• Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
HALMASHAURI YA MJI WA MAKAMBAKO
HALMASHAURI YA MJI WA MAKAMBAKO

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA HALMASHAURI YA MJI WA MAKAMBAKO

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Ardhi na maliasili
      • Raslimali watu na Utawala
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Usafi na mazingira
      • Elimu ya Msingi
      • Ujenzi na Uokoaji
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Elimu ya Sekondari
      • Kilimo, Ushirika na umwagiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maji
    • Vitengo
      • Sheria
      • ICT and Public relations
      • Ugavi na Manunuzi
      • Mkaguzi wa ndani
      • Ufugaji Nyuki
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma ya Afya
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Huduma za Jamii
      • Kamati ya Maadili
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Mipango Miji na Mazingira
    • Ratiba
      • Ratiba ya kumwona Mwenyekiti wa Halmashauri
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
  • Miradi
    • Miradi iliyo kwenye Mpango
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Ripoti mbalimbali
    • Mikataba
    • Mpango Mkakati
    • Hatua
    • Fomu za maombi
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Hotuba
    • Habari Mpya
    • Matukio
    • jarida la mji

MIL 350.8 ZA MIKOPO YA 10% ZATOLEWA KWA AWAMU YA PILI KWA MWAKA 2024/2025.

Tarehe iliyowekwa: August 1st, 2025

-Wanufaika watakiwa kusoma na kuielewa mikataba ya mikopo kabla ya kusaini kuepuka adhabu.


Na. Lina Sanga


Mwanasheria wa Halmashauri ya Mji Makambako, Bi. Amina Kassim amewataka wanufaika wa mikopo ya asilimia 10,kusoma na kuielewa mikataba ya mikopo kabla ya kusaini ili kutokuwa na sintofahamu katika utekelezaji wa vipengele vya sheria na kanuni zinazohusu utoaji wa mikopo hiyo.

Bi. Amina ametoa wito huo leo katika mafunzo kwa wanufaika wa mikopo ya asilimia 10 awamu ya pili kwa mwaka wa fedha 2024/2025, yaliyofanyika katika ukumbi wa Halmashauri ya Mji Makambako, ili kuwajengea uelewa wanufaika hao kabla ya kuanza kutekeleza miradi waliyoombea mikopo.

Amesema kuwa, Serikali kwa kutambua umuhimu wa mikopo hiyo na changamoto zinazoweza kujitokeza wakati wa utekelezaji wa miradi, imetoa nafasi kupitia sheria na kanuni za mikopo hiyo ili kuwawezesha wanufaika kugawana fedha na kuanzisha miradi binafsi,kuomba kubadilisha mradi baada ya mradi kusuasua,kuomba punguzo la kiwango cha marejesho au nyongeza ya Muda wa marejesho.  

"Ili muweze kutekeleza vipengele vya sheria ya mikopo ni lazima msome na kuuelewa mkataba husika,ili muweze kutambua wajibu na haki zenu kwani kusaini mikataba bila kusoma pia ni kosa kisheria,nawasisitiza msome na kuielewa kama kuna kipengele hukielewi uliza ueleweshwe", alisema Bi. Amina.

Naye Mkuu wa divisheni ya maendeleo ya jamii katika Halmashauri ya Mji Makambako, Bi. Lilian Mwelupungwi kabla ya kufungua mafunzo hayo, aliwataka wanufaika wote kuzingatia matumizi sahihi ya mikopo hiyo pamoja na kufanya marejesho ndani ya muda husika ili kujiongezea nafasi ya kupata mkopo mkubwa zaidi.

Spailo Nzalalila, Mmoja kati ya wanufaika wa mikopo hiyo ambaye pia ni Mwenyekiti wa kikundi cha Boda five  ametoa rai kwa Serikali kuendelea kutoa elimu ya mikopo ya asilimia 10 kwa vijana ili waweze kuunda vikundi, na kupata mikopo itayowawezesha kutekeleza miradi ya kiuchumi kwa mikopo isiyo na riba.

Halmashauri ya Mji Makambako katika kipindi cha awamu ya pili kwa mwaka wa fedha 2024/2025 imetoa jumla ya Mil 350.8 kwa vikundi 11 vya wanawake,vikundi 17 vya vijana na watu wenye ulemavu 2.

Matangazo

  • Ujio wa Mwenge wa Uhuru 2025, bado siku 13 April 19, 2025
  • Ujio wa Mwenge wa Uhuru 2025, bado siku 12. April 20, 2025
  • Ujio wa Mwenge wa Uhuru 2025, bado siku 11. April 21, 2025
  • Ujio wa Mwenge wa Uhuru 2025, bado siku 10. April 22, 2025
  • Fungua

Habari Mpya

  • Mil. 350.8 za Mikopo ya 10% zimetolewa kwa vikundi 30 Halmashauri ya Mji Makambako,DC aagiza mikopo hiyo kuwa chanzo cha utajiri.

    August 14, 2025
  • MIL 350.8 ZA MIKOPO YA 10% ZATOLEWA KWA AWAMU YA PILI KWA MWAKA 2024/2025.

    August 01, 2025
  • Wataalamu na viongozi watakiwa kusimamia upatikanaji na utoaji wa huduma za chanjo.

    April 25, 2025
  • Makambako yang'ara katika tuzo za Afya ya Usafi wa Mazingira ngazi ya Halmashauri za Miji.

    April 09, 2025
  • Fungua

Video

Shule mpya ya Mbugani Kitandililo sekondari kupitia mradi wa SEQUIP
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Fursa za Usafirishaji
  • Orodha ya Madiwani
  • Uzalishaji wa Umeme wa Upepo
  • Organisation Structure
  • Fursa za Biashara
  • By Laws
  • Permanent Committee

Tovuti Mashuhuri

  • Tovuti ya Ikulu ya Rais
  • Tovuti ya Ofisi ya Utumishi
  • Tovuti ya TAMISEMI
  • Tovuti ya Ofisi ya Takwimu ya Taifa (NBS)
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Open Data Tanzania

Wasomaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Makambako Town Council

    Anuani ya Posta: P.O.BOX 405 Makambako

    Simu ya mezani: 026-2730044

    Simu ya Kiganjani: 0785635383

    Barua pepe: td@makambakotc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Haki miliki ©2017 Halmashauri ya Mji Makambako. Haki zote zimehifadhiwa