• Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
HALMASHAURI YA MJI WA MAKAMBAKO
HALMASHAURI YA MJI WA MAKAMBAKO

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA HALMASHAURI YA MJI WA MAKAMBAKO

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Ardhi na maliasili
      • Raslimali watu na Utawala
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Usafi na mazingira
      • Elimu ya Msingi
      • Ujenzi na Uokoaji
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Elimu ya Sekondari
      • Kilimo, Ushirika na umwagiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maji
    • Vitengo
      • Sheria
      • ICT and Public relations
      • Ugavi na Manunuzi
      • Mkaguzi wa ndani
      • Ufugaji Nyuki
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma ya Afya
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Huduma za Jamii
      • Kamati ya Maadili
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Mipango Miji na Mazingira
    • Ratiba
      • Ratiba ya kumwona Mwenyekiti wa Halmashauri
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
  • Miradi
    • Miradi iliyo kwenye Mpango
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Ripoti mbalimbali
    • Mikataba
    • Mpango Mkakati
    • Hatua
    • Fomu za maombi
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Hotuba
    • Habari Mpya
    • Matukio
    • jarida la mji

Kamati ya Fedha na Uongozi yampongeza mwanachama wa CHADEMA kushiriki uzimamizi wa mradi wa BOOST na kutimiza wajibu wake bila kujali itikadi za Vyama.

Tarehe iliyowekwa: July 24th, 2023

Na. Lina Sanga

Kamati ya Fedha na Uongozi ya Halmashauri ya Mji Makambako imempongeza  Bw. Anthony Mdekwa,mwanachama wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA),kwa kushiriki kikamilifu katika usimamizi wa Mradi wa kuimarisha ufundishaji na ujifunzaji kwa shule z awali na msingi(BOOST) akiwa moja kati ya wajumbe wa kamati ya ujenzi shule ya msingi Uhuru.

Pongezi hizo zimetolewa leo na  Mwenyekiti wa Halmashauri ya Mji Makambako,Mhe. Hanana Mfikwa pamoja na wajumbe wa Kamati ya Fedha na Uongozi,katika ziara ya ukaguzi wa miradi ya maendeleo katika kipindi cha kuishia  robo ya nne (aprili – juni) 2022/2023.

Mhe. Hanana amesema kuwa uwepo wa wananchi mbalimbali kutoka vyama tofauti vya siasa ni kiashiria cha ukomavu wa siasa nchini,kwa kutambua kuwa maendeleo hayana chama na kujitoa kuhakikisha fedha zilizotolewa na Serikali zinatumia kwa lengo lililokusudiwa.

Ametoa wito kwa wananchi kujitoa kushiriki shughuli mbalimbali katika miradi ya maendeleo inayopokea fedha kutoka Serikalini ili fedha zitoshe na kukamilisha miradi ,pamoja na kuimiliki miradi inayotekelezwa kwenye maeneo yao kwa kusimamia kwa ukaribu ili kuhakikisha inakamilika kwa wakati na kutokuwepo kwa ubadhirifu wowote.

Halmashauri ya Mji Makambako ilipokea Mil. 1.171 kwa ajili ya ujenzi wa madarasa,ofisi,jengo la utawala na matundu ya vyoo katika shule sita ambazo ni shule ya msingi Mshikamano, Uhuru, Umoja, Juhudi,Azimio na Magegele.

Shule ya Msingi Mshikamano  madarasa 6 na matundu 3 ya vyoo,Uhuru madarasa 6 na matundu 3 ya vyoo,Umoja madarasa 5 na matundu 3 ya vyoo,Juhudi madarasa 8 na matundu 6 ya vyoo, Magegele ujenzi wa madarasa 6 na matundu 6 ya vyoo na Azimio ujenzi wa shule mpya yenye mkondo mmoja wenye madarasa 7,jengo la utawala 1,matundu 10 ya vyoo,madarasa 2 na matundu ya vyoo 6 ya mfano kwa ajili ya wanafunzi wa darasa la awali pamoja na kichomea taka.

Matangazo

  • Kuitwa Kwenye Usaili septemba,2025 September 04, 2025
  • Tangazo la kazi 2024 March 11, 2024
  • Mkutano wa uhamasishaji zoezi la urasimishaji Kata ya Kitisi na Majengo juni 27 - 29,2024 May 28, 2024
  • Mkutano wa uhamasishaji zoezi la urasimishaji Kata ya Mjimwema May 28, 2024
  • Fungua

Habari Mpya

  • Mil. 350.8 za Mikopo ya 10% zimetolewa kwa vikundi 30 Halmashauri ya Mji Makambako,DC aagiza mikopo hiyo kuwa chanzo cha utajiri.

    August 14, 2025
  • MIL 350.8 ZA MIKOPO YA 10% ZATOLEWA KWA AWAMU YA PILI KWA MWAKA 2024/2025.

    August 01, 2025
  • Wataalamu na viongozi watakiwa kusimamia upatikanaji na utoaji wa huduma za chanjo.

    April 25, 2025
  • Makambako yang'ara katika tuzo za Afya ya Usafi wa Mazingira ngazi ya Halmashauri za Miji.

    April 09, 2025
  • Fungua

Video

Shule mpya ya Mbugani Kitandililo sekondari kupitia mradi wa SEQUIP
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Fursa za Usafirishaji
  • Orodha ya Madiwani
  • Uzalishaji wa Umeme wa Upepo
  • Organisation Structure
  • Fursa za Biashara
  • By Laws
  • Permanent Committee

Tovuti Mashuhuri

  • Tovuti ya Ikulu ya Rais
  • Tovuti ya Ofisi ya Utumishi
  • Tovuti ya TAMISEMI
  • Tovuti ya Ofisi ya Takwimu ya Taifa (NBS)
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Open Data Tanzania

Wasomaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Makambako Town Council

    Anuani ya Posta: P.O.BOX 405 Makambako

    Simu ya mezani: 026-2730044

    Simu ya Kiganjani: 0785635383

    Barua pepe: td@makambakotc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Haki miliki ©2017 Halmashauri ya Mji Makambako. Haki zote zimehifadhiwa