• Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
HALMASHAURI YA MJI WA MAKAMBAKO
HALMASHAURI YA MJI WA MAKAMBAKO

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA HALMASHAURI YA MJI WA MAKAMBAKO

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Ardhi na maliasili
      • Raslimali watu na Utawala
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Usafi na mazingira
      • Elimu ya Msingi
      • Ujenzi na Uokoaji
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Elimu ya Sekondari
      • Kilimo, Ushirika na umwagiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maji
    • Vitengo
      • Sheria
      • ICT and Public relations
      • Ugavi na Manunuzi
      • Mkaguzi wa ndani
      • Ufugaji Nyuki
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma ya Afya
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Huduma za Jamii
      • Kamati ya Maadili
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Mipango Miji na Mazingira
    • Ratiba
      • Ratiba ya kumwona Mwenyekiti wa Halmashauri
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
  • Miradi
    • Miradi iliyo kwenye Mpango
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Ripoti mbalimbali
    • Mikataba
    • Mpango Mkakati
    • Hatua
    • Fomu za maombi
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Hotuba
    • Habari Mpya
    • Matukio
    • jarida la mji

Njombe yazindua mwongozo wa elimu na mkakati mpya wa kutokomeza ziro.

Tarehe iliyowekwa: September 12th, 2022

 Na. Lina Sanga

Mkoa wa Njombe umezindua mwongozo wa elimu leo na  kuweka mkakati mpya  wa kutokomeza ziro kwa wanafunzi wa kidato cha nne,ambapo walimu wametakiwa kuwafundisha watoto masomo matano wanayoyaweza  badala ya kumi na moja.

Akiwasilisha mkakati huo Mkuu wa Mkoa wa Njombe,Mhe. Anthony Mtaka  katika uzinduzi wa Mwongozo wa elimu uliofanyika  leo shule ya sekondali Mpechi, amesema kuwa badala ya walimu kuendelea kuwafundisha wanafunzi masomo yote hata ambayo hawayawezi ni wakati sasa walimu kuwapima wanafunzi hao ili kutambua masomo matano ambayo kila mwanafunzi anayaweza na kuwafundisha zaidi ili waweze kufaulu vizuri badala ya kuwaongezea mzigo wa masomo mengine ambayo hawayawezi.

Ametoa rai kwa walimu na wanafunzi kuhakikisha wanatokomeza ziro na shule ya Serikali  itayofaulisha na kuingia kumi bora,itapewa milioni tano taslimu kwaajili ya walimu sio matumizi ya shule na mwanafunzi atayefaulu daraja la kwanza la pointi saba atapewa laki tano,mwanafunzi wa kike na wenye mahitaji maalumu wataopata daraja la kwanza la pointi nane na tisa (single digit) watapewa laki tano,Mwalimu atayefaulisha kila alama A atapewa elfu ishirini na alama B atapewa elfu tano.

Amesema kuwa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa itatoa fedha hizo kama motisha kwa walimu na wanafunzi,ili mkakati wa kutokomeza ziro ufanikiwe lakini pia wazazi na walezi wa wanafunzi hao wana nafasi kubwa sana katika ufaulu wa wanafunzi hivyo ili mkakati huo ufanikiwe wazazi hawana budi kuhakikisha wanawasimamia watoto wao kujisomea.


Akielezea mikakati iliyopo katika vitabu vitatu vilivyozinduliwa leo Afisa elimu Mkoa wa Njombe,Mwl. Nelasi Mulungu amesema mikakati iliyopo katika vitabu hivyo ni kuhakikisha wanafunzi wote wanaoanza darasa la kwanza wanamaliza darasa la saba,kuhakikisha wanafunzi wote wanapofika  darasa la pili wanajua kusoma,kuandika na kuhesabu na kila mwanafunzi anayeanza kidato cha kwanza anamaliza kidato cha nne.


Mulungu amesema mikakati hiyo inawaelekeza viongozi namna ya kusimamia na kufuatilia  shule katika maeneo yao,huku  ikiwalenga hasa Walimu wakuu,Wakuu wa shule,Maafisa elimu Kata,viongozi ngazi ya Halmashauri na Mikoa.

Matangazo

  • Ujio wa Mwenge wa Uhuru 2025, bado siku 13 April 19, 2025
  • Ujio wa Mwenge wa Uhuru 2025, bado siku 12. April 20, 2025
  • Ujio wa Mwenge wa Uhuru 2025, bado siku 11. April 21, 2025
  • Ujio wa Mwenge wa Uhuru 2025, bado siku 10. April 22, 2025
  • Fungua

Habari Mpya

  • Wataalamu na viongozi watakiwa kusimamia upatikanaji na utoaji wa huduma za chanjo.

    April 25, 2025
  • Makambako yang'ara katika tuzo za Afya ya Usafi wa Mazingira ngazi ya Halmashauri za Miji.

    April 09, 2025
  • Jumla ya Miti 15,000 kupandwa Halmashauri ya Mji Makambako kuelekea siku ya Miti duniani mwaka 2025.

    March 15, 2025
  • Maadhimisho ya siku ya wanawake duniani 2025 Mkoa wa Njombe, Mila kandamizi zaelezwa kuwa kikwazo cha ustawi na uwezeshaji

    March 09, 2025
  • Fungua

Video

Shule mpya ya Mbugani Kitandililo sekondari kupitia mradi wa SEQUIP
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Fursa za Usafirishaji
  • Orodha ya Madiwani
  • Uzalishaji wa Umeme wa Upepo
  • Organisation Structure
  • Fursa za Biashara
  • By Laws
  • Permanent Committee

Tovuti Mashuhuri

  • Tovuti ya Ikulu ya Rais
  • Tovuti ya Ofisi ya Utumishi
  • Tovuti ya TAMISEMI
  • Tovuti ya Ofisi ya Takwimu ya Taifa (NBS)
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Open Data Tanzania

Wasomaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Makambako Town Council

    Anuani ya Posta: P.O.BOX 405 Makambako

    Simu ya mezani: 026-2730044

    Simu ya Kiganjani: 0785635383

    Barua pepe: td@makambakotc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Haki miliki ©2017 Halmashauri ya Mji Makambako. Haki zote zimehifadhiwa