Na. Tanessa Lyimo
Mwenyekiti wa Halmashauri ya Mji Makambako ,Mhe.Salum Mlumbe ameongoza kikao cha Baraza la Madiwani katika kupitia na Kujadili bajeti ya bilioni 35.7 kwa Mwaka wa fedha 2026/2027 kikao kilichofanyika Leo,katika Ukumbi wa Ofisi ya Kata ya Lyamkena, Halmashauri ya Mji Makambako.

Mhe.Mlumbe amewapongeza wataalam na watendaji kwa kuchakata rasimu ya mpango na Bajeti ambayo imeweza kupitiwa na ngazi mbalimbali za uongozi, na kuidhinishwa na baraza la madiwani ili ikasaidie na kunufaisha jamii katika utekelezaji wenye dhamira ya kuleta maendeleo.
Pia amewapongeza wataalam kwa kuzingatia vipaumbele ikiwemo ya Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan ya mikopo ya asilimia 10 inayotolewa na Halmashauri kupitia mapato ya ndani kwa vikundi vya wanawake,vijana na watu wenye ulemavu
Ametoa wito kwa wananchi kuendelea kulipa ushuru na kodi mbalimbali za Serikali ili kuisaidia Halmashauri kuongeza mapato,na kuiwezesha kutekeleza miradi itakayoweza kusaidia jamii katika nyanja mbalimbali.
Naye Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji Makambako Ndg.Kenneth Haule ameahidi kuyafanyia kazi yote ambayo yamejadiliwa kwa maslahi ya halmashauri, kwa lengo la kutimiza azma na kusudi la rasimu ya mpango na bajeti kwa kutoa mrejesho kwa wananchi kupitia waheshimiwa madiwani.

Kuidhinishwa kwa Rasimu ya mpango na Bajeti kwa mwaka wa Fedha 2026/2027 itawezesha Halmashauri kutekeleza majukumu ya kila siku ikiwa ni pamoja na kulipa mishahara watumishi, kutekeleza shughuli mbalimbali za kiutawala na kiutendaji pamoja na kutekeleza miradi ya maendeleo.
Makambako Town Council
Anuani ya Posta: P.O.BOX 405 Makambako
Simu ya mezani: 026-2730044
Simu ya Kiganjani: 0785635383
Barua pepe: td@makambakotc.go.tz
Haki miliki ©2017 Halmashauri ya Mji Makambako. Haki zote zimehifadhiwa