• Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
HALMASHAURI YA MJI WA MAKAMBAKO
HALMASHAURI YA MJI WA MAKAMBAKO

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA HALMASHAURI YA MJI WA MAKAMBAKO

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Ardhi na maliasili
      • Raslimali watu na Utawala
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Usafi na mazingira
      • Elimu ya Msingi
      • Ujenzi na Uokoaji
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Elimu ya Sekondari
      • Kilimo, Ushirika na umwagiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maji
    • Vitengo
      • Sheria
      • ICT and Public relations
      • Ugavi na Manunuzi
      • Mkaguzi wa ndani
      • Ufugaji Nyuki
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma ya Afya
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Huduma za Jamii
      • Kamati ya Maadili
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Mipango Miji na Mazingira
    • Ratiba
      • Ratiba ya kumwona Mwenyekiti wa Halmashauri
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
  • Miradi
    • Miradi iliyo kwenye Mpango
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Ripoti mbalimbali
    • Mikataba
    • Mpango Mkakati
    • Hatua
    • Fomu za maombi
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Hotuba
    • Habari Mpya
    • Matukio
    • jarida la mji

Serikali ipo tayari kupokea ushauri wa Maafisa habari na kuboresha sekta ya habari na mawasiliano nchini.

Tarehe iliyowekwa: March 27th, 2023

Na. Lina Sanga

Dar es salaam

Tamko hilo limetolewa  na Waziri Mkuu,Mhe. Kassim Majaliwa katika ufunguzi wa  kikao kazi cha 18 cha Maafisa habari,Mawasiliano na Uhusiano wa Serikali, kilichofanyika leo katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNICC) jijini Dar es salaam.

Mhe. Majaliwa amesema kuwa ipo haja ya mamlaka mbalimbali kuwapa nafasi Maafisa Habari wa Serikali na Taasisi zote kuwa wasemaji wa taasisi kama ilivyo kwa klabu za mpira ili kuhabarisha umma kwa kutoa habari sahihi kwa  wakati kuepusha  upotoshaji.

"Nataka kuonyesha  mfano ambao  wenzetu wanafanikiwa mfano Msemaji wa Yanga kila siku tunamwona  na Simba  kila siku tunamwona ,Masao Bwire  wa Ruvu shooting tunamuona kila siku hata wa Mtibwa kila siku tunamwona je, sisi? nimetoa mfano huu ili ndani ya siku tano za kikao hiki mfanye tathmini na Serikali ipo tayari kupokea ushauri wenu na kutekeleza matakwa yenu kama Maafisa habari",alisema Mhe. Majaliwa.

Aidha ametoa maagizo kwa Makatibu Tawala wa Mikoa, Wakurugenzi wa Halmashauri na Taasisi zilizo chini ya Serikali kutambua umuhimu wa kuwa na Afisa habari katika taasisi na kukamilisha ikama ya Maafisa habari kama inavyohitajika pamoja na kutenga bajeti ya kutosha kwa ajili ya Vitengo vya Mawasiliano.

Pia,amewataka Viongozi wote kuwajengea uwezo Maafisa habari ili waweze kutumia teknolojia ya kisasa  na kutengeneza utaratibu wa kuwashirikisha  Maafisa habari katika utekelezaji wa shughuli zote za taasisi pamoja  na  miradi ya maendeleo kwa kuwawezesha vyombo vya usafiri wakati wa ziara za viongozi pamoja na kuwawezesha kushiriki vikao kazi.

Aidha, ameitaka Wizara ya Habari na Mawasiliano na Teknolojia ya Habari pamoja na idara ya Habari Maelezo kuwasimamia na kuwakutanisha Maafisa habari kwenye vikao kupitia mitandao na ana kwa ana.

Kikao kazi cha 18 cha Maafisa Habari,Mawasiliano na Uhusiano wa Serikali kinafanyika kwa siku tano ambapo Maafisa hao watapata nafasi ya Kutembelea miradi ya Kimkakati inayotekelezwa na Serikali katika jiji la Dar es salaam machi 31,2023 siku ya Ijumaa.

Matangazo

  • Ujio wa Mwenge wa Uhuru 2025, bado siku 13 April 19, 2025
  • Ujio wa Mwenge wa Uhuru 2025, bado siku 12. April 20, 2025
  • Ujio wa Mwenge wa Uhuru 2025, bado siku 11. April 21, 2025
  • Ujio wa Mwenge wa Uhuru 2025, bado siku 10. April 22, 2025
  • Fungua

Habari Mpya

  • Wataalamu na viongozi watakiwa kusimamia upatikanaji na utoaji wa huduma za chanjo.

    April 25, 2025
  • Makambako yang'ara katika tuzo za Afya ya Usafi wa Mazingira ngazi ya Halmashauri za Miji.

    April 09, 2025
  • Jumla ya Miti 15,000 kupandwa Halmashauri ya Mji Makambako kuelekea siku ya Miti duniani mwaka 2025.

    March 15, 2025
  • Maadhimisho ya siku ya wanawake duniani 2025 Mkoa wa Njombe, Mila kandamizi zaelezwa kuwa kikwazo cha ustawi na uwezeshaji

    March 09, 2025
  • Fungua

Video

Shule mpya ya Mbugani Kitandililo sekondari kupitia mradi wa SEQUIP
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Fursa za Usafirishaji
  • Orodha ya Madiwani
  • Uzalishaji wa Umeme wa Upepo
  • Organisation Structure
  • Fursa za Biashara
  • By Laws
  • Permanent Committee

Tovuti Mashuhuri

  • Tovuti ya Ikulu ya Rais
  • Tovuti ya Ofisi ya Utumishi
  • Tovuti ya TAMISEMI
  • Tovuti ya Ofisi ya Takwimu ya Taifa (NBS)
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Open Data Tanzania

Wasomaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Makambako Town Council

    Anuani ya Posta: P.O.BOX 405 Makambako

    Simu ya mezani: 026-2730044

    Simu ya Kiganjani: 0785635383

    Barua pepe: td@makambakotc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Haki miliki ©2017 Halmashauri ya Mji Makambako. Haki zote zimehifadhiwa