• Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
HALMASHAURI YA MJI WA MAKAMBAKO
HALMASHAURI YA MJI WA MAKAMBAKO

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA HALMASHAURI YA MJI WA MAKAMBAKO

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Ardhi na maliasili
      • Raslimali watu na Utawala
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Usafi na mazingira
      • Elimu ya Msingi
      • Ujenzi na Uokoaji
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Elimu ya Sekondari
      • Kilimo, Ushirika na umwagiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maji
    • Vitengo
      • Sheria
      • ICT and Public relations
      • Ugavi na Manunuzi
      • Mkaguzi wa ndani
      • Ufugaji Nyuki
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma ya Afya
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Huduma za Jamii
      • Kamati ya Maadili
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Mipango Miji na Mazingira
    • Ratiba
      • Ratiba ya kumwona Mwenyekiti wa Halmashauri
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
  • Miradi
    • Miradi iliyo kwenye Mpango
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Ripoti mbalimbali
    • Mikataba
    • Mpango Mkakati
    • Hatua
    • Fomu za maombi
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Hotuba
    • Habari Mpya
    • Matukio
    • jarida la mji

Mkakati wa kutangaza vivutio vya utalii Mikoa ya kusini mwa Tanzania wazinduliwa rasmi leo Mkoani Njombe.

Tarehe iliyowekwa: September 26th, 2022

Na. Lina Sanga

Njombe

Waziri wa Maliasili na Utalii,Mhe. Balozi Pindi Chana(Mb) ,leo amezindua Mkakati wa kutangaza utalii Mikoa ya  kusini mwa Tanzania,na Kuendeleza utalii wa utamaduni wa Mikoa hiyo kwani kuna utajiri mkubwa sana wa utamaduni kama ngoma, mila, desturi pamoja na vyakula ambavyo ni sehemu ya utalii.

Mhe. Chana amesema kuwa kupitia mikakati hiyo  hatua mbalimbali zitazochukuliwa zimeainishwa,ili kuchochea ukuaji wa shughuli za utalii katika Mikoa ya Kusini ikiwemo Mkoa wa Iringa, Njombe, Rukwa, Katavi, Ruvuma, Mbeya, Mtwara,Lindi,Songwe na Morogoro.

Amesema kuwa,mikakati hiyo imezingatia  fursa za utalii zilizopo katika Mikoa ya Kusini hususani utalii wa utamaduni ambao ni hazina kubwa kwa mikoa hiyo,kwani utalii sio tu uwepo wa wanyama bali hata utalii wa utamaduni na kwasasa kuna ubunifu wa aina mpya ya utalii ikiwamo utalii wa masuala ya  nyuki,maua  na matibabu.

Aidha,Mhe. Chana amesema kupitia utekelezaji wa mikakati hiyo wanatarajia utaongeza idadi ya watalii wanaotembelea ukanda wa Kusini,hivyo kuongeza ajira na fursa za uwekezaji pamoja na kuongezeka kwa kipato cha mwananchi mmoja mmoja na mapato ya Serikali kwa ujumla.

Ametoa rai kwa wadau wa utalii na  wananchi wote wa Mikoa ya Kusini kuchangamkia fursa za utalii, zilizopo na zitazojitokeza ili kujipatia kipato na kuongeza  Mapato ya Mikoa yao.

Pia amewaomba Wakuu wa Mikoa kuwaelekeza watumishi wanaohusika na sekta za maliasili na utalii,kushirikiana na bodi ya Utalii Tanzania katika utekelezaji wa mikakati ya utalii iliyozinduliwa.

Ametoa rai kwa viongozi na wadau wote wa utalii kuungana na Mhe. Samia Suluhu Hassan,Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika kuendeleza programu  ya Tanzania The Royal Tour pamoja,na kushirikiana na Wizara ya Maliasili na Utalii katika kuendeleza na kubuni mikakati mbalimbali na mazao mbalimbali ya masuala ya utalii.

 Mwisho  amewashukuru wakuu wa Mikoa kwa kutambua maeneo ya utalii katika mikoa yao na kuwataka, kuendelea kuyatambua maeneo mengine ambayo bado hayajatambulika na kutangazwa kwenye gazeti la Serikali,kama maeneo muhimu ya utalii na Wizara ya Maliasili na Utalii ipo tayari kushirikiana na Mikoa  hiyo katika utambuzi wa maeneo yote ya utalii.

Matangazo

  • Ujio wa Mwenge wa Uhuru 2025, bado siku 13 April 19, 2025
  • Ujio wa Mwenge wa Uhuru 2025, bado siku 12. April 20, 2025
  • Ujio wa Mwenge wa Uhuru 2025, bado siku 11. April 21, 2025
  • Ujio wa Mwenge wa Uhuru 2025, bado siku 10. April 22, 2025
  • Fungua

Habari Mpya

  • Wataalamu na viongozi watakiwa kusimamia upatikanaji na utoaji wa huduma za chanjo.

    April 25, 2025
  • Makambako yang'ara katika tuzo za Afya ya Usafi wa Mazingira ngazi ya Halmashauri za Miji.

    April 09, 2025
  • Jumla ya Miti 15,000 kupandwa Halmashauri ya Mji Makambako kuelekea siku ya Miti duniani mwaka 2025.

    March 15, 2025
  • Maadhimisho ya siku ya wanawake duniani 2025 Mkoa wa Njombe, Mila kandamizi zaelezwa kuwa kikwazo cha ustawi na uwezeshaji

    March 09, 2025
  • Fungua

Video

Shule mpya ya Mbugani Kitandililo sekondari kupitia mradi wa SEQUIP
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Fursa za Usafirishaji
  • Orodha ya Madiwani
  • Uzalishaji wa Umeme wa Upepo
  • Organisation Structure
  • Fursa za Biashara
  • By Laws
  • Permanent Committee

Tovuti Mashuhuri

  • Tovuti ya Ikulu ya Rais
  • Tovuti ya Ofisi ya Utumishi
  • Tovuti ya TAMISEMI
  • Tovuti ya Ofisi ya Takwimu ya Taifa (NBS)
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Open Data Tanzania

Wasomaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Makambako Town Council

    Anuani ya Posta: P.O.BOX 405 Makambako

    Simu ya mezani: 026-2730044

    Simu ya Kiganjani: 0785635383

    Barua pepe: td@makambakotc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Haki miliki ©2017 Halmashauri ya Mji Makambako. Haki zote zimehifadhiwa