Na. Lina Sanga
Katibu Tawala Mkoa wa Njombe, Dkt. Stephen Nindi amewaahidi watumishi na wananchi wa Mkoa wa Njombe kushirikiana nao katika ujenzi wa Njombe bora, kupitia uzoefu,nguvu,maarifa na ubunifu alioupata katika utumishi wake kwenye sekta mbalimbali alizowahi kuzitumikia kabla ya uteuzi wa kuwa Katibu Tawala Mkoa wa Njombe.
Dkt. Nindi amezungumza hayo leo wakati wa hafla ya mapokezi yake yaliyofanyika katika ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Njombe, na kuwashukuru watumishi kwa mapokezi mazuri na kuwa ahidi kushirikiana katika mambo mbalimbali ili kuwatumikia wananchi wa Mkoa wa Njombe na Taifa kwa ujumla.
Awali,Mkuu wa Mkoa wa Njombe, Mhe. Anthony Mtaka alimhakikishia Dkt. Nindi utayari na umakini wa watumishi wa Mkoa wa Njombe katika utekelezaji wa shughuli mbalimbali za maendeleo na kiutawala, na kuwataka watumishi wote kuwa tayari kufanya mabadiliko na maamuzi sahihi kwa maslahi ya wananchi.
Naye, Mkuu wa Wilaya ya Njombe, Mhe. Juma Sweda amemkaribisha Dkt. Nindi na kumhakikishia ushirikiano wenye tija unaotekeleza maono ya Rais wa jamhuri ya Muungano wa Tanzania pamoja na kutatua changamoto za wananchi.
Mapokezi ya Dkt. Nindi yamehusisha watumishi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa na timu za menejimenti za Halmashauri zote ndani Mkoa wa Njombe
Makambako Town Council
Anuani ya Posta: P.O.BOX 405 Makambako
Simu ya mezani: 026-2730044
Simu ya Kiganjani: 0785635383
Barua pepe: td@makambakotc.go.tz
Haki miliki ©2017 Halmashauri ya Mji Makambako. Haki zote zimehifadhiwa