• Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
HALMASHAURI YA MJI WA MAKAMBAKO
HALMASHAURI YA MJI WA MAKAMBAKO

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA HALMASHAURI YA MJI WA MAKAMBAKO

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Ardhi na maliasili
      • Raslimali watu na Utawala
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Usafi na mazingira
      • Elimu ya Msingi
      • Ujenzi na Uokoaji
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Elimu ya Sekondari
      • Kilimo, Ushirika na umwagiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maji
    • Vitengo
      • Sheria
      • ICT and Public relations
      • Ugavi na Manunuzi
      • Mkaguzi wa ndani
      • Ufugaji Nyuki
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma ya Afya
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Huduma za Jamii
      • Kamati ya Maadili
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Mipango Miji na Mazingira
    • Ratiba
      • Ratiba ya kumwona Mwenyekiti wa Halmashauri
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
  • Miradi
    • Miradi iliyo kwenye Mpango
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Ripoti mbalimbali
    • Mikataba
    • Mpango Mkakati
    • Hatua
    • Fomu za maombi
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Hotuba
    • Habari Mpya
    • Matukio
    • jarida la mji

Njombe yafanya kongamano la kuiombea nchi na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania leo

Tarehe iliyowekwa: July 29th, 2022

Na. Lina Sanga

Njombe

Kongamano la kuiombea nchi ya Tanzania  na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Mhe. Samia Suluhu Hassan,kwa kazi kubwa nayoifanya ya kuliongoza taifa la Tanzania na kudumisha amani ya nchi.

Akizungumza na viongozi wa dini,viongozi wa kimila,viongozi wa Serikali na wananchi waliohudhuria kongamano hilo la maombi, lililofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Halmashauri ya Mji Njombe leo,Mhe. Waziri Kindamba ambaye alikuwa Mkuu wa Mkoa wa Njombe kabla ya kuhamishiwa Mkoani Songwe amesema kuwa sala na dua zilizofanyika kwa ajili ya Nchi na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ni kutokana na kazi kubwa inayofanywa na Serikali kwa kutoa fedha nyingi kwa ajili ya miradi mbalimbali ya kimkakati ambayo baadhi imekamilika na mingine ipo hatua ya ukamilishaji na mingine inaanza.

Mhe.Kindamba amesema kuwa,katika utawala wa Mhe. Samia Mkoa wa Njombe umepokea fedha za utekelezaji wa miradi mikubwa ya kimkakati ikiwa ni pamoja na bil. 136 kwa ajili ya ukamilishaji wa barabara ya Njombe na  Makete,zaidi ya bil.179.2 kwa ajili ya ukamilishaji  wa barabara ya Lusitu na Mawendi kwa kiwango cha zege  na bil 95 kwa ajili ya ujenzi wa barabara ya Itonyi na Lusitu.

Amesema kuwa jumla ya  bil 3.3 kwa ajili ya mpango wa uboreshaji wa upatikanaji wa maji katika maeneo ya mijini na vijiji na jumla ya wananchi 24,880 watanufaika na mradi huo,baadhi ya wananchi wataonufaika na mradi huo wa maji ni katika vijiji vya  Mlope,Ludewa mjini,Posta chini, Ngalanga, Sido, Matalawe, Ngelela na Isapulano.

Ameongeza kuwa jumla ya  bil. 1,9 za tozo za miamala ya simu zilipokelewa ambapo  mil. 150 zimetumika katika umaliziaji wa maboma ya madarasa kumi na mbili katika shule za Sekondari, bil 1.8 kwa ajili ya ujenzi wa vituo vipya vya afya saba, zaidi ya bil. 4.7 kwa ajili ya ujenzi wa vyumba vya madarasa katika shule za Msingi,Sekondari na shule shikizi.

Aidha amesema kuwa, manufaa makubwa yamepatikana kupitia fedha hizo zilizotolewa na Serikali kwa ajili ya ujenzi wa miundombinu ya madarasa ni kupunguza msongamano wa wanafunzi madarasani,hivyo kutokana na juhudi za Mhe. Samia na Serikali yake ya awamu ya sita,Mkoa wa Njombe umeandaa maombi hayo maalumu ya kumuombea Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Nchi kwa ujumla ili amani iliyopo iendelee kudumu daima.

Ametoa wito kwa wananchi wote wa Mkoa wa Njombe kuhakikisha wanapata chanjo ya Uviko 19 kwani hakutakuwa na usalama endapo jirani zao hawajapata chanjo,lakini pia amewataka wananchi wote wa Mkoa wa Njombe na Tanzania kwa ujumla,kujiandaa kushiriki kikamilifu katika zoezi la Sensa ya watu na Makazi itakayofanyika kuanzia agosti 23,mwaka huu.  Ili kupata takwimu sahihi kwa manufaa ya Umma.

Matangazo

  • Ujio wa Mwenge wa Uhuru 2025, bado siku 13 April 19, 2025
  • Ujio wa Mwenge wa Uhuru 2025, bado siku 12. April 20, 2025
  • Ujio wa Mwenge wa Uhuru 2025, bado siku 11. April 21, 2025
  • Ujio wa Mwenge wa Uhuru 2025, bado siku 10. April 22, 2025
  • Fungua

Habari Mpya

  • Wataalamu na viongozi watakiwa kusimamia upatikanaji na utoaji wa huduma za chanjo.

    April 25, 2025
  • Makambako yang'ara katika tuzo za Afya ya Usafi wa Mazingira ngazi ya Halmashauri za Miji.

    April 09, 2025
  • Jumla ya Miti 15,000 kupandwa Halmashauri ya Mji Makambako kuelekea siku ya Miti duniani mwaka 2025.

    March 15, 2025
  • Maadhimisho ya siku ya wanawake duniani 2025 Mkoa wa Njombe, Mila kandamizi zaelezwa kuwa kikwazo cha ustawi na uwezeshaji

    March 09, 2025
  • Fungua

Video

Shule mpya ya Mbugani Kitandililo sekondari kupitia mradi wa SEQUIP
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Fursa za Usafirishaji
  • Orodha ya Madiwani
  • Uzalishaji wa Umeme wa Upepo
  • Organisation Structure
  • Fursa za Biashara
  • By Laws
  • Permanent Committee

Tovuti Mashuhuri

  • Tovuti ya Ikulu ya Rais
  • Tovuti ya Ofisi ya Utumishi
  • Tovuti ya TAMISEMI
  • Tovuti ya Ofisi ya Takwimu ya Taifa (NBS)
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Open Data Tanzania

Wasomaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Makambako Town Council

    Anuani ya Posta: P.O.BOX 405 Makambako

    Simu ya mezani: 026-2730044

    Simu ya Kiganjani: 0785635383

    Barua pepe: td@makambakotc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Haki miliki ©2017 Halmashauri ya Mji Makambako. Haki zote zimehifadhiwa