• Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
HALMASHAURI YA MJI WA MAKAMBAKO
HALMASHAURI YA MJI WA MAKAMBAKO

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA HALMASHAURI YA MJI WA MAKAMBAKO

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Ardhi na maliasili
      • Raslimali watu na Utawala
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Usafi na mazingira
      • Elimu ya Msingi
      • Ujenzi na Uokoaji
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Elimu ya Sekondari
      • Kilimo, Ushirika na umwagiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maji
    • Vitengo
      • Sheria
      • ICT and Public relations
      • Ugavi na Manunuzi
      • Mkaguzi wa ndani
      • Ufugaji Nyuki
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma ya Afya
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Huduma za Jamii
      • Kamati ya Maadili
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Mipango Miji na Mazingira
    • Ratiba
      • Ratiba ya kumwona Mwenyekiti wa Halmashauri
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
  • Miradi
    • Miradi iliyo kwenye Mpango
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Ripoti mbalimbali
    • Mikataba
    • Mpango Mkakati
    • Hatua
    • Fomu za maombi
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Hotuba
    • Habari Mpya
    • Matukio
    • jarida la mji

Wananchi wa Makambako watakiwa kutunza mazingira kwa kupanda miti kupunguza athari za upepo mkali

Tarehe iliyowekwa: January 30th, 2026

Na. Lina Sanga

Wito huo umetolewa leo na Mkuu wa Wilaya ya Njombe,Mhe. Juma Sweda akitoa salamu za Serikali katika Mkutano wa Baraza la Madiwani kwa kipindi cha kuishia Robo ya pili kwa mwaka wa fedha 2025/2026 katika Halmashauri ya Mji Makambako uliofanyika katika ukumbi wa mikutano wa ofisi ya Kata ya Lyamkena.

Mhe. Sweda amesema kuwa,ipo haja kwa Kitengo cha mazingira kuandaa program maalum ili kuhamasisha  wananchi kupanda miti kwenye makazi yao ili kupunguza athari zinazotokana na upepo mkali kipindi cha mvua kwani kwa sasa Mji wa Makambako unakabiliwa na uharibifu wa mazingira kwa ukataji wa miti kwa kasi na kusababisha ukame unaopelekea ukosefu wa maji.

Pia,amesisitiza utoaji wa mikopo ya asilimia 10 kutolewa kwa msawazo kwa kila Kata ili kuwafikia walengwa kila Kata pamoja na kuendelea kutoa elimu kwa wananchi kuhusu mikopo inayotolewa na benki ya NMB na CRDB ambazo ni fedha za Serikali zinazokopeshwa kwa riba ndogo ili wanaokosa fedha zinazotolewa na Halmashauri wakakope benki.

Lakini pia, ametoa rai kwa viongozi wa Mitaa na vijiji kubainisha wanafunzi ambao hawajaripoti shuleni kuhakikisha wanaripoti shuleni kwa kubainisha wanafunzi waliofaulu kujiunga sekondari ni wangapi na wapo wapi, kwa kutambua sharia na sera ya elimu kuwa kila mtoto ana haki ya kupata elimu na kuwataka wazazi kutowatumikisha watoto kwenye kazi kama gereji kwani ni kinyume cha sheria.

Pamoja na hayo ameitaka Halmashauri ya Mji Makambako kuhakikisha miradi viporo yote iliyopokea fedha inakamilika pamoja na kuitaka Halmashauri kuweka mikakati ya kukusanya mapato zaidi kwani Makambako kwa sasa inakuwa kwa kasi na inahitaji mipango mikubwa inayohitaji fedha.

Mwisho ametoa wito kwa sekta ya Afya kuweka mikakati ya namna bora ya kutekeleza sera ya bima ya afya kwa wote ili kuepuka malalamiko ya wananchi,kwani wananchi wanalipa kabla ya kupata huduma na kuagiza sekta hiyo kuandaa mpango kazi wa namna watatoa huduma kwa wananchi.

Naye,Makamu Mwenyekiti wa Halmashauri ya Mji Makambako Mhe. Robert Shejamabu kwa niaba ya baraza la Madiwani amemuhakikishia Mkuu wa Wilaya kuwa maelekezo yote wameyapokea na wapo tayari kuyafanyia kazi kwa bidii.

Matangazo

  • Ujio wa Madaktari bingwa Hospitali ya Mji Makambako (Mlowa) September 17, 2025
  • Mapokezi ya ajira mpya januari 2026 January 25, 2026
  • Tangazo la kazi 2024 March 11, 2024
  • Mkutano wa uhamasishaji zoezi la urasimishaji Kata ya Kitisi na Majengo juni 27 - 29,2024 May 28, 2024
  • Fungua

Habari Mpya

  • Baraza la Madiwani lamshukuru Rais Samia kwa fedha za miradi na Mbunge kwa kutekeleza shughuli za maendeleo

    January 30, 2026
  • Wananchi wa Makambako watakiwa kutunza mazingira kwa kupanda miti kupunguza athari za upepo mkali

    January 30, 2026
  • Fungeni mita za maji za luku kumaliza malalamiko ya wananchi kuzidishiwa bili

    January 27, 2026
  • Miradi ya maendeleo yazidi kuleta mageuzi Halmashauri ya Mji Makambako

    January 25, 2026
  • Fungua

Video

Shule mpya ya Mbugani Kitandililo sekondari kupitia mradi wa SEQUIP
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Fursa za Usafirishaji
  • Orodha ya Madiwani
  • Uzalishaji wa Umeme wa Upepo
  • Organisation Structure
  • Fursa za Biashara
  • By Laws
  • Permanent Committee

Tovuti Mashuhuri

  • Tovuti ya Ikulu ya Rais
  • Tovuti ya Ofisi ya Utumishi
  • Tovuti ya TAMISEMI
  • Tovuti ya Ofisi ya Takwimu ya Taifa (NBS)
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Open Data Tanzania

Wasomaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Makambako Town Council

    Anuani ya Posta: P.O.BOX 405 Makambako

    Simu ya mezani: 026-2730044

    Simu ya Kiganjani: 0785635383

    Barua pepe: td@makambakotc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Haki miliki ©2017 Halmashauri ya Mji Makambako. Haki zote zimehifadhiwa