• Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
HALMASHAURI YA MJI WA MAKAMBAKO
HALMASHAURI YA MJI WA MAKAMBAKO

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA HALMASHAURI YA MJI WA MAKAMBAKO

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Ardhi na maliasili
      • Raslimali watu na Utawala
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Usafi na mazingira
      • Elimu ya Msingi
      • Ujenzi na Uokoaji
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Elimu ya Sekondari
      • Kilimo, Ushirika na umwagiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maji
    • Vitengo
      • Sheria
      • ICT and Public relations
      • Ugavi na Manunuzi
      • Mkaguzi wa ndani
      • Ufugaji Nyuki
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma ya Afya
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Huduma za Jamii
      • Kamati ya Maadili
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Mipango Miji na Mazingira
    • Ratiba
      • Ratiba ya kumwona Mwenyekiti wa Halmashauri
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
  • Miradi
    • Miradi iliyo kwenye Mpango
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Ripoti mbalimbali
    • Mikataba
    • Mpango Mkakati
    • Hatua
    • Fomu za maombi
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Hotuba
    • Habari Mpya
    • Matukio
    • jarida la mji

Wizara ya kilimo kukutana na wakulima na wanunuzi wa chai Mkoa wa Njombe Mwezi septemba mwaka huu

Tarehe iliyowekwa: August 10th, 2022

Na. Lina Sanga

Njombe

Mwezi septemba mwaka huu Wizara ya Kilimo itakutana na wakulima wa zao la chai wa Mkoa wa Njombe na wanunuzi wote wa chai ili kupitia upya mfumo wa bei ya chai na  kuzitazama upya bei ya chai.

Hayo yameelezwa na Waziri wa Kilimo,Hussein Bashe katika Mkutano wa hadhara uliofanyika leo katika viwanja vya sabasaba Mkoani Njombe wakati akitoa salamu kwa Mhe. Samia Suluhu Hassan,Rais wa Jamhuri ya Tanzania.

Mhe. Bashe amesema kuwa chai  ni moja ya mazao yaliyopata misukosuko hivyo sababu ya kupitia upya bei  zipo, kwani Serikali inatoa ruzuku ya mbolea hivyo estate zote na wanunuzi wote wa chai watakua sehemu ya wanufaika wa bei ya ruzuku na gharama ya uzalishaji zitapungua.

Amesema kuwa,chai imekuwa ikiuzwa kupitia mnada wa Mombasa,Serikali ya awamu ya sita kwa kushirikiana na kampuni ya Mtanzania inayoitwa Bravo inaanzisha mnada wa kuuza chai unafunguliwa Dar es salaam,na magodauni yameanza kuandaliwa na mfumo wa kuuza chai umeanza na mikataba yote ya kuuza chai itasajiliwa katika soko la chai la Tanzania ili kujua bei halisi ya chai inayouzwa nje ili kutambua bei anayopata mkulima.

Aidha,amemuagiza mkuu wa mkoa wa Njombe Anthony Mtaka kutafuta ardhi zisizopungua jumla ya ekari 40,000,fedha zilizotolewa kwa Wizara ya Kilimo kwa  ajili ya kufungua mashamba ya vijana, zitawekezwa Njombe na kuanzisha kituo cha kuzalisha Mbegu ukanda wa nyanda za juu kusini kwa ajili ya uzalishaji wa mbegu za ngano, na maombi ya awali mil. 400 zilizotengwa kwa ajili ya kuzalisha mbegu za ukanda wa baridi yameshafanyika ili kuanza hatua ya uzalishaji mbegu.

Ameongeza kuwa mwongozo utaoongoza sekta ya parachichi umeshatengenezwa,kwa ajili ya kuongoza msimu wa parachichi, bei ya kuanzia,madaraja ya parachichi,viwango vya parachichi ili wanunuzi wanapojngia sokoni kuwe na chombo cha kuwaongoza ili kuona ushindani wa haki sokoni na mazao yanachumwa kwa viwango vinavyotakiwa.

Ametoa rai  kwa wakulima kuacha kuwauzia madalali parachichi ambazo hazijakomaa kwani zinaua soko la nje,na kuwataka wakuu wa Wilaya na Wakurugenzi kusimamia Mwongozo utaotolewa ili parachichi zote zifungwe zikiwa zimekomaa na zimeiva ili kutouwa soko la nje.

Matangazo

  • Ujio wa Mwenge wa Uhuru 2025, bado siku 13 April 19, 2025
  • Ujio wa Mwenge wa Uhuru 2025, bado siku 12. April 20, 2025
  • Ujio wa Mwenge wa Uhuru 2025, bado siku 11. April 21, 2025
  • Ujio wa Mwenge wa Uhuru 2025, bado siku 10. April 22, 2025
  • Fungua

Habari Mpya

  • Wataalamu na viongozi watakiwa kusimamia upatikanaji na utoaji wa huduma za chanjo.

    April 25, 2025
  • Makambako yang'ara katika tuzo za Afya ya Usafi wa Mazingira ngazi ya Halmashauri za Miji.

    April 09, 2025
  • Jumla ya Miti 15,000 kupandwa Halmashauri ya Mji Makambako kuelekea siku ya Miti duniani mwaka 2025.

    March 15, 2025
  • Maadhimisho ya siku ya wanawake duniani 2025 Mkoa wa Njombe, Mila kandamizi zaelezwa kuwa kikwazo cha ustawi na uwezeshaji

    March 09, 2025
  • Fungua

Video

Shule mpya ya Mbugani Kitandililo sekondari kupitia mradi wa SEQUIP
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Fursa za Usafirishaji
  • Orodha ya Madiwani
  • Uzalishaji wa Umeme wa Upepo
  • Organisation Structure
  • Fursa za Biashara
  • By Laws
  • Permanent Committee

Tovuti Mashuhuri

  • Tovuti ya Ikulu ya Rais
  • Tovuti ya Ofisi ya Utumishi
  • Tovuti ya TAMISEMI
  • Tovuti ya Ofisi ya Takwimu ya Taifa (NBS)
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Open Data Tanzania

Wasomaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Makambako Town Council

    Anuani ya Posta: P.O.BOX 405 Makambako

    Simu ya mezani: 026-2730044

    Simu ya Kiganjani: 0785635383

    Barua pepe: td@makambakotc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Haki miliki ©2017 Halmashauri ya Mji Makambako. Haki zote zimehifadhiwa