• Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
HALMASHAURI YA MJI WA MAKAMBAKO
HALMASHAURI YA MJI WA MAKAMBAKO

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA HALMASHAURI YA MJI WA MAKAMBAKO

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Ardhi na maliasili
      • Raslimali watu na Utawala
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Usafi na mazingira
      • Elimu ya Msingi
      • Ujenzi na Uokoaji
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Elimu ya Sekondari
      • Kilimo, Ushirika na umwagiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maji
    • Vitengo
      • Sheria
      • ICT and Public relations
      • Ugavi na Manunuzi
      • Mkaguzi wa ndani
      • Ufugaji Nyuki
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma ya Afya
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Huduma za Jamii
      • Kamati ya Maadili
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Mipango Miji na Mazingira
    • Ratiba
      • Ratiba ya kumwona Mwenyekiti wa Halmashauri
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
  • Miradi
    • Miradi iliyo kwenye Mpango
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Ripoti mbalimbali
    • Mikataba
    • Mpango Mkakati
    • Hatua
    • Fomu za maombi
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Hotuba
    • Habari Mpya
    • Matukio
    • jarida la mji

Mkuu wa Wilaya ya Njombe,Mhe. Kissa Gwakisa Kasongwa akabidhi Pikipiki 28 kwa Maafisa Ugani na Ushirika leo

Tarehe iliyowekwa: June 14th, 2022

Na. Lina Sanga

Mkuu wa wa Wilaya ya Njombe,Mhe. Kissa Gwakisa Kasongwa leo amewakabidhi Maafisa Ugani na Ushirika wa halmashauri ya Mji Makambako pikipiki 28 na amewataka Maafisa hao  kuzitunza pikipiki walizokabidhiwa,ili ziweze kudumu kwa muda mrefu kwa  kuzitumia kwa kazi iliyokusudiwa badala ya kubebea nyasi za ng’ombe,Mkaa na Mizigo mingine kuliko uwezo wa pikipiki hizo.

Mhe. Kasongwa ametoa wito huo wakati wa zoezi la ugawaji wa pikipiki hizo zilizotolewa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Mhe. Samia Suluhu Hassan kwa Maafisa Ugani wa Mikoa kumi Nchini  ili kuwawezesha maafisa hao kuwafikia wakulima kwa urahisi.

Aidha Mhe. Kasongwa  amesema kuwa  Mhe. Samia Suluhu Hassan kwa sasa ametoa pikipiki hizo kwa mikoa kumi ya mwanzo,ikiwa ni mikoa ambayo inatekeleza shughuli  za  kilimo na kuzalisha chakula kwa ajili ya Nchi yetu,hivyo baada ya kuwezeshwa pikipiki hizo ni matarajio ya Serikali kuona matokeo makubwa katika utendaji kazi wa maafisa Ugani.

 “Mhe. Samia Suluhu Hassan anasema kazi iendelee hivyo kupitia uwezeshwaji huu wa pikipiki 28 tunaamini kazi itaendelea zaidi,kwa kupata matokeo makubwa katika sekta ya kilimo kwa kuona utofauti wa kabla ya kupewa pikipiki na baada ya kupewa pikipiki hizi,hivyo mnatakiwa kujiwekea malengo ya kabla ya kuwa na pikipiki hali ilikuaje na baada ya kupewa pikipiki”,amesema Mhe. Kasongwa.

Pia ameipongeza halmashauri ya Mji  Makambako kwa kuitikia wito wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Mhe. Samia Suluhu Hassan  na Waziri Mkuu, Mhe. Kassim Majaliwa kuhusu ugawaji wa pikipiki hizo kwa Maafisa Ugani,na halmashauri ya Mji Makambako imetekeleza ugawaji wa pikipiki hizo  zikiwa na usajili wa awali ili zianze kazi na mengine yataendelea kukamilishwa kwenye maeneo yao kazi.

Akitoa shukrani kwa niaba ya Maafisa Ugani wote,Bw.Patrick Kyalawa ambaye ni Afisa Kilimo wa Kijiji cha Mkolango ametoa shukrani kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Mhe. Samia Suluhu Hassan  kwa kuwajali  na kuwapa pikipiki hizo ambazo  zitawasaidia kuwafikia wakulima kwa wakati,na kuleta matokeo makubwa tofauti na mwanzo kwani awali ilikuwa ngumu kuwafikia  wakulima kwa wakati,kwani vituo vya kazi vipo maeneo tofauti maeneo mengine kuna  milima na mabonde na kuwafikia wakulima kwa haraka ilikuwa ngumu,lakini kwa sasa wataweza kuwafikia wakulima kwa wakati na kutatua changamoto kwa haraka na kuleta mabadiliko makubwa  kupitia idara ya Kilimo.

Naye Afisa Usafirishaji wa halmashauri ya Mji Makambako,Bw. David Mbunda ametoa rai kwa Maafisa ugani wote waliokabidhiwa Pikipiki hizo kuzingatia sheria za barabarani na kuhakikisha wanapata leseni za udereva pamoja na kuhakikisha wanatunza pikipiki hizo na kuzitumia kwa matumizi yaliyokusudiwa na si vinginevyo.

Halmashauri ya Mji Makambako imepokea jumla ya pikipiki 28 ambapo pikipiki 27 ni kwa ajili ya Maafisa Ugani na pikipiki moja kwa ajili ya Afisa ushirika wa halmashauri ya Mji Makambako.

Matangazo

  • Ujio wa Mwenge wa Uhuru 2025, bado siku 13 April 19, 2025
  • Ujio wa Mwenge wa Uhuru 2025, bado siku 12. April 20, 2025
  • Ujio wa Mwenge wa Uhuru 2025, bado siku 11. April 21, 2025
  • Ujio wa Mwenge wa Uhuru 2025, bado siku 10. April 22, 2025
  • Fungua

Habari Mpya

  • Wataalamu na viongozi watakiwa kusimamia upatikanaji na utoaji wa huduma za chanjo.

    April 25, 2025
  • Makambako yang'ara katika tuzo za Afya ya Usafi wa Mazingira ngazi ya Halmashauri za Miji.

    April 09, 2025
  • Jumla ya Miti 15,000 kupandwa Halmashauri ya Mji Makambako kuelekea siku ya Miti duniani mwaka 2025.

    March 15, 2025
  • Maadhimisho ya siku ya wanawake duniani 2025 Mkoa wa Njombe, Mila kandamizi zaelezwa kuwa kikwazo cha ustawi na uwezeshaji

    March 09, 2025
  • Fungua

Video

Shule mpya ya Mbugani Kitandililo sekondari kupitia mradi wa SEQUIP
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Fursa za Usafirishaji
  • Orodha ya Madiwani
  • Uzalishaji wa Umeme wa Upepo
  • Organisation Structure
  • Fursa za Biashara
  • By Laws
  • Permanent Committee

Tovuti Mashuhuri

  • Tovuti ya Ikulu ya Rais
  • Tovuti ya Ofisi ya Utumishi
  • Tovuti ya TAMISEMI
  • Tovuti ya Ofisi ya Takwimu ya Taifa (NBS)
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Open Data Tanzania

Wasomaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Makambako Town Council

    Anuani ya Posta: P.O.BOX 405 Makambako

    Simu ya mezani: 026-2730044

    Simu ya Kiganjani: 0785635383

    Barua pepe: td@makambakotc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Haki miliki ©2017 Halmashauri ya Mji Makambako. Haki zote zimehifadhiwa