• Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
HALMASHAURI YA MJI WA MAKAMBAKO
HALMASHAURI YA MJI WA MAKAMBAKO

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA HALMASHAURI YA MJI WA MAKAMBAKO

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Ardhi na maliasili
      • Raslimali watu na Utawala
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Usafi na mazingira
      • Elimu ya Msingi
      • Ujenzi na Uokoaji
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Elimu ya Sekondari
      • Kilimo, Ushirika na umwagiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maji
    • Vitengo
      • Sheria
      • ICT and Public relations
      • Ugavi na Manunuzi
      • Mkaguzi wa ndani
      • Ufugaji Nyuki
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma ya Afya
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Huduma za Jamii
      • Kamati ya Maadili
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Mipango Miji na Mazingira
    • Ratiba
      • Ratiba ya kumwona Mwenyekiti wa Halmashauri
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
  • Miradi
    • Miradi iliyo kwenye Mpango
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Ripoti mbalimbali
    • Mikataba
    • Mpango Mkakati
    • Hatua
    • Fomu za maombi
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Hotuba
    • Habari Mpya
    • Matukio
    • jarida la mji

Wizara ya afya kupunguza gharama ya kumuona daktari

Tarehe iliyowekwa: August 10th, 2022

Na. Lina Sanga

Njombe

Taarifa hiyo imetolewa na Waziri wa Afya,Mhe. Ummy Mwalimu Mkoani Njombe,katika Mkutano wa hadhara uliofanyika leo katika  Viwanja vya sabasaba. 

Mhe. Ummy amesema kuwa Wizara ya Afya ina deni la kupunguza gharama za kupata huduma za  matibabu nchini kama ilivyofanyika kwenye mbolea,Sekta ya afya ina wajibu wakuwapunguzia mzigo watanzania wa kulipa fedha nyingi kwa ajili ya kupata huduma ya afya kwani huduma za afya ni huduma na sio biashara hivyo gharama za kumuona daktari zitashushwa.

"Kumuona daktari tu unalipa elfu kumi na tano kwa sababu gani? Mhe. Rais timu yangu tayari  inafanya tathimini na tutashusha gharama za kumuona daktari ili kuwapunguzia mzigo watanzania kama ulivyotuelekeza kwa sababu afya sio biashara bali huduma,"amesema Mhe. Ummy.

Kuhusu vitambulisho vya matibabu kwa wazee wasio na uwezo,Mhe. Ummy amesema kuwa sera ya afya inasema matibabu kwa wazee wasio na uwezo ni bure,lakini kuna baadhi ya watumishi wanakiuka maelekezo na miongozo ya Serikali ya kuhakikisha wazee wasio na uwezo wanapata matibabu bure.

Ametoa agizo kwa Wakurugenzi wa Halmashauri zote na Waganga wakuu wa Mikoa na Wilaya kuhakikisha wazee wasio na uwezo wanapewa vitambulisho vya matibabu bure ,na vitambulisho hivyo viheshimiwe sio mzee anapofika kwenye kituo cha afya kupata huduma aambiwe dawa hakuna wakati dawa zipo.

Pia,amesema kuwa Wizara inatambua   bado wanahitaji kubeba gharama za kutoa huduma za afya ikiwemo kwa kina mama wajawazito na wanaamini bima  ya afya kwa kila mtu itasaidia kuondoa changamoto ya wazee wasio na uwezo,wajawazito na watoto chini ya miaka mitano kupata huduma za afya bila kikwazo cha fedha.

Mwisho amewahakikishia  wana Njombe kuwa sekta ya afya itaendelea kutekeleza wajibu wake  wa kuhakikisha wananchi wanapata huduma bora za afya,watu hawatakwenda tena  Mbeya,Dar es salaam au Dodoma kwa ajili ya baadhi ya vipimo na huduma za kusafisha damu zitapatikana  ndani ya Mkoa wa Njombe hakutakuwa na haja ya kwenda Mbeya au Dar es salaam tena.

Mwisho ametoa wito kwa Watanzania kupata chanjo ya Uviko 19 ili kuwa salama, takwimu za  kitaifa  hadi jana agosti 9,jumla ya watanzania  waliochanja  ni  Mil 15.5 wenye umri kuanzia miaka 18 na kuendelea ambayo ni sawa na asilimia 50.53 na Mkoa wa Njombe una asilimia 46 ya watu waliopata chanjo ya Uviko 19.

Matangazo

  • Ujio wa Mwenge wa Uhuru 2025, bado siku 13 April 19, 2025
  • Ujio wa Mwenge wa Uhuru 2025, bado siku 12. April 20, 2025
  • Ujio wa Mwenge wa Uhuru 2025, bado siku 11. April 21, 2025
  • Ujio wa Mwenge wa Uhuru 2025, bado siku 10. April 22, 2025
  • Fungua

Habari Mpya

  • Wataalamu na viongozi watakiwa kusimamia upatikanaji na utoaji wa huduma za chanjo.

    April 25, 2025
  • Makambako yang'ara katika tuzo za Afya ya Usafi wa Mazingira ngazi ya Halmashauri za Miji.

    April 09, 2025
  • Jumla ya Miti 15,000 kupandwa Halmashauri ya Mji Makambako kuelekea siku ya Miti duniani mwaka 2025.

    March 15, 2025
  • Maadhimisho ya siku ya wanawake duniani 2025 Mkoa wa Njombe, Mila kandamizi zaelezwa kuwa kikwazo cha ustawi na uwezeshaji

    March 09, 2025
  • Fungua

Video

Shule mpya ya Mbugani Kitandililo sekondari kupitia mradi wa SEQUIP
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Fursa za Usafirishaji
  • Orodha ya Madiwani
  • Uzalishaji wa Umeme wa Upepo
  • Organisation Structure
  • Fursa za Biashara
  • By Laws
  • Permanent Committee

Tovuti Mashuhuri

  • Tovuti ya Ikulu ya Rais
  • Tovuti ya Ofisi ya Utumishi
  • Tovuti ya TAMISEMI
  • Tovuti ya Ofisi ya Takwimu ya Taifa (NBS)
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Open Data Tanzania

Wasomaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Makambako Town Council

    Anuani ya Posta: P.O.BOX 405 Makambako

    Simu ya mezani: 026-2730044

    Simu ya Kiganjani: 0785635383

    Barua pepe: td@makambakotc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Haki miliki ©2017 Halmashauri ya Mji Makambako. Haki zote zimehifadhiwa