• Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
HALMASHAURI YA MJI WA MAKAMBAKO
HALMASHAURI YA MJI WA MAKAMBAKO

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA HALMASHAURI YA MJI WA MAKAMBAKO

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Ardhi na maliasili
      • Raslimali watu na Utawala
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Usafi na mazingira
      • Elimu ya Msingi
      • Ujenzi na Uokoaji
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Elimu ya Sekondari
      • Kilimo, Ushirika na umwagiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maji
    • Vitengo
      • Sheria
      • ICT and Public relations
      • Ugavi na Manunuzi
      • Mkaguzi wa ndani
      • Ufugaji Nyuki
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma ya Afya
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Huduma za Jamii
      • Kamati ya Maadili
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Mipango Miji na Mazingira
    • Ratiba
      • Ratiba ya kumwona Mwenyekiti wa Halmashauri
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
  • Miradi
    • Miradi iliyo kwenye Mpango
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Ripoti mbalimbali
    • Mikataba
    • Mpango Mkakati
    • Hatua
    • Fomu za maombi
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Hotuba
    • Habari Mpya
    • Matukio
    • jarida la mji

Kiwanda cha idofi ujenzi hausimami -Mhe. Ummy Mwalimu

Tarehe iliyowekwa: October 24th, 2023

Na. Lina Sanga

Mhe Ummy Mwalimu,Waziri wa Afya amewahakikishia wakazi wa Mkoa wa Njombe kuwa hakuna kilichosimama katika ujenzi wa kiwanda cha mipira ya mikono cha MSD kilichopo Mtaa wa Idofi katika Halmashauri ya Mji Makambako.

Ametoa kauli hiyo leo katika ziara yake katika kiwanda hicho mara baada ya Mbunge wa jimbo la Makambako, Mhe. Deo Sanga kuhoji kuhusu ukamilishaji wa kiwanda hicho na aina ya bidhaa zitazozalishwa mbali na uzalishaji wa mipira ya mikono (gloves).

Mhe. Ummy amesema kuwa,chini ya Serikali ya awamu ya sita ya hakuna kilichosimama kwani ujenzi wa kiwanda hicho bado unaendelea na kwa mwaka huu kuna maendeleo makubwa ya mradi huo na Serikali kwa sasa imetoa Bil. 11 na  itaendelea kutoa fedha kwa ajili ya ukamilishaji wa miradi ya maendeleo yote iliyoanzishwa katika Serikali ya awamu ya tano.

Pia,katika sekta ya Afya wamedhamiria kuongeza uzalishaji wa ndani wa dawa,vifaa tiba na bidhaa nyingine za Afya ili kupunguza uhaba wa dawa na vifaa tiba, kwani kwa sasa bidhaa hizo asilimia 85 zinaagizwa nje kwa gharama kubwa na zinafika kwa kuchelewa nchini hivyo kusababisha uhaba wa dawa na vifaa tiba.

Amesema kuwa, lengo  la Serikali kujenga viwanda vya dawa na vifaa tiba nchini ni kufikia  asilimia 50 ya bidhaa za Afya kununuliwa ndani ya nchi ifikapo 2030 kupitia Bohari kuu ya dawa (MSD) ambapo kwa  sasa ni asilimia 15 pekee za bidhaa za Afya zinanunuliwa ndani ya nchi.

Ameongeza kuwa ,kwa sasa kuna jumla ya viwanda 30 vya dawa na vifaa tiba na viwanda 11 vinafanya kazi ikiwa ni pamoja na viwanda viwili vya uzalishaji chupa Mil. 90 za maji tiba (dripu) na mahitaji ni Mil 24 hadi 26 ,hivyo maji tiba hayatanunuliwa tena nje bali yataanza kununuliwa nchini.

Amebainisha kuwa,Bohari ya dawa (MSD) katika bajeti ya mwaka 2021/2022  imenunua bidhaa za Afya zilizotengenezwa ndani ya nchi zenye thamani ya Bil 14. 1,bajeti ya mwaka 2022/2023 imenunua bidhaa za Afya zenye thamani ya Bil. 39.4 matarajio kwa sasa ni kuhakikisha  ununuzi wa bidhaa hizo kufikia  Bil. 50 ifikapo kipindi cha kufunga mwaka wa fedha wa Bunge.

Ametoa rai kwa Mbunge wa jimbo la Makambako kuridhia kiwanda hicho kuanza na uzalishaji wa mipira ya mikono kwa sasa na mapendekezo ya Kamati iliyopita katika kiwanda hicho yatajadiliwa katika kikao cha pamoja cha kamati za Bunge za  uwekezaji mitaji ya Umma, Afya na masuala ya UKIMWI, Hesabu za Serikali na Mbunge wa jimbo la Makambako.

Matangazo

  • Ujio wa Mwenge wa Uhuru 2025, bado siku 13 April 19, 2025
  • Ujio wa Mwenge wa Uhuru 2025, bado siku 12. April 20, 2025
  • Ujio wa Mwenge wa Uhuru 2025, bado siku 11. April 21, 2025
  • Ujio wa Mwenge wa Uhuru 2025, bado siku 10. April 22, 2025
  • Fungua

Habari Mpya

  • Wataalamu na viongozi watakiwa kusimamia upatikanaji na utoaji wa huduma za chanjo.

    April 25, 2025
  • Makambako yang'ara katika tuzo za Afya ya Usafi wa Mazingira ngazi ya Halmashauri za Miji.

    April 09, 2025
  • Jumla ya Miti 15,000 kupandwa Halmashauri ya Mji Makambako kuelekea siku ya Miti duniani mwaka 2025.

    March 15, 2025
  • Maadhimisho ya siku ya wanawake duniani 2025 Mkoa wa Njombe, Mila kandamizi zaelezwa kuwa kikwazo cha ustawi na uwezeshaji

    March 09, 2025
  • Fungua

Video

Shule mpya ya Mbugani Kitandililo sekondari kupitia mradi wa SEQUIP
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Fursa za Usafirishaji
  • Orodha ya Madiwani
  • Uzalishaji wa Umeme wa Upepo
  • Organisation Structure
  • Fursa za Biashara
  • By Laws
  • Permanent Committee

Tovuti Mashuhuri

  • Tovuti ya Ikulu ya Rais
  • Tovuti ya Ofisi ya Utumishi
  • Tovuti ya TAMISEMI
  • Tovuti ya Ofisi ya Takwimu ya Taifa (NBS)
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Open Data Tanzania

Wasomaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Makambako Town Council

    Anuani ya Posta: P.O.BOX 405 Makambako

    Simu ya mezani: 026-2730044

    Simu ya Kiganjani: 0785635383

    Barua pepe: td@makambakotc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Haki miliki ©2017 Halmashauri ya Mji Makambako. Haki zote zimehifadhiwa