• Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
HALMASHAURI YA MJI WA MAKAMBAKO
HALMASHAURI YA MJI WA MAKAMBAKO

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA HALMASHAURI YA MJI WA MAKAMBAKO

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Ardhi na maliasili
      • Raslimali watu na Utawala
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Usafi na mazingira
      • Elimu ya Msingi
      • Ujenzi na Uokoaji
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Elimu ya Sekondari
      • Kilimo, Ushirika na umwagiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maji
    • Vitengo
      • Sheria
      • ICT and Public relations
      • Ugavi na Manunuzi
      • Mkaguzi wa ndani
      • Ufugaji Nyuki
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma ya Afya
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Huduma za Jamii
      • Kamati ya Maadili
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Mipango Miji na Mazingira
    • Ratiba
      • Ratiba ya kumwona Mwenyekiti wa Halmashauri
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
  • Miradi
    • Miradi iliyo kwenye Mpango
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Ripoti mbalimbali
    • Mikataba
    • Mpango Mkakati
    • Hatua
    • Fomu za maombi
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Hotuba
    • Habari Mpya
    • Matukio
    • jarida la mji

Hongera Halmashauri ya Mji Makambako kwa ukamilishaji wa miradi-Mkurugenzi Msaidizi OR TAMISEMI

Tarehe iliyowekwa: July 5th, 2022

Na. Lina Sanga

Mkurugenzi msaidizi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI),Mhandisi Enock Nyanda ameipongeza Halmashauri ya Mji Makambako kwa utekelezaji mzuri wa miradi iliyopata fedha kutoka Serikali kuu.

Nyanda ametoa pongezi hizo  katika ziara ya ukaguzi wa miradi iliyopokea fedha kutoka Serikali kuu, iliyofanyika  leo katika Halmashauri ya Mji Makambako yenye lengo la kukagua ukamilishaji wa majengo ya madarasa, maabara,zahanati na hospitali na kulinganisha thamani ya fedha iliyotumika katika ukamilishaji wa majengo hayo.

Amesema kuwa ameridhishwa na ujenzi wa majengo yote aliyokagua na kutoa rai kwa Mkurugenzi,kuhakikisha majengo yaliyokamilika kuanza kutumika mara baada ya ujenzi kukamilika ili kutoa matokeo chanya kwa wanafunzi na jamii kwa kupata huduma na kunufaiki kupitia majengo hayo.

Kwa upande wa miradi ya ujenzi wa zahanati za vijiji na mitaa,Nyanda amesema kuwa baada ya majengo hayo kukamilika,yaanze kutoa huduma kwa jamii huku ukamilishaji wa miundombinu mingine ikiendelea kujengwa na changamoto ya nyumba za watumishi itafutiwe ufumbuzi na kuwaagiza watendaji wa Kata na Mitaa kwa kushirikiana na wajumbe wa  kamati za ujenzi,kuwatafutia watumishi nyumba za kupanga wakati mchakato wa ujenzi wa nyumba za watumishi ukiendelea hasa kwa maeneo ya pembezoni mwa mji.

Kuhusu Madarasa na Maabara,Mhandisi Nyanda ameipongeza Halmashauri ya Mji Makambako kwa kutumia vizuri fedha zilizoletwa kwa ajili ya ukamilishaji wa maabara na madarasa,kwa kuzingatia mahitaji halisi yaliyopo na kuokoa fedha kwa kiasi kikubwa na kuzitumia kupunguza uhaba wa majengo mengine na huduma muhimu  kama miundombinu ya maji shule ya sekondari mukilima,ofisi ya mwalimu mkuu shule ya msingi Ushindi  na matundu ya vyoo kwa ajili ya wanafunzi shule ya sekondari Deosanga na ujenzi wa maabara ya kisasa shule ya sekondari Makambako.

Ametoa wito kwa Mkurugenzi kukutana na menejimenti za shule na kujadiliana kuhusu kuongeza ufaulu wa wanafunzi,kwani Serikali imeshajenga madarasa na maabara jukumu lililobaki ni kuongezeka kwa ufaulu wa wanafunzi  pekee.

