• Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
HALMASHAURI YA MJI WA MAKAMBAKO
HALMASHAURI YA MJI WA MAKAMBAKO

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA HALMASHAURI YA MJI WA MAKAMBAKO

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Ardhi na maliasili
      • Raslimali watu na Utawala
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Usafi na mazingira
      • Elimu ya Msingi
      • Ujenzi na Uokoaji
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Elimu ya Sekondari
      • Kilimo, Ushirika na umwagiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maji
    • Vitengo
      • Sheria
      • ICT and Public relations
      • Ugavi na Manunuzi
      • Mkaguzi wa ndani
      • Ufugaji Nyuki
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma ya Afya
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Huduma za Jamii
      • Kamati ya Maadili
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Mipango Miji na Mazingira
    • Ratiba
      • Ratiba ya kumwona Mwenyekiti wa Halmashauri
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
  • Miradi
    • Miradi iliyo kwenye Mpango
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Ripoti mbalimbali
    • Mikataba
    • Mpango Mkakati
    • Hatua
    • Fomu za maombi
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Hotuba
    • Habari Mpya
    • Matukio
    • jarida la mji

Kamati ya Fedha na Uongozi,yazindua kilimo cha parachichi shuleni.

Tarehe iliyowekwa: March 3rd, 2023

Na. Lina Sanga

Kamati ya Fedha na Uongozi ya Halmashauri ya Mji Makambako  jana imezindua  zoezi la upandaji wa miti ya  parachichi   shuleni ,kwa kupanda miti ya parachichi shule ya Sekondari Makambako,kwa lengo la kuboresha lishe ya wanafunzi,kukuza uchumi wa shule na kujenga dhana ya kujitegemea.

Akizungumza na wanafunzi wa shule ya sekondari Makambako pamoja na Walimu wa shule zote za Msingi na Sekondari za Serikali na binafsi waliohudhuria uzinduzi wa zoezi la upandaji wa miti ya parachichi shuleni,uliofanyika jana katika shule ya Sekondari ya Makambako,Mwenyekiti wa Halmashauri ya Mji Makambako,Mhe. Hanana Mfikwa amesema kuwa ndani ya parachichi lishe,uchumi na mambo mengine yanapatikana kwani bila lishe hakuna mwanafunzi atayeweza kusoma vizuri.

Amesema kuwa,miti ya parachichi itayopandwa kila shule italeta manufaa kwa wanafunzi na shule kwani zao hilo kwa sasa linauhitaji mkubwa katika soko la dunia, lakini pia wanafunzi wanaweza kutumia tunda hilo kwenye chakula kwa muda mrefu endapo itahudumiwa vizuri.

Ameongeza kuwa,Halmashauri imeamua kupanda parachichi shuleni ili kutoa elimu kwa wanafunzi na kuwawezesha kupata ujuzi wa kilimo cha parachichi,ili baada ya kuhitimu masomo na wakati wa likizo waweze kupanda miti ya parachichi nyumbani kwao ambayo itawapa ajira na kipato cha muda mrefu baada ya miaka 3 hadi 5.

Ametoa wito kwa walimu kupanda miti waliyokabidhiwa kabla ya msimu wa mfua kuisha na kuwagawia miti ya kuihudumia wanafunzi na kila mwanafunzi ahakikishe anauhudumia mti huo kwa kumwagilia maji kadri inavyohitajika.

Naye Kenneth Haule,Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji Makambako ametoa rai kwa walimu na wanafunzi kujitoa kwa ajili ya utekelezaji wa kilimo cha parachichi katika shule zao,kwa kutumia rasilimali zinazopatikana katika maeneo yao badala ya  kuibua changamoto zisizo na msingi ili kukwamisha zoezi hilo kama vile ukosefu wa maji ya kutosha shuleni na samadi.

Amesema kuwa, ipo haja kwa jamii kuondoa dhana ya kuwatumikisha wanafunzi katika utendaji wa kazi za miradi mbalimbali inayoanzishwa shuleni,na kujenga dhana ya kujitegemea kwa wanafunzi kushiriki shughuli mbalimbali za miradi ya shule kwa kubeba kidumu cha maji kwa ajili ya kumwagilia mbogamboga na miti ya matunda ilyopo shule  pamoja na kumjengea mtoto uwezo wa kufanya shughuli ndogondogo na kuongeza ujuzi.

Halmashauri ya Mji Makambako imetoa jumla ya miche 5,901 yenye thamani ya mil. 17.7 kwa shule zote zilizopo Katika Halmashauri ya Mji Makambako,kulingana na ukubwa wa eneo la shule, ambapo shule zenye maeneo makubwa zimepewa miche kuanzia 50 hadi 200.

Kauli mbiu ya zoezi la upandaji wa miti ya parachichi katika shule za msingi na sekondari,katika Halmashauri ya Mji Makambako inasema” BORESHA LISHE,KUZA UCHUMI WA SHULE,JENGA DHANA YA KUJITEGEMEA”.

 

Matangazo

  • Ujio wa Mwenge wa Uhuru 2025, bado siku 13 April 19, 2025
  • Ujio wa Mwenge wa Uhuru 2025, bado siku 12. April 20, 2025
  • Ujio wa Mwenge wa Uhuru 2025, bado siku 11. April 21, 2025
  • Ujio wa Mwenge wa Uhuru 2025, bado siku 10. April 22, 2025
  • Fungua

Habari Mpya

  • Wataalamu na viongozi watakiwa kusimamia upatikanaji na utoaji wa huduma za chanjo.

    April 25, 2025
  • Makambako yang'ara katika tuzo za Afya ya Usafi wa Mazingira ngazi ya Halmashauri za Miji.

    April 09, 2025
  • Jumla ya Miti 15,000 kupandwa Halmashauri ya Mji Makambako kuelekea siku ya Miti duniani mwaka 2025.

    March 15, 2025
  • Maadhimisho ya siku ya wanawake duniani 2025 Mkoa wa Njombe, Mila kandamizi zaelezwa kuwa kikwazo cha ustawi na uwezeshaji

    March 09, 2025
  • Fungua

Video

Shule mpya ya Mbugani Kitandililo sekondari kupitia mradi wa SEQUIP
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Fursa za Usafirishaji
  • Orodha ya Madiwani
  • Uzalishaji wa Umeme wa Upepo
  • Organisation Structure
  • Fursa za Biashara
  • By Laws
  • Permanent Committee

Tovuti Mashuhuri

  • Tovuti ya Ikulu ya Rais
  • Tovuti ya Ofisi ya Utumishi
  • Tovuti ya TAMISEMI
  • Tovuti ya Ofisi ya Takwimu ya Taifa (NBS)
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Open Data Tanzania

Wasomaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Makambako Town Council

    Anuani ya Posta: P.O.BOX 405 Makambako

    Simu ya mezani: 026-2730044

    Simu ya Kiganjani: 0785635383

    Barua pepe: td@makambakotc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Haki miliki ©2017 Halmashauri ya Mji Makambako. Haki zote zimehifadhiwa