• Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
HALMASHAURI YA MJI WA MAKAMBAKO
HALMASHAURI YA MJI WA MAKAMBAKO

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA HALMASHAURI YA MJI WA MAKAMBAKO

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Ardhi na maliasili
      • Raslimali watu na Utawala
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Usafi na mazingira
      • Elimu ya Msingi
      • Ujenzi na Uokoaji
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Elimu ya Sekondari
      • Kilimo, Ushirika na umwagiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maji
    • Vitengo
      • Sheria
      • ICT and Public relations
      • Ugavi na Manunuzi
      • Mkaguzi wa ndani
      • Ufugaji Nyuki
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma ya Afya
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Huduma za Jamii
      • Kamati ya Maadili
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Mipango Miji na Mazingira
    • Ratiba
      • Ratiba ya kumwona Mwenyekiti wa Halmashauri
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
  • Miradi
    • Miradi iliyo kwenye Mpango
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Ripoti mbalimbali
    • Mikataba
    • Mpango Mkakati
    • Hatua
    • Fomu za maombi
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Hotuba
    • Habari Mpya
    • Matukio
    • jarida la mji

Halmashauri ya Mji Makambako yasaini mikataba ya lishe leo.

Tarehe iliyowekwa: October 26th, 2022

Na. Lina Sanga

Mikataba ya lishe itakayotumika kwa miaka nane,imesainiwa leo katika Halmashauri ya Mji Makambako na Mkurugenzi pamoja na Watendaji wa Kata 12 zilizopo katika Mji wa Makambako.

Kabla ya Utiaji saini wa Mikataba hiyo,Mada zinazohusu lishe ziliwasilishwa na Katibu wa Afya wa Halmashauri ya Mji Makambako,Benedict Musiba sambamba na Afisa Lishe Meckfrida Mmari ili kuwajengea uelewa Watendaji juu ya majukumu yao katika usimamizi wa Lishe kwenye Kata zao ili kufanikisha uboreshaji wa lishe kwa watoto chini ya miaka mitano.

Mkoa wa Njombe unakabiliwa na tatizo la Udumavu kwa asilimia 53.6, hali inayoelezwa kuchangiwa na lishe duni kwa watoto chini ya miaka mitano ambapo Halmashauri ya Mji Makambako asilimia 0.9 ya watoto wana tatizo la udumavu na asilimia 0.7 wanakabiliwa na tatizo la ukondefu, unaosababishwa na ukosefu wa virutubisho muhimu katika chakula.

Ili kukabiliana na tatizo la udumavu na ukondefu kwa watoto chini ya miaka mitano,Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji Makambako,Kenneth Haule ametoa agizo kwa Afisa lishe na Maafisa elimu Msingi na Sekondari kuhakikisha kila shule inakuwa na vitalu vya mbogamboga na matunda badala ya maua,ili zitumike katika vyakula vya wanafunzi shuleni.

Pia,amemuagiza Kaimu  Mganga Mkuu wa Halmashauri ya Mji Makambako,Dkt. Ally Senga kuhakikisha Watendaji wa Kata,Mitaa na Vijiji wanashirikiana na Kamati za Afya katika utekelezaji wa majukumu mbalimbali yanayohusu afya na lishe katika Mitaa na vijiji ili kuwajengea uwezo Watendaji wa kutoa elimu ya lishe kwa wananchi.

Aidha,Halmashauri ya Mji Makambako imetenga zaidi ya Mil. 26 kwa mwaka wa Fedha 2022/2023 ambapo mapato ya ndani ni Mil. 18 ikiwa ni fedha kwa ajili ya lishe ya   watoto  shuleni, ambapo kila mtoto anatengewa wastani wa shilingi 1,000 ikiwa ni agizo la Serikali.

Matangazo

  • Ujio wa Madaktari bingwa Hospitali ya Mji Makambako (Mlowa) September 17, 2025
  • Tangazo la kazi 2024 March 11, 2024
  • Mkutano wa uhamasishaji zoezi la urasimishaji Kata ya Kitisi na Majengo juni 27 - 29,2024 May 28, 2024
  • Mkutano wa uhamasishaji zoezi la urasimishaji Kata ya Mjimwema May 28, 2024
  • Fungua

Habari Mpya

  • Mil. 350.8 za Mikopo ya 10% zimetolewa kwa vikundi 30 Halmashauri ya Mji Makambako,DC aagiza mikopo hiyo kuwa chanzo cha utajiri.

    August 14, 2025
  • MIL 350.8 ZA MIKOPO YA 10% ZATOLEWA KWA AWAMU YA PILI KWA MWAKA 2024/2025.

    August 01, 2025
  • Wataalamu na viongozi watakiwa kusimamia upatikanaji na utoaji wa huduma za chanjo.

    April 25, 2025
  • Makambako yang'ara katika tuzo za Afya ya Usafi wa Mazingira ngazi ya Halmashauri za Miji.

    April 09, 2025
  • Fungua

Video

Shule mpya ya Mbugani Kitandililo sekondari kupitia mradi wa SEQUIP
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Fursa za Usafirishaji
  • Orodha ya Madiwani
  • Uzalishaji wa Umeme wa Upepo
  • Organisation Structure
  • Fursa za Biashara
  • By Laws
  • Permanent Committee

Tovuti Mashuhuri

  • Tovuti ya Ikulu ya Rais
  • Tovuti ya Ofisi ya Utumishi
  • Tovuti ya TAMISEMI
  • Tovuti ya Ofisi ya Takwimu ya Taifa (NBS)
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Open Data Tanzania

Wasomaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Makambako Town Council

    Anuani ya Posta: P.O.BOX 405 Makambako

    Simu ya mezani: 026-2730044

    Simu ya Kiganjani: 0785635383

    Barua pepe: td@makambakotc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Haki miliki ©2017 Halmashauri ya Mji Makambako. Haki zote zimehifadhiwa