“Serikali inafarijika sana kuona ufaulu mzuri wa wanafunzi ukiongezeka kila mwaka,hivyo ni vema Mkurugenzi kukaa na walimu kujadiliana nao kuhusu mbinu za ujifunzaji na ufundishaji hasa kwa shule ambazo hazifanyi vizuri kwa sasa,ili kutambua changamoto zinazosababisha kupatikana kwa ufaulu hafifu wa baadhi ya wanafunzi lakini pia suala la ujenzi wa hosteli ni vema lianze kufikiriwa ili kuwasaidia wananfunzi kupata muda mwingi wa kujisomea”, alisema Nyanda.

Baadhi ya Miradi iliyopokea fedha kutoka Serikali kuu ni pamoja na ujenzi wa zahanati ya kijiji cha Mahongole  mil 50, Zahanati ya Maguvani  mil 50, Ukamilishaji wa darasa moja shule ya msingi Manga mil 21.2,Ujenzi wa maabara Maguvani sekondari  mil 25.9,Maabara lyamkena sekondari mil 25 na madarasa mawili yenye thamani ya mil 22.5, maabara Makambako sekondari mil 41,Mukilima sekondari maabara yenye thamani ya mil 25,ukamilishaji wa madarasa mawili Deosanga sekondari yenye thamani ya mil 10.4 pamoja na vyoo matundu 11 vyenye thamani ya mil 12.

Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji Makambako, Kenneth Haule pamoja na watumishi wa Hamashauri ya Mji Makambako wameishukuru Serikali  na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanazania, Mhe. Samia Suluhu Hassan kwa fedha zilizotolewa na kukamilisha maboma ya madarasa, zahanati na maabara kwa ajili ya masomo ya Sayansi,nakuahidi kutoa huduma bora kwa wananchi na kuongeza Ufaulu wa wanafunzi.

#jiandaekuhesabiwa2022

Matangazo

  • Ujio wa Mwenge wa Uhuru 2025, bado siku 13 April 19, 2025
  • Ujio wa Mwenge wa Uhuru 2025, bado siku 12. April 20, 2025
  • Ujio wa Mwenge wa Uhuru 2025, bado siku 11. April 21, 2025
  • Ujio wa Mwenge wa Uhuru 2025, bado siku 10. April 22, 2025
  • Fungua

Habari Mpya

  • Wataalamu na viongozi watakiwa kusimamia upatikanaji na utoaji wa huduma za chanjo.

    April 25, 2025
  • Makambako yang'ara katika tuzo za Afya ya Usafi wa Mazingira ngazi ya Halmashauri za Miji.

    April 09, 2025
  • Jumla ya Miti 15,000 kupandwa Halmashauri ya Mji Makambako kuelekea siku ya Miti duniani mwaka 2025.

    March 15, 2025
  • Maadhimisho ya siku ya wanawake duniani 2025 Mkoa wa Njombe, Mila kandamizi zaelezwa kuwa kikwazo cha ustawi na uwezeshaji

    March 09, 2025
  • Fungua

Video

Shule mpya ya Mbugani Kitandililo sekondari kupitia mradi wa SEQUIP
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Fursa za Usafirishaji
  • Orodha ya Madiwani
  • Uzalishaji wa Umeme wa Upepo
  • Organisation Structure
  • Fursa za Biashara
  • By Laws
  • Permanent Committee

Tovuti Mashuhuri

  • Tovuti ya Ikulu ya Rais
  • Tovuti ya Ofisi ya Utumishi
  • Tovuti ya TAMISEMI
  • Tovuti ya Ofisi ya Takwimu ya Taifa (NBS)
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Open Data Tanzania

Wasomaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Makambako Town Council

    Anuani ya Posta: P.O.BOX 405 Makambako

    Simu ya mezani: 026-2730044

    Simu ya Kiganjani: 0785635383

    Barua pepe: td@makambakotc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Haki miliki ©2017 Halmashauri ya Mji Makambako. Haki zote zimehifadhiwa