Na. Lina Sanga
Kauli hiyo ilitolewa jana na Mhe.Deo Kasenyenda Sanga,Mbunge wa jimbo la Makambako alipokuwa akihutubia wananchi katika ziara yake katika Kijiji cha Mawande,Kata ya Utengule.
Mhe. Sanga alisema kuwa,katika mwaka wa fedha 2023/2024 Halmashauri ya Mji Makambako, imepata mgawa wa Mil. 55.7 za fedha za mfuko wa jimbo ambazo zimegawanywa kila Kata kulingana na mahitaji.
"Ipo kamati ya Mfuko wa jimbo ambayo inakuwa na Mbunge ambaye ni Mwenyekiti na Katibu afisa mipango,fedha hizo zinaletwa mara moja tu kwa mwaka sio mara nne kama wanavyosema huko mitaani na mwaka huu Mhe. Samia ametupa mil. 55 katika jimbo letu na tumeshazigawa kwa kila Kata kuna Kata zimepata Mil. 4.5, zingine Mil. 4,Mil. 3 na Kata ya Mlowa imepata Mil. 14 kulingana na mahitaji",alisema Mhe. Sanga.
Aidha,alibainisha kuwa fedha anazochangia katika shughuli za maendeleo,sio za mfuko wa Jimbo ni fedha kutoka kwenye kampuni yake ya Jah people ili kuunga mkono juhudi za Serikali.
Ametoa shukrani kwa Mhe. Samia Suluhu Hassan,Rais wa jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kuongeza fedha za mfuko wa jimbo la Makambako kutoka Mil. 32.3 hadi Mil. 55.7 kwa mwaka huu wa fedha.
Makambako Town Council
Anuani ya Posta: P.O.BOX 405 Makambako
Simu ya mezani: 026-2730044
Simu ya Kiganjani: 0785635383
Barua pepe: td@makambakotc.go.tz
Haki miliki ©2017 Halmashauri ya Mji Makambako. Haki zote zimehifadhiwa