• Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
HALMASHAURI YA MJI WA MAKAMBAKO
HALMASHAURI YA MJI WA MAKAMBAKO

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA HALMASHAURI YA MJI WA MAKAMBAKO

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Ardhi na maliasili
      • Raslimali watu na Utawala
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Usafi na mazingira
      • Elimu ya Msingi
      • Ujenzi na Uokoaji
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Elimu ya Sekondari
      • Kilimo, Ushirika na umwagiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maji
    • Vitengo
      • Sheria
      • ICT and Public relations
      • Ugavi na Manunuzi
      • Mkaguzi wa ndani
      • Ufugaji Nyuki
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma ya Afya
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Huduma za Jamii
      • Kamati ya Maadili
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Mipango Miji na Mazingira
    • Ratiba
      • Ratiba ya kumwona Mwenyekiti wa Halmashauri
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
  • Miradi
    • Miradi iliyo kwenye Mpango
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Ripoti mbalimbali
    • Mikataba
    • Mpango Mkakati
    • Hatua
    • Fomu za maombi
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Hotuba
    • Habari Mpya
    • Matukio
    • jarida la mji

Mafunzo ya mradi wa BOOST kwa timu za utekelezaji ngazi za Mikoa na Halmashauri Nyanda za juu kusini yaanza rasmi leo Mkoani Iringa.

Tarehe iliyowekwa: December 16th, 2022


Na. Lina Sanga

Iringa

Mikoa mitatu ya Nyanda za juu Kusini imeanza mafunzo ya Mradi wa BOOST leo yanayotolewa na Ofisi ya Rais –TAMISEMI kwa kushirikiana na Wizara ya Elimu,Sayansi na Teknolojia Mkoani Iringa.

Akifungua mafunzo hayo Mkurugenzi wa michezo Ofisi ya Rais –TAMISEMI, Yusuph Singo ambaye pia ni mratibu wa mafunzo hayo amesema kuwa,mradi wa BOOST ni mradi wa kuimarisha ujifunzaji shule za  awali na msingi unaofadhiliwa na benki ya dunia na unatarajiwa kutumia jumla ya trillion 1.15.

Amesema kuwa kupitia fedha hizo jumla ya madarasa 12,000 yanatarajiwa kujengwa katika shule za  awali na msingi kwa miaka mitano ambapo kwa mwaka mmoja jumla ya madarasa 3,000 yatajengwa,kufunga vifaa vya TEHAMA kwenye vituo vya walimu na shule za msingi 800 na utekelezaji wa mradi huo umeanza mwaka huu 2022/2023 na unatarajiwa kumalizika 2025/2026 kwa utaratibu wa lipa kulingana na matokeo.

Ameongeza kuwa mradi wa BOOST una jumla ya afua 8 za utekelezaji ikiwa ni pamoja na afua ya Mamlaka za Serikali za Mitaa kutekeleza mafunzo endelevu ya walimu kazini,Upatikanaji wa vifaa vya kufundishia na kujifunzia,Kuongeza uandikishaji wa wanafunzi wa darasa la awali,Mpango wa shule salama kwa shule 6,000 na Mpango wa ujenzi wa miundombinu ya madarasa na vyoo.

Ametoa wito kwa timu za utekelezaji wa mradi huo ngazi za Mikoa na Halmashauri kuhakikisha wanasimamia miradi kwa kuzingatia ubora na viwango vinavyokubalika,kwani endapo utekelezaji wa miradi hiyo utakuwa hauridhishi fedha za utekelezaji hazitatolewa.

Mikoa ya Nyanda za juu Kusini iliyoshiriki mafunzo hayo yaliyoanza kutolewa leo na yatahitimishwa kesho ni Mkoa wa Iringa,Njombe na Ruvuma kwa kuhusishwa washiriki 250 kutoka ngazi za Mikoa na  Halmashauri.

Matangazo

  • Ujio wa Mwenge wa Uhuru 2025, bado siku 13 April 19, 2025
  • Ujio wa Mwenge wa Uhuru 2025, bado siku 12. April 20, 2025
  • Ujio wa Mwenge wa Uhuru 2025, bado siku 11. April 21, 2025
  • Ujio wa Mwenge wa Uhuru 2025, bado siku 10. April 22, 2025
  • Fungua

Habari Mpya

  • Wataalamu na viongozi watakiwa kusimamia upatikanaji na utoaji wa huduma za chanjo.

    April 25, 2025
  • Makambako yang'ara katika tuzo za Afya ya Usafi wa Mazingira ngazi ya Halmashauri za Miji.

    April 09, 2025
  • Jumla ya Miti 15,000 kupandwa Halmashauri ya Mji Makambako kuelekea siku ya Miti duniani mwaka 2025.

    March 15, 2025
  • Maadhimisho ya siku ya wanawake duniani 2025 Mkoa wa Njombe, Mila kandamizi zaelezwa kuwa kikwazo cha ustawi na uwezeshaji

    March 09, 2025
  • Fungua

Video

Shule mpya ya Mbugani Kitandililo sekondari kupitia mradi wa SEQUIP
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Fursa za Usafirishaji
  • Orodha ya Madiwani
  • Uzalishaji wa Umeme wa Upepo
  • Organisation Structure
  • Fursa za Biashara
  • By Laws
  • Permanent Committee

Tovuti Mashuhuri

  • Tovuti ya Ikulu ya Rais
  • Tovuti ya Ofisi ya Utumishi
  • Tovuti ya TAMISEMI
  • Tovuti ya Ofisi ya Takwimu ya Taifa (NBS)
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Open Data Tanzania

Wasomaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Makambako Town Council

    Anuani ya Posta: P.O.BOX 405 Makambako

    Simu ya mezani: 026-2730044

    Simu ya Kiganjani: 0785635383

    Barua pepe: td@makambakotc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Haki miliki ©2017 Halmashauri ya Mji Makambako. Haki zote zimehifadhiwa