• Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
HALMASHAURI YA MJI WA MAKAMBAKO
HALMASHAURI YA MJI WA MAKAMBAKO

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA HALMASHAURI YA MJI WA MAKAMBAKO

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Ardhi na maliasili
      • Raslimali watu na Utawala
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Usafi na mazingira
      • Elimu ya Msingi
      • Ujenzi na Uokoaji
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Elimu ya Sekondari
      • Kilimo, Ushirika na umwagiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maji
    • Vitengo
      • Sheria
      • ICT and Public relations
      • Ugavi na Manunuzi
      • Mkaguzi wa ndani
      • Ufugaji Nyuki
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma ya Afya
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Huduma za Jamii
      • Kamati ya Maadili
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Mipango Miji na Mazingira
    • Ratiba
      • Ratiba ya kumwona Mwenyekiti wa Halmashauri
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
  • Miradi
    • Miradi iliyo kwenye Mpango
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Ripoti mbalimbali
    • Mikataba
    • Mpango Mkakati
    • Hatua
    • Fomu za maombi
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Hotuba
    • Habari Mpya
    • Matukio
    • jarida la mji

Serikali italipa madeni ya nyuma ya  mbolea za ruzuku,baada ya uchunguzi wa uhalali wa madai kukamilika.

Tarehe iliyowekwa: January 17th, 2023

Na. Lina Sanga

Kauli hiyo imetolewa na Waziri wa Kilimo, Mhe. Hussein Bashe leo katika kikao kilichofanyika katika Ukumbi wa Halmashauri ya Mji Makambako,baada ya kufanya ziara kwenye baadhi ya maeneo ndani ya Mkoa wa Njombe ikiwa ni pamoja na  Halmashauri ya Mji Makambako.

Mhe. Bashe ametoa kauli hiyo baada ya baadhi ya Mawakala wa mbolea waliosambaza mbolea mwaka 2014 na 2015 kuiomba Serikali kupitia Wizara ya Kilimo  kuwalipa madai yao ili waweze kuendeleza biashara zao.

Mhe. Bashe amesema kuwa,kutokana na njia za utoaji wa mbolea za ruzuku kipindi cha nyuma kutokuwa na usimamizi mzuri,kuna baadhi ya watumishi wa Serikali walishiriki katika udanganyifu wa uuzaji wa mbolea hizo kinyume na malengo yaliyokusudiwa kwa kujinufaisha wenyewe na makampuni ya usambazaji wa mbolea pamoja na mawakala badala ya mkulima.

Ameongeza kuwa, kutokana na udanganyifu uliofanyika katika zoezi hilo,Serikali inaendelea kufanya uchunguzi juu ya uhalali wa madai hayo,kwani asilimia hamsini ya madai hayo sio halali na kuna baadhi ya vocha zilighushiwa hivyo malipo yatafanyika baada ya uchunguzi kukamilika.

Aidha,Mhe. Bashe ameifungia  Kampuni ya parachichi inayofahamika kwa jina la  Kandia Fresh Produces Ltd yenye makao makuu  nchini  Kenya inayofanya biashara ya  ununuzi wa parachichi katika Mkoa wa Njombe , kutojishughulisha na biashara ya parachichi ndani ya nchi ya Tanzania tena ,kwani kitendo walichofanya cha kutupa dampo parachichi walizonunua shambani kwa madai ya kutokomaa ni kitendo cha uonevu kwa wakulima na wameonyesha kukosa uaminifu ambao unaweza kuharibu sifa ya soko la nje la bidhaa hiyo kutoka Tanzania.

Mhe. Bashe amesema kitendo kilichofanywa na Kampuni hiyo ni kitendo kibaya chenye lengo la kukwamisha jitihada za Serikali ya awamu ya sita, za kufungua mipaka ya nchi na kutafuta masoko ya uhakika nchi za nje.

Ametoa wito kwa wakulima wa zao la parachichi kutokuuza matunda ambayo hayajakomaa vizuri na kuzitaka kampuni za ununuzi wa parachichi nchini kutosafirisha matunda yasiyo na ubora ili kutunza soko la zao hilo.


Matangazo

  • Ujio wa Madaktari bingwa Hospitali ya Mji Makambako (Mlowa) September 17, 2025
  • Tangazo la kazi 2024 March 11, 2024
  • Mkutano wa uhamasishaji zoezi la urasimishaji Kata ya Kitisi na Majengo juni 27 - 29,2024 May 28, 2024
  • Mkutano wa uhamasishaji zoezi la urasimishaji Kata ya Mjimwema May 28, 2024
  • Fungua

Habari Mpya

  • Mil. 350.8 za Mikopo ya 10% zimetolewa kwa vikundi 30 Halmashauri ya Mji Makambako,DC aagiza mikopo hiyo kuwa chanzo cha utajiri.

    August 14, 2025
  • MIL 350.8 ZA MIKOPO YA 10% ZATOLEWA KWA AWAMU YA PILI KWA MWAKA 2024/2025.

    August 01, 2025
  • Wataalamu na viongozi watakiwa kusimamia upatikanaji na utoaji wa huduma za chanjo.

    April 25, 2025
  • Makambako yang'ara katika tuzo za Afya ya Usafi wa Mazingira ngazi ya Halmashauri za Miji.

    April 09, 2025
  • Fungua

Video

Shule mpya ya Mbugani Kitandililo sekondari kupitia mradi wa SEQUIP
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Fursa za Usafirishaji
  • Orodha ya Madiwani
  • Uzalishaji wa Umeme wa Upepo
  • Organisation Structure
  • Fursa za Biashara
  • By Laws
  • Permanent Committee

Tovuti Mashuhuri

  • Tovuti ya Ikulu ya Rais
  • Tovuti ya Ofisi ya Utumishi
  • Tovuti ya TAMISEMI
  • Tovuti ya Ofisi ya Takwimu ya Taifa (NBS)
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Open Data Tanzania

Wasomaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Makambako Town Council

    Anuani ya Posta: P.O.BOX 405 Makambako

    Simu ya mezani: 026-2730044

    Simu ya Kiganjani: 0785635383

    Barua pepe: td@makambakotc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Haki miliki ©2017 Halmashauri ya Mji Makambako. Haki zote zimehifadhiwa