• Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
HALMASHAURI YA MJI WA MAKAMBAKO
HALMASHAURI YA MJI WA MAKAMBAKO

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA HALMASHAURI YA MJI WA MAKAMBAKO

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Ardhi na maliasili
      • Raslimali watu na Utawala
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Usafi na mazingira
      • Elimu ya Msingi
      • Ujenzi na Uokoaji
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Elimu ya Sekondari
      • Kilimo, Ushirika na umwagiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maji
    • Vitengo
      • Sheria
      • ICT and Public relations
      • Ugavi na Manunuzi
      • Mkaguzi wa ndani
      • Ufugaji Nyuki
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma ya Afya
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Huduma za Jamii
      • Kamati ya Maadili
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Mipango Miji na Mazingira
    • Ratiba
      • Ratiba ya kumwona Mwenyekiti wa Halmashauri
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
  • Miradi
    • Miradi iliyo kwenye Mpango
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Ripoti mbalimbali
    • Mikataba
    • Mpango Mkakati
    • Hatua
    • Fomu za maombi
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Hotuba
    • Habari Mpya
    • Matukio
    • jarida la mji

Ziara ya Madiwani wa Halmashauri ya Mji Makambako Halmashauri ya Manispaa ya Kahama.

Tarehe iliyowekwa: September 5th, 2023

Na. Lina Sanga - Kahama

Baraza la Madiwani Halmashauri ya Mji Makambako leo limefanya ziara ya Kikazi,katika Halmashauri ya Manispaa ya Kahama yenye lengo la kujifunza masuala mbalimbali ya Uendeshaji wa Halmashauri ikiwa ni pamoja na ukusanyaji Mapato,uwekezaji na ukuzaji wa wananchi kiuchumi kupitia mapato ya ndani na Mikopo ya asilimia 10 iliyokuwa ikitolewa kwa vikundi vya  Vijana,Wanawake na watu Wenye Ulemavu.


Katika ziara hiyo Wahe. Madiwani pamoja na baadhi ya wakuu wa idara na vitengo,wamepata fursa ya kutembelea eneo la uwekezaji wa viwanda la Ummy Mwalimu lenye ukubwa wa ekari 500,ambalo limetengwa kwa ajili ya viwanda vidogovidogo kwa mtu mmoja mmoja na vikundi.

Katika eneo la Ummy Mwalimu kuna baadhi ya vijana ambao ni wanufaika wa mikopo ya asilimia 10,ambao kwa sasa wanamiliki viwanda vidogo vya kutengeneza samani za ndani na kuzalisha ajira kwa vijana wengine ili kuunga mkono jitihada za Serikali za kuwawezesha vijana kiuchumi  na wananchi kwa ujumla.

"Tulitenga maeneo kwa ajili ya uwekezaji wa viwanda vidogo vidogo kwa kutoa maeneo bure kwa vijana wanaojitambua na fedha walizonazo kutumia kufanya uwekezaji,Halmashauri tulitoa hati ya kiwanja ambayo mnufaika aliweza kwenda benki na saccos kupata mkopo na kufanya uwekezaji,Halmashauri tunakusanya mapato,kodi na ushuru wa huduma baada ya kuwawezesha wananchi wetu kiuchumi na kuhakikisha tunanunua bidhaa zao ili wakue kutoka nafasi moja hadi nyingine na tumefanikiwa pakubwa"alisema Anderson Msumba, Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Kahama.

Kupitia ziara hiyo Wahe. Madiwani pamoja na Wakuu wa idara na vitengo wamepata nafasi ya kutembelea maeneo ya uwekezaji uliofanywa na vijana katika eneo la Ummy Mwalimu na stendi ndogo ya mabasi ambayo imesheheni vibanda vilivyojengwa na wajasiriamali wadogo ambao walikuwa maeneo yasiyo rasmi na kwa sasa wamepata eneo rasmi kwa ajiri ya biashara na wanapata mikopo kupitia benki na saccos kwa urahisi na kulipa mapato ya Serikali baada ya kuwezeshwa kiuchumi.


Matangazo

  • Ujio wa Mwenge wa Uhuru 2025, bado siku 13 April 19, 2025
  • Ujio wa Mwenge wa Uhuru 2025, bado siku 12. April 20, 2025
  • Ujio wa Mwenge wa Uhuru 2025, bado siku 11. April 21, 2025
  • Ujio wa Mwenge wa Uhuru 2025, bado siku 10. April 22, 2025
  • Fungua

Habari Mpya

  • Wataalamu na viongozi watakiwa kusimamia upatikanaji na utoaji wa huduma za chanjo.

    April 25, 2025
  • Makambako yang'ara katika tuzo za Afya ya Usafi wa Mazingira ngazi ya Halmashauri za Miji.

    April 09, 2025
  • Jumla ya Miti 15,000 kupandwa Halmashauri ya Mji Makambako kuelekea siku ya Miti duniani mwaka 2025.

    March 15, 2025
  • Maadhimisho ya siku ya wanawake duniani 2025 Mkoa wa Njombe, Mila kandamizi zaelezwa kuwa kikwazo cha ustawi na uwezeshaji

    March 09, 2025
  • Fungua

Video

Shule mpya ya Mbugani Kitandililo sekondari kupitia mradi wa SEQUIP
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Fursa za Usafirishaji
  • Orodha ya Madiwani
  • Uzalishaji wa Umeme wa Upepo
  • Organisation Structure
  • Fursa za Biashara
  • By Laws
  • Permanent Committee

Tovuti Mashuhuri

  • Tovuti ya Ikulu ya Rais
  • Tovuti ya Ofisi ya Utumishi
  • Tovuti ya TAMISEMI
  • Tovuti ya Ofisi ya Takwimu ya Taifa (NBS)
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Open Data Tanzania

Wasomaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Makambako Town Council

    Anuani ya Posta: P.O.BOX 405 Makambako

    Simu ya mezani: 026-2730044

    Simu ya Kiganjani: 0785635383

    Barua pepe: td@makambakotc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Haki miliki ©2017 Halmashauri ya Mji Makambako. Haki zote zimehifadhiwa