewa fedha hizo hizo bila nguvu za wananchi wanashindwa wanaambiwa wameiba kumbe gharama ya mradi haikuwa halisi”,alisema Mhe. Hanana.

Ametoa rai kwa watendaji wote na wasimamizi wa miradi pamoja na watunza stoo kuandika kila kitu kinachofanyika kwenye mradi,ikiwa ni pamoja na taarifa ya mapokezi ya vifaa vilivyonunuliwa kwa fedha za  Serikali kuu au wananchi,kwa kuonyesha mchanganuo wa gharama halisi za vifaa na kazi zilizofanywa na wananchi kwa thamani ya pesa.

Aidha Kamati ya Fedha na Uongozi imeipongeza Kamati ya Ujenzi ya Shule ya Sekondari ya Kitisi na Uongozi wa Kata ya Kitisi,kwa usimamizi mzuri wa ujenzi wa miundombinu  ya madarasa na maabara.

Kamati ya Fedha na Uongozi leo imekagua miradi mitano ya ujenzi wa Zahanati ya Kijiji cha Ikelu,Ujenzi wa bweni shule ya Sekondari ya Mtimbwe,Mnada katika Kijiji cha Utengule,Ujenzi wa madarasa matatu na vyoo shule ya Msingi Magongo na ujenzi wa jengo la utawala,Maabara tatu,madarasa nane,ofisi mbili na  choo matundu kumi katika Shule ya Sekondari Kitisi.

Matangazo

  • Kuitwa Kwenye Usaili septemba,2025 September 04, 2025
  • Tangazo la kazi 2024 March 11, 2024
  • Mkutano wa uhamasishaji zoezi la urasimishaji Kata ya Kitisi na Majengo juni 27 - 29,2024 May 28, 2024
  • Mkutano wa uhamasishaji zoezi la urasimishaji Kata ya Mjimwema May 28, 2024
  • Fungua

Habari Mpya

  • Mil. 350.8 za Mikopo ya 10% zimetolewa kwa vikundi 30 Halmashauri ya Mji Makambako,DC aagiza mikopo hiyo kuwa chanzo cha utajiri.

    August 14, 2025
  • MIL 350.8 ZA MIKOPO YA 10% ZATOLEWA KWA AWAMU YA PILI KWA MWAKA 2024/2025.

    August 01, 2025
  • Wataalamu na viongozi watakiwa kusimamia upatikanaji na utoaji wa huduma za chanjo.

    April 25, 2025
  • Makambako yang'ara katika tuzo za Afya ya Usafi wa Mazingira ngazi ya Halmashauri za Miji.

    April 09, 2025
  • Fungua

Video

Shule mpya ya Mbugani Kitandililo sekondari kupitia mradi wa SEQUIP
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Fursa za Usafirishaji
  • Orodha ya Madiwani
  • Uzalishaji wa Umeme wa Upepo
  • Organisation Structure
  • Fursa za Biashara
  • By Laws
  • Permanent Committee

Tovuti Mashuhuri

  • Tovuti ya Ikulu ya Rais
  • Tovuti ya Ofisi ya Utumishi
  • Tovuti ya TAMISEMI
  • Tovuti ya Ofisi ya Takwimu ya Taifa (NBS)
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Open Data Tanzania

Wasomaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Makambako Town Council

    Anuani ya Posta: P.O.BOX 405 Makambako

    Simu ya mezani: 026-2730044

    Simu ya Kiganjani: 0785635383

    Barua pepe: td@makambakotc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Haki miliki ©2017 Halmashauri ya Mji Makambako. Haki zote zimehifadhiwa