• Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
HALMASHAURI YA MJI WA MAKAMBAKO
HALMASHAURI YA MJI WA MAKAMBAKO

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA HALMASHAURI YA MJI WA MAKAMBAKO

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Ardhi na maliasili
      • Raslimali watu na Utawala
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Usafi na mazingira
      • Elimu ya Msingi
      • Ujenzi na Uokoaji
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Elimu ya Sekondari
      • Kilimo, Ushirika na umwagiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maji
    • Vitengo
      • Sheria
      • ICT and Public relations
      • Ugavi na Manunuzi
      • Mkaguzi wa ndani
      • Ufugaji Nyuki
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma ya Afya
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Huduma za Jamii
      • Kamati ya Maadili
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Mipango Miji na Mazingira
    • Ratiba
      • Ratiba ya kumwona Mwenyekiti wa Halmashauri
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
  • Miradi
    • Miradi iliyo kwenye Mpango
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Ripoti mbalimbali
    • Mikataba
    • Mpango Mkakati
    • Hatua
    • Fomu za maombi
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Hotuba
    • Habari Mpya
    • Matukio
    • jarida la mji

Mbinu za Kibenki kutumika katika ufuatiliaji wa Madeni ya Mkopo wa 10% wa Vikundi vya Wanawake,Vijana na Watu wenye Ulemavu..

Tarehe iliyowekwa: June 14th, 2022

Na. Lina Sanga

Watendaji wa halmashauri wametakiwa kuwasilisha orodha za wadaiwa wa  mikopo ya asilimia kumi ya  vikundi vya  wanawake,vijana na watu wenye ulemavu inayokopeshwa na halmashauri,ikionyesha tarehe za mikopo,muda wa deni na kata wanazotoka wadaiwa hao na kuziwasilisha kwa Katibu Tawala wa Mkoa ili kuongeza msukumo wa kukusanya madeni hayo.

 Agizo hilo limetolewa leo na Mkuu wa Mkoa wa Njombe ,Mhe.Waziri Kindamba katika mkutano maalumu wa baraza la Madiwani la kuwasilish mpango kazi na majibu ya Menejimenti kwa ajili ya utekelezaji wa hoja za Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa hesabu za Serikali kuishia Juni 30,2021.

Mhe.Kindamba amesema kuwa katika hoja ambazo hazijafungwa na zinatakiwa kufanyiwa kazi na mamlaka nyingine na hoja  ambazo zimefungwa,halmashauri ya Mji Makambako imefanya vizuri sana katika kupunguza au kumaliza hoja hizo na jitihada hizo ziendelee hasa katika ukusanyaji wa deni la mikopo ya wanawake ,vijana na watu wenye ulemavu,kwa kutumia mbinu za kibenki katika utoaji mikopo hiyo na kuweka mikakati madhubuti kuhakikisha madeni yote  yanalipwa kwa wakati uliopangwa.

“Sisi waswahili utamaduni wa kulipa madeni haujalimwa vizuri ndani yetu na mtu akipata fedha za namna hii anaona ni haki yake,hajui kama anawajibika kuzirudisha ili wengine waweze kukopeshwa,kila mtu ana mikakati ya namna ya kuhakikisha madeni yanalipwa wenzetu wa benki wana mikakati mizuri sana katika kuhakikisha madeni yanalipwa kwa wakati uliopangwa kama ni ndani ya siku thelathini,mkopo ukianza kwenda siku sitini mkopo unaenda kwenye matata na ukifika siku tisini unakua ni matata zaidi”,alisema Kindamba.

 Amemtaka Mkurugenzi kupanga watu kwenye vitengo vya mikopo kwani waswahili kukopa harusi kulipa matanga,hivyo katika vitengo hivyo  watu wa kukopesha na watu wa kudai madeni  ni muhimu sana na itasaidia katika kusimamia urejeshwaji wa madeni kwa wakati,kwani kudai pia inategemea ujuzi wa mtu katika kudai pasipo kuwa na huruma.

Aidha Mhe. Kindamba amesema elimu ya fedha ni muhimu kwa vikundi hivyo ili kuwaelimisha namna ya kutumia fedha hizo katika malengo yaliyokusudia,kwani wengine hawana elimu ya mikopo wakipata mikopo wanaitumia katika malengo mengine kama kuoa na matumizi mengine.

Ametoa wito kwa Mkurugenzi wa halmashauri ya Mji Makambako kuwakabidhi Madiwani katika ufuatiliaji wa vikundi vya wanawake,vijana na watu wenye ulemavu na kuhakikisha madeni yanalipwa,katika usimamizi na ukusanyaji wa mapato kwani Mji wa Makambako ni kituo cha biashara hivyo makusanyo ya mapato yaendane na hadhi ya Mji.

Pia ametoa wito kwa wananchi wote kujiandaa kushiriki zoezi la Sensa ya watu na makazi kikamilifu itayofanyika Agosti 23,2022 kwa maendeleo endelevu ya Taifa letu pamoja na kujitokeza kupata Chanjo ya Uviko 19.

Mwisho ametoa pongezi kwa halmashauri ya Mji Makambako kwa kupata hati safi ya ufungaji wa hesabu za Serikali,usimamizi  wa utekelezaji wa maelekezo yanayotolewa na Serikali,utekelezaji wa Miradi,Utoaji wa huduma kwa wananchi pamoja na kusimamia miongozo mbalimbali iliyowekwa, pamoja na ukamilishaji wa zoezi la anwani za makazi na postikodi kwa kutekeleza zoezi hilo ndani ya muda na kukamilisha kwa asilimia mia moja.

Matangazo

  • Ujio wa Mwenge wa Uhuru 2025, bado siku 13 April 19, 2025
  • Ujio wa Mwenge wa Uhuru 2025, bado siku 12. April 20, 2025
  • Ujio wa Mwenge wa Uhuru 2025, bado siku 11. April 21, 2025
  • Ujio wa Mwenge wa Uhuru 2025, bado siku 10. April 22, 2025
  • Fungua

Habari Mpya

  • Wataalamu na viongozi watakiwa kusimamia upatikanaji na utoaji wa huduma za chanjo.

    April 25, 2025
  • Makambako yang'ara katika tuzo za Afya ya Usafi wa Mazingira ngazi ya Halmashauri za Miji.

    April 09, 2025
  • Jumla ya Miti 15,000 kupandwa Halmashauri ya Mji Makambako kuelekea siku ya Miti duniani mwaka 2025.

    March 15, 2025
  • Maadhimisho ya siku ya wanawake duniani 2025 Mkoa wa Njombe, Mila kandamizi zaelezwa kuwa kikwazo cha ustawi na uwezeshaji

    March 09, 2025
  • Fungua

Video

Shule mpya ya Mbugani Kitandililo sekondari kupitia mradi wa SEQUIP
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Fursa za Usafirishaji
  • Orodha ya Madiwani
  • Uzalishaji wa Umeme wa Upepo
  • Organisation Structure
  • Fursa za Biashara
  • By Laws
  • Permanent Committee

Tovuti Mashuhuri

  • Tovuti ya Ikulu ya Rais
  • Tovuti ya Ofisi ya Utumishi
  • Tovuti ya TAMISEMI
  • Tovuti ya Ofisi ya Takwimu ya Taifa (NBS)
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Open Data Tanzania

Wasomaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Makambako Town Council

    Anuani ya Posta: P.O.BOX 405 Makambako

    Simu ya mezani: 026-2730044

    Simu ya Kiganjani: 0785635383

    Barua pepe: td@makambakotc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Haki miliki ©2017 Halmashauri ya Mji Makambako. Haki zote zimehifadhiwa