• Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
HALMASHAURI YA MJI WA MAKAMBAKO
HALMASHAURI YA MJI WA MAKAMBAKO

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA HALMASHAURI YA MJI WA MAKAMBAKO

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Ardhi na maliasili
      • Raslimali watu na Utawala
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Usafi na mazingira
      • Elimu ya Msingi
      • Ujenzi na Uokoaji
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Elimu ya Sekondari
      • Kilimo, Ushirika na umwagiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maji
    • Vitengo
      • Sheria
      • ICT and Public relations
      • Ugavi na Manunuzi
      • Mkaguzi wa ndani
      • Ufugaji Nyuki
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma ya Afya
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Huduma za Jamii
      • Kamati ya Maadili
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Mipango Miji na Mazingira
    • Ratiba
      • Ratiba ya kumwona Mwenyekiti wa Halmashauri
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
  • Miradi
    • Miradi iliyo kwenye Mpango
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Ripoti mbalimbali
    • Mikataba
    • Mpango Mkakati
    • Hatua
    • Fomu za maombi
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Hotuba
    • Habari Mpya
    • Matukio
    • jarida la mji

WAKULIMA THELATHINI WA ZAO LA ALIZETI WANUFAIKA NA MKOPO .

Tarehe iliyowekwa: October 25th, 2021
  1. Halmashauri ya Mji Makambako kupitia idara ya Kilimo na Umwagiliaji na idara ya Maendeleo ya Jamii,imetoa kiasi cha shilingi mil.9  kwa vikundi vitatu vya wanawake na Vijana  wanaolima zao la alizeti ambapo fedha hizo zimetolewa kwenye Mfuko wa Maendeleo ya Vijana,Wanawake na watu wenye ulemavu,ili kuwawezesha wakulima hao kuzalisha zao hilo kwa wingi,

Kauli hiyo imetolewa leo na Kaimu Afisa kilimo,Umwagiliaji na Ushirika  wa Halmashauri ya Mji Makambako Bi. Beatrice Tarimo,katika ufunguzi wa mafunzo kuhusu kilimo cha zao la alizeti hususani katika  suala la matumizi ya Mbolea na Uchaguzi wa mbegu bora,yaliyofanyika  katika ukumbi wa Mikutano wa Halmashauri,ambapo jumla ya vikundi vitatu vimenufaika  na mkopo huo.

Bi. Tarimo  amesema kuwa,Nchi ya Tanzania kwa sasa inalazimika kuagiza mafuta ya alizeti nje ya Nchi,kutokana na uhaba wa zao la alizeti Nchini,kwani wakulima wengi hulima zao hilo kama ziada na kwa matumizi ya nyumbani na sio kwa ajili ya  biashara.

Amesema kuwa serikali kupitia Wizara ya Kilimo na Umwagiliaji, imeona ni bora fedha zinazotumika kununua mafuta Nje ya Nchi kwa bei ghali,itolewe mikopo kwa vikundi vya wakulima wanaolima zao la alizeti ili kuwasaidia wakulima wa zao la alizeti,kulima zao hilo kwa uhakika na kwa viwango vinavyokubalika ili uzalishaji wa mafuta uwe wa kutosha.

“Halmashauri kupitia idara ya Kilimo na Maendeleo ya jamii inatoa mikopo hiyo kwa wakulima ili kuwawezesha wakulima wa zao la alizeti ambao kwa sasa uzalishaji wake ni kidogo ili waweze kuzalisha alizeti kwa wingi,lakini pia lengo la pili ni kuwainua wakulima kiuchumi ili waweze kuhudumia familia zao.Kwa sasa mikopo inayotolewa ni kiasi kidogo lakini endapo vikundi hivi vikirejesha mikopo hiyo kwa uaminifu kiwango cha mikopo hiyo kitaongezwa”, alisema Tarimo.

Naye Afisa Maendeleo ya Jamii, Bw. John Mwamahonje amewataka wakulima hao kutokubadili matumizi ya  mikopo hiyo, na ili kufanikisha suala hilo vikundi vijitaidi kulima kwa pamoja ili kurahisisha ufuatiliaji.Kwa kikundi kitachofanya marejesho kwa uaminifu wataongezewa kiwango cha mkopo,kwani mikopo hiyo haina riba na endapo wakifanyia kazi kwa uaminifu na umakini watapata faida na kujipatia mtaji utaowawezesha kuzalisha zaidi msimu wa kilimo unaofuata.

Aidha Bw. Mwamahonje amewataka wakulima hao  kuzingatia matumizi sahihi ya mbolea, kuzingatia muda sahihi wa kupanda mbegu na palizi, kusafisha shamba kwa wakati wote hadi wakati wa mavuno,kupanda mbegu kwa nafasi kwa kuzingatia vipimo vya kitaalamu. kutokupuliza dawa ya kuua magugu baada ya alizeti kuota kwani kwa kufanya hivyo mimea itateketea maana alizeti inafanana na magugu,kufukia mbolea wakati wa kukuzia ili virutubisho visipotee lakini pia kukuzia mazao wakati ardhi ina unyevu na sio wakati wa jua kali na mambo mengine ambayo yanaweza kuharibu mazao kama ambavyo wameelekezwa na wakufunzi wa mafunzo hayo Bw. Joshua ivan na Bw. Jovinatus Frednand wa makampuni ya ocp na Zambia Seed ambayo yanazalisha pembejeo za kilimo (Mbolea na Mbegu za alizeti).

MWISHO.

Matangazo

  • Ujio wa Mwenge wa Uhuru 2025, bado siku 13 April 19, 2025
  • Ujio wa Mwenge wa Uhuru 2025, bado siku 12. April 20, 2025
  • Ujio wa Mwenge wa Uhuru 2025, bado siku 11. April 21, 2025
  • Ujio wa Mwenge wa Uhuru 2025, bado siku 10. April 22, 2025
  • Fungua

Habari Mpya

  • Wataalamu na viongozi watakiwa kusimamia upatikanaji na utoaji wa huduma za chanjo.

    April 25, 2025
  • Makambako yang'ara katika tuzo za Afya ya Usafi wa Mazingira ngazi ya Halmashauri za Miji.

    April 09, 2025
  • Jumla ya Miti 15,000 kupandwa Halmashauri ya Mji Makambako kuelekea siku ya Miti duniani mwaka 2025.

    March 15, 2025
  • Maadhimisho ya siku ya wanawake duniani 2025 Mkoa wa Njombe, Mila kandamizi zaelezwa kuwa kikwazo cha ustawi na uwezeshaji

    March 09, 2025
  • Fungua

Video

Shule mpya ya Mbugani Kitandililo sekondari kupitia mradi wa SEQUIP
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Fursa za Usafirishaji
  • Orodha ya Madiwani
  • Uzalishaji wa Umeme wa Upepo
  • Organisation Structure
  • Fursa za Biashara
  • By Laws
  • Permanent Committee

Tovuti Mashuhuri

  • Tovuti ya Ikulu ya Rais
  • Tovuti ya Ofisi ya Utumishi
  • Tovuti ya TAMISEMI
  • Tovuti ya Ofisi ya Takwimu ya Taifa (NBS)
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Open Data Tanzania

Wasomaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Makambako Town Council

    Anuani ya Posta: P.O.BOX 405 Makambako

    Simu ya mezani: 026-2730044

    Simu ya Kiganjani: 0785635383

    Barua pepe: td@makambakotc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Haki miliki ©2017 Halmashauri ya Mji Makambako. Haki zote zimehifadhiwa