• Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
HALMASHAURI YA MJI WA MAKAMBAKO
HALMASHAURI YA MJI WA MAKAMBAKO

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA HALMASHAURI YA MJI WA MAKAMBAKO

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Ardhi na maliasili
      • Raslimali watu na Utawala
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Usafi na mazingira
      • Elimu ya Msingi
      • Ujenzi na Uokoaji
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Elimu ya Sekondari
      • Kilimo, Ushirika na umwagiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maji
    • Vitengo
      • Sheria
      • ICT and Public relations
      • Ugavi na Manunuzi
      • Mkaguzi wa ndani
      • Ufugaji Nyuki
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma ya Afya
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Huduma za Jamii
      • Kamati ya Maadili
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Mipango Miji na Mazingira
    • Ratiba
      • Ratiba ya kumwona Mwenyekiti wa Halmashauri
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
  • Miradi
    • Miradi iliyo kwenye Mpango
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Ripoti mbalimbali
    • Mikataba
    • Mpango Mkakati
    • Hatua
    • Fomu za maombi
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Hotuba
    • Habari Mpya
    • Matukio
    • jarida la mji

Mwenyekiti wa halmashauri ya Mji Makambako aagiza ukusanyaji wa mapato ufikie 100% kabla ya mwaka wa fedha kuisha

Tarehe iliyowekwa: May 24th, 2022

 Na. Lina Sanga

Watendaji wa halmashauri ya Mji Makambako pamoja na Madiwani wametakiwa kuhakikisha lengo la ukusanyaji mapato katika mwaka wa fedha 2021/2022 unafikia asilimia mia moja kabla ya mwaka kuisha.

Rai hiyo imetolewa leo na Mwenyekiti wa baraza la Madiwani katika halmashauri ya mji Makambako,Mhe. Hanana Mfikwa wakati wa ufunguzi wa mkutano wa baraza la madiwani kuishia robo ya tatu kwa kipindi cha januari hadi machi kwa mwaka wa fedha 2021/2022,uliofanyika leo katika ukumbi wa mikutano wa halmashauri ya mji makambako.

Mhe. Hanana amesema kuwa fedha zinazokusanywa zinaiwezesha halmashauri na Serikali kutekeleza shughuli mbalimbali kwa faida ya wananchi,hivyo ni wajibu wa kila mtendaji wa Serikali,viongozi wa wafanyabiashara na Madiwani kukusanya mapato ya halmashauri kwa haki bila kubugudhi wananchi hadi kufikia asilimia miamoja la lengo la ukusanyaji mapato.

Aidha Mhe. Hanana ameagiza usimamizi wa shughuli za ujenzi katika maeneo mbalimbali,mtendaji na diwani wana wajibu wa kusimamia na kuandika taarifa za miradi,kwa uwazi  kwa kuonyesha fedha za miradi zilizotolewa na Serikali,nguvu ya wananchi na michango ya viongozi na halmashauri ili kuondoa malalamiko ya wananchi dhidi ya Serikali. 

“Baadhi ya wananchi huuliza Serikali imetufanyia nini katika ujenzi wa miradi mbalimbali,hivyo endapo mtendaji ukiandika na kutafsiri taarifa ya mradi vizuri kwa kutaja fedha zilizotolewa na  Serikali katika ujenzi wa mradi,mchango wa diwani na viongozi wengine,mchango wa halmashauri na nguvu za wananchi katika kukamilisha mradi itasaidia kuwabana wananchi ambao hawajashiriki katika kuchangia lakini pia watatambua kazi inayofanywa na Serikali”,alisema Mhe. Hanana.

Aidha amewataka wananchi wote kutunza mazao yao na kuweka akiba ya chakula  ili kukabiliana na janga la njaa,ambalo linaweza kutokea kutokana na hali halisi iliyopo mashambani kutokana na uhaba wa mvua.

Wakati huo huo ametoa wito kwa wananchi wote kushiriki zoezi la utoaji chanjo ya Uviko 19 pamoja na polio inayotolewa kwa watoto chini ya umri wa miaka mitano ili kuwalinda na ugonjwa huo unaosababisha kupooza,lakini pia kila Mwananchi ahakikishe nyumba yake ina kibao che namba na ajiandae kushiriki Sensa ya watu agosti 23,2022.

Matangazo

  • Ujio wa Mwenge wa Uhuru 2025, bado siku 13 April 19, 2025
  • Ujio wa Mwenge wa Uhuru 2025, bado siku 12. April 20, 2025
  • Ujio wa Mwenge wa Uhuru 2025, bado siku 11. April 21, 2025
  • Ujio wa Mwenge wa Uhuru 2025, bado siku 10. April 22, 2025
  • Fungua

Habari Mpya

  • Wataalamu na viongozi watakiwa kusimamia upatikanaji na utoaji wa huduma za chanjo.

    April 25, 2025
  • Makambako yang'ara katika tuzo za Afya ya Usafi wa Mazingira ngazi ya Halmashauri za Miji.

    April 09, 2025
  • Jumla ya Miti 15,000 kupandwa Halmashauri ya Mji Makambako kuelekea siku ya Miti duniani mwaka 2025.

    March 15, 2025
  • Maadhimisho ya siku ya wanawake duniani 2025 Mkoa wa Njombe, Mila kandamizi zaelezwa kuwa kikwazo cha ustawi na uwezeshaji

    March 09, 2025
  • Fungua

Video

Shule mpya ya Mbugani Kitandililo sekondari kupitia mradi wa SEQUIP
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Fursa za Usafirishaji
  • Orodha ya Madiwani
  • Uzalishaji wa Umeme wa Upepo
  • Organisation Structure
  • Fursa za Biashara
  • By Laws
  • Permanent Committee

Tovuti Mashuhuri

  • Tovuti ya Ikulu ya Rais
  • Tovuti ya Ofisi ya Utumishi
  • Tovuti ya TAMISEMI
  • Tovuti ya Ofisi ya Takwimu ya Taifa (NBS)
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Open Data Tanzania

Wasomaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Makambako Town Council

    Anuani ya Posta: P.O.BOX 405 Makambako

    Simu ya mezani: 026-2730044

    Simu ya Kiganjani: 0785635383

    Barua pepe: td@makambakotc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Haki miliki ©2017 Halmashauri ya Mji Makambako. Haki zote zimehifadhiwa