• Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
HALMASHAURI YA MJI WA MAKAMBAKO
HALMASHAURI YA MJI WA MAKAMBAKO

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA HALMASHAURI YA MJI WA MAKAMBAKO

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Ardhi na maliasili
      • Raslimali watu na Utawala
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Usafi na mazingira
      • Elimu ya Msingi
      • Ujenzi na Uokoaji
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Elimu ya Sekondari
      • Kilimo, Ushirika na umwagiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maji
    • Vitengo
      • Sheria
      • ICT and Public relations
      • Ugavi na Manunuzi
      • Mkaguzi wa ndani
      • Ufugaji Nyuki
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma ya Afya
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Huduma za Jamii
      • Kamati ya Maadili
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Mipango Miji na Mazingira
    • Ratiba
      • Ratiba ya kumwona Mwenyekiti wa Halmashauri
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
  • Miradi
    • Miradi iliyo kwenye Mpango
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Ripoti mbalimbali
    • Mikataba
    • Mpango Mkakati
    • Hatua
    • Fomu za maombi
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Hotuba
    • Habari Mpya
    • Matukio
    • jarida la mji

OR TAMISEMI yarahisisha ulipaji kodi za majengo,mabango na vibali vya Ujenzi kidigirali kupitia mfumo wa TAUSI.

Tarehe iliyowekwa: June 26th, 2024

Na. Lina Sanga

Ofisi ya Rais ,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) kupitia mfumo wa TAUSI imefanikiwa kuboresha utoaji wa huduma ya ukusanyaji wa kodi za majengo,mabango na utoaji wa vibali vya ujenzi kidigitali na kupunguza usumbufu kwa wananchi kufika Halmashauri kwa ajili ya kupata huduma hizo.

Taarifa hiyo imetolewa leo na Afisa Mipangomiji mwandamizi wa Ofisi ya Rais TAMISEMI, George Miringay katika semina ya mafunzo ya ukusanyaji wa kodi za majengo,mabango na utoaji wa vibali kidigitali kupitia mfumo wa TAUSI, kwa wataalamu wa Halmashauri ya Mji Makambako.

Miringay amesema kuwa, awali huduma ya ukusanyaji wa kodi za majengo na mabango  zilikuwa zikitolewa kupitia Mamlaka ya  mapato Tanzania (TRA) kwa njia ya analogia na kwa sasa huduma hizo zimerejeshwa OR TAMISEMI na zitakuwa zikikusanywa na watendaji wa mitaa badala ya kuajiri watu wa kukusanya na vibali vya ujenzi vitatolewa na wataalamu kidigitali pasipo mwananchi kufika ofisini.

Amesema kuwa, kupitia mfumo wa TAUSI mwananchi anaweza kupata kibali cha ujenzi ndani ya siku moja tofauti na awali ambapo vibali vilitolewa hata baada ya miezi miwili, kujua kiasi cha gharama anachotakiwa kulipa kwa ajili ya bango pamoja na kodi ya majengo ambayo inakusanywa kupitia luku za umeme kwa sasa.

Pia, amesema kuwa kutokana na baadhi ya majengo kutolipiwa kodi ya majengo kwa kukosa umeme kupitia mfumo wa TAUSI majengo yote yanayotumika wamiliki watatakiwa kulipa kodi baada ya watendaji wa Kata, Mitaa na Vijiji kuwasajili kwenye mfumo isipokuwa nyumba zilizojengwa kwa tope,ofisi na majengo ya Serikali,makanisa, misikiti na nyumba zinazomilikiwa na kanisa au msikiti.

Aidha, amebainisha kuwa kupitia ukusanyaji wa kodi hizo Halmashauri kupitia  makusanyo ya kodi za majengo itapata asilimia 20 na asilimia 100 kupitia makusanyo ya ushuru wa mabango ambapo awali fedha hizo zilielekezwa Serikali kuu.

Ametoa wito kwa wananchi kutoa ushirikiano kwa watendaji wanapofika katika maeneo yao kwa ajili ya usajili kwani kodi hizo sio mpya bali ni maboresho yamefanyika kutoka analogia kwenda digitali ili kurahisisha utoaji na upatikanaji wa huduma kwa ufanisi.

Matangazo

  • Ujio wa Mwenge wa Uhuru 2025, bado siku 13 April 19, 2025
  • Ujio wa Mwenge wa Uhuru 2025, bado siku 12. April 20, 2025
  • Ujio wa Mwenge wa Uhuru 2025, bado siku 11. April 21, 2025
  • Ujio wa Mwenge wa Uhuru 2025, bado siku 10. April 22, 2025
  • Fungua

Habari Mpya

  • Wataalamu na viongozi watakiwa kusimamia upatikanaji na utoaji wa huduma za chanjo.

    April 25, 2025
  • Makambako yang'ara katika tuzo za Afya ya Usafi wa Mazingira ngazi ya Halmashauri za Miji.

    April 09, 2025
  • Jumla ya Miti 15,000 kupandwa Halmashauri ya Mji Makambako kuelekea siku ya Miti duniani mwaka 2025.

    March 15, 2025
  • Maadhimisho ya siku ya wanawake duniani 2025 Mkoa wa Njombe, Mila kandamizi zaelezwa kuwa kikwazo cha ustawi na uwezeshaji

    March 09, 2025
  • Fungua

Video

Shule mpya ya Mbugani Kitandililo sekondari kupitia mradi wa SEQUIP
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Fursa za Usafirishaji
  • Orodha ya Madiwani
  • Uzalishaji wa Umeme wa Upepo
  • Organisation Structure
  • Fursa za Biashara
  • By Laws
  • Permanent Committee

Tovuti Mashuhuri

  • Tovuti ya Ikulu ya Rais
  • Tovuti ya Ofisi ya Utumishi
  • Tovuti ya TAMISEMI
  • Tovuti ya Ofisi ya Takwimu ya Taifa (NBS)
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Open Data Tanzania

Wasomaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Makambako Town Council

    Anuani ya Posta: P.O.BOX 405 Makambako

    Simu ya mezani: 026-2730044

    Simu ya Kiganjani: 0785635383

    Barua pepe: td@makambakotc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Haki miliki ©2017 Halmashauri ya Mji Makambako. Haki zote zimehifadhiwa