• Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
HALMASHAURI YA MJI WA MAKAMBAKO
HALMASHAURI YA MJI WA MAKAMBAKO

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA HALMASHAURI YA MJI WA MAKAMBAKO

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Ardhi na maliasili
      • Raslimali watu na Utawala
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Usafi na mazingira
      • Elimu ya Msingi
      • Ujenzi na Uokoaji
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Elimu ya Sekondari
      • Kilimo, Ushirika na umwagiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maji
    • Vitengo
      • Sheria
      • ICT and Public relations
      • Ugavi na Manunuzi
      • Mkaguzi wa ndani
      • Ufugaji Nyuki
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma ya Afya
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Huduma za Jamii
      • Kamati ya Maadili
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Mipango Miji na Mazingira
    • Ratiba
      • Ratiba ya kumwona Mwenyekiti wa Halmashauri
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
  • Miradi
    • Miradi iliyo kwenye Mpango
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Ripoti mbalimbali
    • Mikataba
    • Mpango Mkakati
    • Hatua
    • Fomu za maombi
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Hotuba
    • Habari Mpya
    • Matukio
    • jarida la mji

Makamu wa Rais aweka jiwe la msingi kiwanda cha MSD Idofi,aagiza ujenzi ukamilike na kuanza uzalishaji ifikapo januari mosi,2024.

Tarehe iliyowekwa: October 26th, 2023

Na. Lina Sanga

Makamu wa Rais wa jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Mhe. Dkt Philip Mpango ameuagiza uongozi wa Bohari ya Dawa nchini (MSD),kuhakikisha shughuli za uzalishaji katika kiwanda cha kutengeneza mipira ya mikono(gloves) kilichopo Mtaa wa Idofi,katika Halmashauri ya Mji Makambako unaanza kufanyika januari mosi,2024.

Dkt. Mpango ametoa agizo hilo leo mara baada ya kuweka jiwe la msingi katika kiwanda hicho,na kuagiza uongozi wa kiwanda hicho pamoja na Wizara ya Afya kuandaa taarifa ya kina inayoeleza sababu ya kutofungwa kwa mitambo iliyopo kiwandani hapo kwa miaka miwili pamoja na hoja za Mkaguzi mkuu wa Serikali  (CAG).

Amesema kuwa changamoto za kiutendaji zilizopo katika kiwanda hicho zishughulikiwe na kuwahakikishia wakazi wa Idofi kuwa kiwanda hicho hakitahamishwa kitaendelea kuwa Idofi na kuzalisha dawa,vifaa tiba na vitendanishi.

Amemuagiza Naibu Waziri wa Wizara ya Afya na Naibu Waziri wa ofisi ya Rais TAMISEMI, kuhakikisha bidhaa zingine zinazalishwa katika kiwanda hicho kwa kutumia miundombinu iliyopo kiwandani hapo kama maji tiba na vitendanishi vya maabara ili kuongeza tija.

Aidha,ameitaka kampuni tanzu ya MSD kuzingatia misingi ya kibiashara,ili waweze kujitegemea katika uzalishaji kutoka katika kiwanda cha Idofi na viwanda vingine na kuagiza uongozi wa kiwanda cha Idofi kuongeza ajira za wananchi wa Idofi katika kiwanda hicho hasa wanawake.

Ameagiza Wakala wa barabara Mijini na Vijijini  (TARURA) kufanya tathmini ya  ujenzi wa barabara ya lami kuelekea eneo la kiwanda inayokadiriwa kugharimu Bil. 1.4 na kuifikisha ofisi ya Rais TAMISEMI kwa ajili ya kupata fedha ya utekelezaji wa ujenzi huo.

Matangazo

  • Ujio wa Mwenge wa Uhuru 2025, bado siku 13 April 19, 2025
  • Ujio wa Mwenge wa Uhuru 2025, bado siku 12. April 20, 2025
  • Ujio wa Mwenge wa Uhuru 2025, bado siku 11. April 21, 2025
  • Ujio wa Mwenge wa Uhuru 2025, bado siku 10. April 22, 2025
  • Fungua

Habari Mpya

  • Wataalamu na viongozi watakiwa kusimamia upatikanaji na utoaji wa huduma za chanjo.

    April 25, 2025
  • Makambako yang'ara katika tuzo za Afya ya Usafi wa Mazingira ngazi ya Halmashauri za Miji.

    April 09, 2025
  • Jumla ya Miti 15,000 kupandwa Halmashauri ya Mji Makambako kuelekea siku ya Miti duniani mwaka 2025.

    March 15, 2025
  • Maadhimisho ya siku ya wanawake duniani 2025 Mkoa wa Njombe, Mila kandamizi zaelezwa kuwa kikwazo cha ustawi na uwezeshaji

    March 09, 2025
  • Fungua

Video

Shule mpya ya Mbugani Kitandililo sekondari kupitia mradi wa SEQUIP
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Fursa za Usafirishaji
  • Orodha ya Madiwani
  • Uzalishaji wa Umeme wa Upepo
  • Organisation Structure
  • Fursa za Biashara
  • By Laws
  • Permanent Committee

Tovuti Mashuhuri

  • Tovuti ya Ikulu ya Rais
  • Tovuti ya Ofisi ya Utumishi
  • Tovuti ya TAMISEMI
  • Tovuti ya Ofisi ya Takwimu ya Taifa (NBS)
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Open Data Tanzania

Wasomaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Makambako Town Council

    Anuani ya Posta: P.O.BOX 405 Makambako

    Simu ya mezani: 026-2730044

    Simu ya Kiganjani: 0785635383

    Barua pepe: td@makambakotc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Haki miliki ©2017 Halmashauri ya Mji Makambako. Haki zote zimehifadhiwa