• Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
HALMASHAURI YA MJI WA MAKAMBAKO
HALMASHAURI YA MJI WA MAKAMBAKO

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA HALMASHAURI YA MJI WA MAKAMBAKO

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Ardhi na maliasili
      • Raslimali watu na Utawala
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Usafi na mazingira
      • Elimu ya Msingi
      • Ujenzi na Uokoaji
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Elimu ya Sekondari
      • Kilimo, Ushirika na umwagiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maji
    • Vitengo
      • Sheria
      • ICT and Public relations
      • Ugavi na Manunuzi
      • Mkaguzi wa ndani
      • Ufugaji Nyuki
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma ya Afya
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Huduma za Jamii
      • Kamati ya Maadili
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Mipango Miji na Mazingira
    • Ratiba
      • Ratiba ya kumwona Mwenyekiti wa Halmashauri
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
  • Miradi
    • Miradi iliyo kwenye Mpango
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Ripoti mbalimbali
    • Mikataba
    • Mpango Mkakati
    • Hatua
    • Fomu za maombi
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Hotuba
    • Habari Mpya
    • Matukio
    • jarida la mji

Baraza la Madiwani laishauri Menejimenti kuhusu uwekezaji.

Tarehe iliyowekwa: November 7th, 2023

Na. Lina Sanga

Baraza la Madiwani la Halmashauri ya Mji Makambako limeishauri Menejimenti kuendesha miradi ya uwekezaji kwa faida ili kuanzisha miradi mipya ya uwekezaji na kuongeza mapato ,badala ya kukopa kwa ajili ya kuanzisha miradi mipya ikiwa ni pamoja na ununuzi wa mzani katika soko la mazao lililopo Mtaa wa Makatani,Kata ya Lyamkena.

Ushauri huo umetolewa leo katika mkutano wa baraza la Madiwani katika kipindi cha kuishia robo ya kwanza (julai – septemba)katika mwaka wa fedha 2023/2024,uliyofanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Halmashauri.

Wakitoa ushauri huo kwa nyakati tofauti wajumbe wa baraza hilo wamesema kuwa, ombi la kukopa fedha kwa ajili  kuingizwa kwenye biashara ya  mzani ambao Halmashauri haijawai kuifanya halikubaliki,hivyo ni vema mradi huo ubinafsishwe au kujengwa  kwa mfumo wa jenga,tumia rejesha ili kutoa fursa kwa watu binafsi kuwekeza na Halmashauri kupata asilimia kadhaa.

Aidha, wameipongeza timu ya menejimenti kwa kubuni miradi kwa ajili ya kuongeza vyanzo vya mapato na kuishauri kujikita katika kusimamia miradi iliyopo ,ili fedha zinazozalishwa zitumike kwa ajili ya ukamilishaji wa maboma na kuanzisha miradi mipya ya uwekezaji.

Mhe. Hanana Mfikwa, Mwenyekiti wa Halmashauri ya Mji Makambako amesema kuwa,jambo la Halmashauri kujitegemea na kubuni miradi ni jambo la msingi na Halmashauri inahitaji kuanzisha  vyanzo vya mapato , ambavyo vitasaidia kupunguza adha ya kufukuzana  na wananchi  kwenye kodi mbalimbali , hivyo ni vema vyanzo vilivyopo makusanyo yake yatumike kununua mzani au kuingia ubia na mzabuni au mwananchi anayeweza kuweka mzani kwa mfumo wa jenga,tumia rejesha na sio kubinafsisha.

Amesema kuwa kubinafsisha kwa mtu binafsi kuweka mzani katika soko hilo haiwezekani ,kwani mwisho wa safari Halmashauri itakosa vyanzo vya mapato na kushindwa kubuni vyanzo vingine ,kwani vyanzo vyote vya mapato vitakuwa mikononi mwa wananchi na kuanza kukimbizana na wananchi kuhusu kodi.

Ameongeza kuwa,kwa sasa mambo yanayotakiwa kufanyika ni pamoja na uwekezaji wa Halmashauri, kwa Halmashauri kujipanga kuwekeza kupitia vyanzo vya mapato ambavyo imewekeza,hivyo kujenga kwa mfumo wa jenga,tumia,rejesha inawezekana vinginevyo Halmashauri ijenge mzani fedha zitakapo patikana.

Matangazo

  • Ujio wa Mwenge wa Uhuru 2025, bado siku 13 April 19, 2025
  • Ujio wa Mwenge wa Uhuru 2025, bado siku 12. April 20, 2025
  • Ujio wa Mwenge wa Uhuru 2025, bado siku 11. April 21, 2025
  • Ujio wa Mwenge wa Uhuru 2025, bado siku 10. April 22, 2025
  • Fungua

Habari Mpya

  • Wataalamu na viongozi watakiwa kusimamia upatikanaji na utoaji wa huduma za chanjo.

    April 25, 2025
  • Makambako yang'ara katika tuzo za Afya ya Usafi wa Mazingira ngazi ya Halmashauri za Miji.

    April 09, 2025
  • Jumla ya Miti 15,000 kupandwa Halmashauri ya Mji Makambako kuelekea siku ya Miti duniani mwaka 2025.

    March 15, 2025
  • Maadhimisho ya siku ya wanawake duniani 2025 Mkoa wa Njombe, Mila kandamizi zaelezwa kuwa kikwazo cha ustawi na uwezeshaji

    March 09, 2025
  • Fungua

Video

Shule mpya ya Mbugani Kitandililo sekondari kupitia mradi wa SEQUIP
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Fursa za Usafirishaji
  • Orodha ya Madiwani
  • Uzalishaji wa Umeme wa Upepo
  • Organisation Structure
  • Fursa za Biashara
  • By Laws
  • Permanent Committee

Tovuti Mashuhuri

  • Tovuti ya Ikulu ya Rais
  • Tovuti ya Ofisi ya Utumishi
  • Tovuti ya TAMISEMI
  • Tovuti ya Ofisi ya Takwimu ya Taifa (NBS)
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Open Data Tanzania

Wasomaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Makambako Town Council

    Anuani ya Posta: P.O.BOX 405 Makambako

    Simu ya mezani: 026-2730044

    Simu ya Kiganjani: 0785635383

    Barua pepe: td@makambakotc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Haki miliki ©2017 Halmashauri ya Mji Makambako. Haki zote zimehifadhiwa