• Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
HALMASHAURI YA MJI WA MAKAMBAKO
HALMASHAURI YA MJI WA MAKAMBAKO

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA HALMASHAURI YA MJI WA MAKAMBAKO

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Ardhi na maliasili
      • Raslimali watu na Utawala
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Usafi na mazingira
      • Elimu ya Msingi
      • Ujenzi na Uokoaji
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Elimu ya Sekondari
      • Kilimo, Ushirika na umwagiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maji
    • Vitengo
      • Sheria
      • ICT and Public relations
      • Ugavi na Manunuzi
      • Mkaguzi wa ndani
      • Ufugaji Nyuki
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma ya Afya
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Huduma za Jamii
      • Kamati ya Maadili
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Mipango Miji na Mazingira
    • Ratiba
      • Ratiba ya kumwona Mwenyekiti wa Halmashauri
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
  • Miradi
    • Miradi iliyo kwenye Mpango
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Ripoti mbalimbali
    • Mikataba
    • Mpango Mkakati
    • Hatua
    • Fomu za maombi
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Hotuba
    • Habari Mpya
    • Matukio
    • jarida la mji

CHANJO YA UVIKO 19 HAINA MADHARA WANA MAKAMBAKO JITOKEZENI KUCHANJA

Tarehe iliyowekwa: September 30th, 2021


Rai hiyo imetolewa na Katibu Tawala wa Wilaya ya Njombe (DAS),Emmanuel George wakati wa ufunguzi wa  semina  ya uhamasishaji wa chanjo ya uviko 19, iliyofanyika jana katika ukumbi wa mikutano wa halmashauri ya Mji Makambako.

Bw. Emmanuel  amesema kuwa serikali imeamua kuhamasisha watu kupata chanjo kutokana na dhana potofu kwa baadhi ya watu juu ya chanjo ya uviko 19 ambayo imepokelewa kwa mitazamo tofauti na chanjo zingine zilizowahi kutolewa kama chanjo ya tetenasi,surua na homa ya ini.

“Kila mtu atambue kuwa jukumu la kuhamasisha wengine kupata chanjo ya uviko 19  ili kupunguza kasi ya maambukizi na kupunguza idadi ya vifo kutokana na ugonjwa huu,kwani ambao walishapata maambukizi na kupona wanajua maumivu ya  ugonjwa huu,hivyo uhamasishaji uanzie katika ngazi ya kaya zetu na jamii kwa ujumla kwa kila mmoja kutambua umuhimu wa kujilinda na kuwalinda wengine” alisema Bw. Emmanuel.

Naye Mganga Mkuu wa Halmashauri ya Mji Makambako, Dtk. Alexander Mchome amesema kuwa katika halmashauri ya Mji Makambako wananchi waliopata chanjo ya uviko 19 ni 687 sawa na asilimia 16.3 ya  dozi lengwa 4220 ya J&J.

Dkt. Mchome  amebainisha kuwa watu wengi ambao bado hawajapata chanjo wanajificha kwenye kauli iliyowahi kutolewa na  Hayati John Pombe Magufuli aliyekuwa raisi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, aliposema kuwa tusiharakishe kupokea chanjo hadi tujiridhishe kama ni salama kwa watanzania,na kwa sasa wataalamu wamejiridhisha kuwa ni salama ndio maana wananchi wanahamasishwa kuchanja.

Akitolea ufafanuzi wa suala la kuganda kwa damu kama ambavyo watu wengine wanavyohofia,Dkt Mchome amesema kuwa wapo baadhi ya watu wanakabiliwa na tatizo la kuganda kwa damu hata kabla ya kupata chanjo,hivyo watu wajitokeze kupata chanjo hiyo kwani wataalamu wameshajiridhisha kuwa haina madhara kwa watu.


Akitolea ufafanuzi wa uzushi unaosambazwa mitaani juu ya chanjo hiyo, Mratibu wa huduma za chanjo katika halmashauri ya Mji Makambako,Tindichebwa Mazala Amesema kuwa sio kweli kwamba mtu aliyepata chanjo atageuka kuwa zombie kama watu wengine wanavyosema,wala hakuna sumaku kwenye mwili wa mtu aliyepata chanjo na chanjo hiyo haibadilishi vinasaba vya mtu wala kusababisha matatizo ya uzazi kama ugumba na upungufu wa nguvu za kiume,watu wajitokeze kupata chanjo ili kujilinda wao wenyewe na wanaowazunguka.

Semina hiyo iliwashirikisha madiwani,watumishi wa umma,viongozi wa dini na serikali,Viongozi wa wafanyabiashara,viongozi wa bodaboda na bajaji.  

#TOKOMEZA UVIKO 19



Matangazo

  • Ujio wa Mwenge wa Uhuru 2025, bado siku 13 April 19, 2025
  • Ujio wa Mwenge wa Uhuru 2025, bado siku 12. April 20, 2025
  • Ujio wa Mwenge wa Uhuru 2025, bado siku 11. April 21, 2025
  • Ujio wa Mwenge wa Uhuru 2025, bado siku 10. April 22, 2025
  • Fungua

Habari Mpya

  • Wataalamu na viongozi watakiwa kusimamia upatikanaji na utoaji wa huduma za chanjo.

    April 25, 2025
  • Makambako yang'ara katika tuzo za Afya ya Usafi wa Mazingira ngazi ya Halmashauri za Miji.

    April 09, 2025
  • Jumla ya Miti 15,000 kupandwa Halmashauri ya Mji Makambako kuelekea siku ya Miti duniani mwaka 2025.

    March 15, 2025
  • Maadhimisho ya siku ya wanawake duniani 2025 Mkoa wa Njombe, Mila kandamizi zaelezwa kuwa kikwazo cha ustawi na uwezeshaji

    March 09, 2025
  • Fungua

Video

Shule mpya ya Mbugani Kitandililo sekondari kupitia mradi wa SEQUIP
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Fursa za Usafirishaji
  • Orodha ya Madiwani
  • Uzalishaji wa Umeme wa Upepo
  • Organisation Structure
  • Fursa za Biashara
  • By Laws
  • Permanent Committee

Tovuti Mashuhuri

  • Tovuti ya Ikulu ya Rais
  • Tovuti ya Ofisi ya Utumishi
  • Tovuti ya TAMISEMI
  • Tovuti ya Ofisi ya Takwimu ya Taifa (NBS)
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Open Data Tanzania

Wasomaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Makambako Town Council

    Anuani ya Posta: P.O.BOX 405 Makambako

    Simu ya mezani: 026-2730044

    Simu ya Kiganjani: 0785635383

    Barua pepe: td@makambakotc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Haki miliki ©2017 Halmashauri ya Mji Makambako. Haki zote zimehifadhiwa