• Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
HALMASHAURI YA MJI WA MAKAMBAKO
HALMASHAURI YA MJI WA MAKAMBAKO

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA HALMASHAURI YA MJI WA MAKAMBAKO

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Ardhi na maliasili
      • Raslimali watu na Utawala
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Usafi na mazingira
      • Elimu ya Msingi
      • Ujenzi na Uokoaji
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Elimu ya Sekondari
      • Kilimo, Ushirika na umwagiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maji
    • Vitengo
      • Sheria
      • ICT and Public relations
      • Ugavi na Manunuzi
      • Mkaguzi wa ndani
      • Ufugaji Nyuki
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma ya Afya
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Huduma za Jamii
      • Kamati ya Maadili
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Mipango Miji na Mazingira
    • Ratiba
      • Ratiba ya kumwona Mwenyekiti wa Halmashauri
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
  • Miradi
    • Miradi iliyo kwenye Mpango
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Ripoti mbalimbali
    • Mikataba
    • Mpango Mkakati
    • Hatua
    • Fomu za maombi
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Hotuba
    • Habari Mpya
    • Matukio
    • jarida la mji

Halmashauri ya Mji Makambako yashika nafasi ya Kwanza Tanzania Kwa Utendaji bora 2021/2022

Tarehe iliyowekwa: June 24th, 2022

Na. Lina Sanga

Halmashauri ya Mji Makambako  kupitia idara ya Utumishi na Utawala imepokea tuzo ya Utendaji bora kwa mwaka wa fedha 2021/2022 na kushika nafasi ya kwanza kati ya  halmashauri zote za  Miji Tanzania .

Tuzo hiyo ilitolewa na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi na Utawala Bora,Mh. Jenister Mhagama (MB) kwa halmashauri zilizofanya vizuri katika utendaji bora,katika kikao kazi kilichoitishwa na  Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi  wa Umma na Utawala bora kilichofanyika Jijini Dodoma Mei,2022.

Tuzo hiyo imewasilishwa leo na Mkurugenzi wa halmashauri ya Mji Makambako, Bw. Kenneth Haule  katika kikao maalumu cha Kamati ya Fedha na Uongozi kilichofanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa halmashauri amesema kuwa,tuzo hiyo imetolewa kwa halmashauri ya Mji Makambako baada ya kukidhi vigezo katika utekelezaji wa maagizo ya Serikali kwa wakati na kwa kufuata miongozo inayotolewa.

“Kutokuwa na malalamiko mengi yanayohusu masuala ya watumishi,kuwa na taarifa safi za watumishi,utoaji wa huduma bora kwa wakati na uzingatiaji wa maadili katika matumizi ya mifumo mbalimbali ya kiutumishi ni vigezo vikuu ambavyo vimeiwezesha halmashauri yetu kushika nafasi ya kwanza kati ya halmashauri zote za Mji Nchini”, alisema Haule.

Mwenyekiti wa halmashauri ya Mji Makambako ambaye pia ni Mwenyekiti wa  Kamati ya Fedha na Uongozi, Mhe. Hanana Mfikwa kwa niaba ya madiwani wote, amempongeza Mkurugenzi na timu ya Menejimenti,idara ya Utumishi na Utawala kwa utendaji bora wa majukumu mbalimbali na kufuata miongozo inayotolewa na Serikali na halmashauri ya Mji Makambako kuibuka mshindi kwa kushika nafasi ya kwanza ya Utendaji bora na kunyakua tuzo.

Matangazo

  • Ujio wa Mwenge wa Uhuru 2025, bado siku 13 April 19, 2025
  • Ujio wa Mwenge wa Uhuru 2025, bado siku 12. April 20, 2025
  • Ujio wa Mwenge wa Uhuru 2025, bado siku 11. April 21, 2025
  • Ujio wa Mwenge wa Uhuru 2025, bado siku 10. April 22, 2025
  • Fungua

Habari Mpya

  • Mil. 350.8 za Mikopo ya 10% zimetolewa kwa vikundi 30 Halmashauri ya Mji Makambako,DC aagiza mikopo hiyo kuwa chanzo cha utajiri.

    August 14, 2025
  • MIL 350.8 ZA MIKOPO YA 10% ZATOLEWA KWA AWAMU YA PILI KWA MWAKA 2024/2025.

    August 01, 2025
  • Wataalamu na viongozi watakiwa kusimamia upatikanaji na utoaji wa huduma za chanjo.

    April 25, 2025
  • Makambako yang'ara katika tuzo za Afya ya Usafi wa Mazingira ngazi ya Halmashauri za Miji.

    April 09, 2025
  • Fungua

Video

Shule mpya ya Mbugani Kitandililo sekondari kupitia mradi wa SEQUIP
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Fursa za Usafirishaji
  • Orodha ya Madiwani
  • Uzalishaji wa Umeme wa Upepo
  • Organisation Structure
  • Fursa za Biashara
  • By Laws
  • Permanent Committee

Tovuti Mashuhuri

  • Tovuti ya Ikulu ya Rais
  • Tovuti ya Ofisi ya Utumishi
  • Tovuti ya TAMISEMI
  • Tovuti ya Ofisi ya Takwimu ya Taifa (NBS)
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Open Data Tanzania

Wasomaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Makambako Town Council

    Anuani ya Posta: P.O.BOX 405 Makambako

    Simu ya mezani: 026-2730044

    Simu ya Kiganjani: 0785635383

    Barua pepe: td@makambakotc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Haki miliki ©2017 Halmashauri ya Mji Makambako. Haki zote zimehifadhiwa