• Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
HALMASHAURI YA MJI WA MAKAMBAKO
HALMASHAURI YA MJI WA MAKAMBAKO

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA HALMASHAURI YA MJI WA MAKAMBAKO

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Ardhi na maliasili
      • Raslimali watu na Utawala
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Usafi na mazingira
      • Elimu ya Msingi
      • Ujenzi na Uokoaji
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Elimu ya Sekondari
      • Kilimo, Ushirika na umwagiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maji
    • Vitengo
      • Sheria
      • ICT and Public relations
      • Ugavi na Manunuzi
      • Mkaguzi wa ndani
      • Ufugaji Nyuki
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma ya Afya
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Huduma za Jamii
      • Kamati ya Maadili
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Mipango Miji na Mazingira
    • Ratiba
      • Ratiba ya kumwona Mwenyekiti wa Halmashauri
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
  • Miradi
    • Miradi iliyo kwenye Mpango
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Ripoti mbalimbali
    • Mikataba
    • Mpango Mkakati
    • Hatua
    • Fomu za maombi
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Hotuba
    • Habari Mpya
    • Matukio
    • jarida la mji

Kikundi cha By nature tech cha Mtaa wa Mlando chakabidhiwa mashine za uchomeleaji kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi, Vijana, Ajira na Wenye ulemavu.

Tarehe iliyowekwa: November 25th, 2022

Na. Lina Sanga

Kikundi cha Vijana cha By Nature tech kutoka katika Mtaa wa Mlando, Kata ya Mjimwema katika Halmashauri ya Mji Makambako, kinachojishughulisha na kazi ya uchomeleaji vyuma kimekabidhiwa mashine tatu za kuchomelea    na mashine tatu za kukatia vyuma,zilizotolewa na Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi,Vijana Ajira na Wenye ulemavu kupitia Ofisi ya Rais - TAMISEMI ikiwa ni sehemu ya kuwawezesha vijana kujiajiri.

Akitoa taarifa ya mapokezi ya vifaa hivyo katika hafla ya makabidhiano iliyofanyika leo katika ukumbi wa mikutano wa Halmashauri ya Mji Makambako, Mkuu wa idara ya maendeleo ya jamii, Bi. Zuena Ungele amesema kuwa Ofisi ya Rais – TAMISEMI ilitoa maelekezo juu ya kutuma taarifa za vikundi vinavyofanya shughuli za uchomeleaji, kikundi cha By nature tech ni moja ya kati ya vikundi vilivyochaguliwa kuwa mnufaika wa mashine  hizo zilizotolewa na Ofisi Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi,Vijana,Ajira na Wenye ulemavu kwa Halmashauri zote nchini.

Amesema kuwa, kikundi hicho chenye jumla ya vijana watano kilianzishwa mwaka 2021 na walipata mkopo wa mil 5 inayotolewa na Halmashauri kwa vikundi vya Wanawake, Vijana na watu wenye ulemavu na kimefanikiwa kurejesha jumla ya shilingi mil 4.6 ndani ya muda na mnamo novemba 30,mwaka huu wanakamilisha deni lote.

Kabla ya kukabidhi mashine hizo,Mwenyekiti wa Halmashauri ya Mji Makambako, Mhe. Hanana Mfikwa ameishukuru Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi,Vijana,Ajira na Wenye ulemavu na Ofisi ya Rais – TAMISEMI kwa kutoa mashine hizo ili kuwawezesha vijana kujiajiri.

Amewapongeza vijana hao kwa kujitambua na kuweza kufanya marejesho ya mkopo vizuri na kuwataka kuendelea kutumia fedha wanazozipata kwa malengo,na kujiepusha na matumizi mabaya ya fedha wanazozipata kwa kufuata vipaumbele walivyojiwekea kufikia malengo yao.

Ametoa wito kwa Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji Makambako kukitumia kikundi hicho katika kazi mbalimbali za uchomeleaji katika miradi inayotekelezwa na Halmashauri,ili kukiwezesha kikundi hicho kupata fedha na kuwataka vijana kuwa wabunifu na kufanya kazi zilizo ndani ya uwezo wao badala ya kazi za kufikirika.

Elichalido Ng’olo mmoja kati ya vijana watano wanaounda kikundi cha By nature tech, amemshukuru Rais wa jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan,Makamu wa Rais,Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi, Vijana,Ajira na Wenye ulemavu na Ofisi ya Rais – TAMISEMI kwa kuwapa mashine za uchomeleaji ambazo zitawasaidia kufanya kazi kwa uhakika kwani vifaa vya zamani vimechakaa.

Ametoa hamasa kwa  vijana kuunda vikundi na kuaminiana ili waweze kupata mikopo kutoka Halmashauri, na kutumia fedha hizo kufanikisha malengo waliyojiwekea kwani fedha za mikopo ya Halmashauri zipo.

Mashine walizokabidhiwa Vijana wa kikundi cha by nature tech.


Vijana wanaounda kikundi cha by nature tech.

Matangazo

  • Ujio wa Mwenge wa Uhuru 2025, bado siku 13 April 19, 2025
  • Ujio wa Mwenge wa Uhuru 2025, bado siku 12. April 20, 2025
  • Ujio wa Mwenge wa Uhuru 2025, bado siku 11. April 21, 2025
  • Ujio wa Mwenge wa Uhuru 2025, bado siku 10. April 22, 2025
  • Fungua

Habari Mpya

  • Wataalamu na viongozi watakiwa kusimamia upatikanaji na utoaji wa huduma za chanjo.

    April 25, 2025
  • Makambako yang'ara katika tuzo za Afya ya Usafi wa Mazingira ngazi ya Halmashauri za Miji.

    April 09, 2025
  • Jumla ya Miti 15,000 kupandwa Halmashauri ya Mji Makambako kuelekea siku ya Miti duniani mwaka 2025.

    March 15, 2025
  • Maadhimisho ya siku ya wanawake duniani 2025 Mkoa wa Njombe, Mila kandamizi zaelezwa kuwa kikwazo cha ustawi na uwezeshaji

    March 09, 2025
  • Fungua

Video

Shule mpya ya Mbugani Kitandililo sekondari kupitia mradi wa SEQUIP
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Fursa za Usafirishaji
  • Orodha ya Madiwani
  • Uzalishaji wa Umeme wa Upepo
  • Organisation Structure
  • Fursa za Biashara
  • By Laws
  • Permanent Committee

Tovuti Mashuhuri

  • Tovuti ya Ikulu ya Rais
  • Tovuti ya Ofisi ya Utumishi
  • Tovuti ya TAMISEMI
  • Tovuti ya Ofisi ya Takwimu ya Taifa (NBS)
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Open Data Tanzania

Wasomaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Makambako Town Council

    Anuani ya Posta: P.O.BOX 405 Makambako

    Simu ya mezani: 026-2730044

    Simu ya Kiganjani: 0785635383

    Barua pepe: td@makambakotc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Haki miliki ©2017 Halmashauri ya Mji Makambako. Haki zote zimehifadhiwa