• Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
HALMASHAURI YA MJI WA MAKAMBAKO
HALMASHAURI YA MJI WA MAKAMBAKO

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA HALMASHAURI YA MJI WA MAKAMBAKO

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Ardhi na maliasili
      • Raslimali watu na Utawala
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Usafi na mazingira
      • Elimu ya Msingi
      • Ujenzi na Uokoaji
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Elimu ya Sekondari
      • Kilimo, Ushirika na umwagiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maji
    • Vitengo
      • Sheria
      • ICT and Public relations
      • Ugavi na Manunuzi
      • Mkaguzi wa ndani
      • Ufugaji Nyuki
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma ya Afya
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Huduma za Jamii
      • Kamati ya Maadili
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Mipango Miji na Mazingira
    • Ratiba
      • Ratiba ya kumwona Mwenyekiti wa Halmashauri
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
  • Miradi
    • Miradi iliyo kwenye Mpango
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Ripoti mbalimbali
    • Mikataba
    • Mpango Mkakati
    • Hatua
    • Fomu za maombi
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Hotuba
    • Habari Mpya
    • Matukio
    • jarida la mji

Halmashauri ya Mji Makambako yapongezwa kwa kuvuka vizuri ukaguzi wa hesabu na kupata hati safi.

Tarehe iliyowekwa: June 16th, 2023

Na. Lina Sanga

Halmashauri ya Mji Makambako imepongezwa kwa kuvuka vizuri hatua  ya  ukaguzi wa hesabu za Serikali  na kupata hati safi mfululizo tangu kuanzishwa kwa Halmashauri  mwaka 2012.

Pongezi hizo zimetolewa leo na Katibu Tawala Mkoa wa Njombe,Bi. Judica Omari kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Njombe,Mhe. Anthony Mtaka katika mkutano maalum wa baraza la madiwani la kupitia mpango kazi na majibu ya menejimenti kwa ajili ya utekelezaji wa hoja za mdhibiti mkuu wa hesabu za Serikali kuishia juni 30,2022.

Judica amesema kuwa,kupata hati safi mfululizo ni kiashiria kikubwa cha uwepo wa ushirikiano baina ya Madiwani na wataalamu  katika kusimamia miongozo,sheria na kanuni katika usimamizi fedha zilizopo kwenye bajeti na utekelezaji wa  miradi  ya maendeleo ambayo imepokea fedha nyingi kutoka Serikali kuu na kuhakikisha inakamilika kwa wakati.

Aidha,ameipongeza Halmashauri ya Mji Makambako kwa kufikia asilimia 95 ya ukusanyaji wa mapato  na kutoa rai kwa Menejimenti kuhakikisha asilimia 5 iliyobaki inapatikana na kufikia asilimia 100 ya ukusanyaji wa mapato ifikapo juni 30,mwaka huu.

Naye,Willy Undule, Mkaguzi Mkuu wa hesabu  Mkoa wa Njombe, amepongeza na kutoa rai kwa Halmashauri ya Mji Makambako  kuendeleza ushirikiano katika utendaji kazi ili kuendelea kupata hati safi na kuhakikisha hoja zilizobaki zinafungwa.

Awali akiwasilisha taarifa ya kupitia mpango kazi na majibu ya menejimenti kwa ajili ya utekelezaji wa hoja za Mdhibiti Mkuu wa hesabu za Serikali, Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji Makambako,Kenneth Haule amesema kuwa,katika taarifa ya ukaguzi wa hesabu kwa mwaka 2021/2022 Halmashauri ilikuwa na jumla ya hoja 20,kati ya hizo hoja 15 zilijibiwa na kufungwa na hoja 5 zilizobaki utekelezaji umefanyika kwa sehemu na ufuatiliaji unaendelea kufanyika.

Pia, katika taarifa ya hesabu za mradi wa mfuko wa Afya wa pamoja kwa mwaka 2021/2022,Halmashauri ilikuwa na jumla ya hoja 4,kati ya hizo hoja 3 zimejibiwa na kufungwa na hoja 1 iliyobaki utekelezaji wake umefanyika kwa sehemu.

Aidha,katika taarifa  ya hesabu za mradi wa mfuko wa wanawake, Vijana na watu wenye ulemavu kwa mwaka 2021/2022,Halmashauri ilikuwa na jumla ya hoja 5,kati ya hizo hoja 3 zimejibiwa na kufungwa na hoja 2 utekelezaji wake umefanyika kwa sehemu.

Matangazo

  • Ujio wa Mwenge wa Uhuru 2025, bado siku 13 April 19, 2025
  • Ujio wa Mwenge wa Uhuru 2025, bado siku 12. April 20, 2025
  • Ujio wa Mwenge wa Uhuru 2025, bado siku 11. April 21, 2025
  • Ujio wa Mwenge wa Uhuru 2025, bado siku 10. April 22, 2025
  • Fungua

Habari Mpya

  • Wataalamu na viongozi watakiwa kusimamia upatikanaji na utoaji wa huduma za chanjo.

    April 25, 2025
  • Makambako yang'ara katika tuzo za Afya ya Usafi wa Mazingira ngazi ya Halmashauri za Miji.

    April 09, 2025
  • Jumla ya Miti 15,000 kupandwa Halmashauri ya Mji Makambako kuelekea siku ya Miti duniani mwaka 2025.

    March 15, 2025
  • Maadhimisho ya siku ya wanawake duniani 2025 Mkoa wa Njombe, Mila kandamizi zaelezwa kuwa kikwazo cha ustawi na uwezeshaji

    March 09, 2025
  • Fungua

Video

Shule mpya ya Mbugani Kitandililo sekondari kupitia mradi wa SEQUIP
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Fursa za Usafirishaji
  • Orodha ya Madiwani
  • Uzalishaji wa Umeme wa Upepo
  • Organisation Structure
  • Fursa za Biashara
  • By Laws
  • Permanent Committee

Tovuti Mashuhuri

  • Tovuti ya Ikulu ya Rais
  • Tovuti ya Ofisi ya Utumishi
  • Tovuti ya TAMISEMI
  • Tovuti ya Ofisi ya Takwimu ya Taifa (NBS)
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Open Data Tanzania

Wasomaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Makambako Town Council

    Anuani ya Posta: P.O.BOX 405 Makambako

    Simu ya mezani: 026-2730044

    Simu ya Kiganjani: 0785635383

    Barua pepe: td@makambakotc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Haki miliki ©2017 Halmashauri ya Mji Makambako. Haki zote zimehifadhiwa