• Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
HALMASHAURI YA MJI WA MAKAMBAKO
HALMASHAURI YA MJI WA MAKAMBAKO

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA HALMASHAURI YA MJI WA MAKAMBAKO

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Ardhi na maliasili
      • Raslimali watu na Utawala
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Usafi na mazingira
      • Elimu ya Msingi
      • Ujenzi na Uokoaji
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Elimu ya Sekondari
      • Kilimo, Ushirika na umwagiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maji
    • Vitengo
      • Sheria
      • ICT and Public relations
      • Ugavi na Manunuzi
      • Mkaguzi wa ndani
      • Ufugaji Nyuki
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma ya Afya
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Huduma za Jamii
      • Kamati ya Maadili
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Mipango Miji na Mazingira
    • Ratiba
      • Ratiba ya kumwona Mwenyekiti wa Halmashauri
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
  • Miradi
    • Miradi iliyo kwenye Mpango
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Ripoti mbalimbali
    • Mikataba
    • Mpango Mkakati
    • Hatua
    • Fomu za maombi
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Hotuba
    • Habari Mpya
    • Matukio
    • jarida la mji

Kampeni ya Chanjo dhidi ya Ugonjwa wa Polio Kutolewa Nyumba kwa Nyumba,Mtoto kwa Mtoto

Tarehe iliyowekwa: March 19th, 2022

Ugonjwa wa Polio ni ugonjwa unaosababishwa na Virusi vya Polio, ambavyo huenezwa kwa njia ya kula na kunywa maji yaliyochafuliwa na kinyesi,na njia pekee ya kuudhibiti ugonjwa huu ni chanjo kwani mpaka sasa tiba haijapatikana.

Akizungumza katika semina ya kamati ya afya kuhusu chanjo dhidi ya polio,iliyofanyika leo katika ukumbi wa mikutano wa Halmashauri ya Mji Makambako,Dr. George Kanki ambaye ni Afisa Mfuatiliaji wa Magonjwa ya Mlipuko Nchini kutoka  Shirika la Afya Duniani (WHO), amesema kuwa katika nchi jirani ya Malawi Mgonjwa mmoja amegundulika kuwa na ugonjwa wa polio,hivyo mikoa iliyopo karibu na Nchi hiyo inatakiwa watoto wote kuanzia umri wa miaka sifuri hadi miaka mitano lazima wapate chanjo hiyo ili kuudhibiti ugonjwa huo na kampeni hii itafanyika nyumba kwa nyumba, mtoto kwa mtoto ili kuhakikisha watoto wote wamepata chanjo na kuwekewa alama ya wino ili kurahisisha uhakiki wa watoto waliopata chanjo na ambao hawajapata chanjo.

Dr. Kanki amesema kuwa Shirika la Afya Duniani linaichukulia kampeni ya chanjo  dhidi ya polio kuwa ni muhimu sana kwani ugonjwa huo unasababisha mgonjwa kupooza na kupata ulemavu wa kudumu hata kifo,na ili kuutokomeza ugonjwa huo ni lazima watoto wapewe chanjo dhidi ya polio kwa awamu nne na endapo mlipuko umetokea kama sasa haijalishi mtoto ambaye amepata chanjo zote awamu nne au moja au siku moja baada ya Mlipuko ni lazima apewe chanjo tena.

“Mgonjwa wa polio aliyepatikana Malawi ,haijulikani amepita mikoa gani na Nchi gani,huenda alifika hadi upande wa Tanzania ndiyo maana Serikali imeamua mikoa iliyo karibu na Nchi hiyo kutolewa chanjo haraka ili kuzuia maambukizi kutokea ndani ya nchi yetu,hivyo mikoa ya Mbeya, Songwe, Njombe na Ruvuma watoto wote lazima wapate chanjo ili kuwakinga na maambukizi ya ugonjwa huo”,alisema Dr. Kanki.

Samweli Vianga ambaye nia Afisa afya katika Halmashauri ya Mji Makambako na Mwezeshaji katika semina hiyo,amesema kuwa kampeni ya chanjo hiyo imefanyika tofauti na miaka mingine ambapo Wazazi walikuwa na wajibu wa kuwapeleka watoto wao, katika vituo vya kutolea huduma ya afya kupata chanjo ya polio ,kwa sasa kampeni hiyo itafanyika nyumba kwa nyumba kwa sababu ya tishio la Nchi jirani ya Malawi juu ya uwepo wa Ugonjwa huo na lengo la pili ni kuwatafuta watoto chini ya umri wa miaka mitano waliopata ulemavu wa gafla (tepetepe).

Mwaka 2015 Nchi ya Tanzania ilipata cheti cha mafanikio ya kuutokomeza ugonjwa wa polio na Mwaka 2020 Bara la Afrika lilikuwa huru kwa maradhi haya ya polio na kupewa cheti kuonyesha mafanikio ya kuutokomeza ugonjwa huu katika Bara lote la Afrika baada ya Nchi ya Nigeria kukubali chanjo Dhidi ya Polio,na duniani kote ugonjwa huu ulikuwa umeshatokomezwa isipokuwa nchi mbili tu,nchi ya Pakistan na Afganistan kutokana na uwepo wa vita na pingamizi lakini dunia yote ilitarajia endapo ugonjwa wa polio ukitokomezwa katika nchi hizo mbili  dunia ingekuwa imefanikiwa  kutokomeza  ugonjwa wa polio kama ilivyofanikiwa kuutokomeza ugonjwa wa ndui.

Kampeni ya Chanjo dhidi ya polio inatarajiwa kufanyika kwa siku nne kuanzia Machi 24,2022 hadi Machi 27, 2022 katika Halmashauri ya Mji Makambako endapo mwitikio utakua hafifu kampeni hiyo itaendelea hadi kufikia malengo ya utoaji wa Chanjo hiyo.

Semina hiyo ilihudhuriwa na Afisa Mpango wa Taifa wa chanjo kutoka Wizara ya Afya, Katibu Tawala wa Wilaya ya Njombe,Mkuu wa Polisi wilaya ya Kipolisi Makambako(OCD),Viongozi wa madhehebu ya Dini mbalimbali,Mwakilishi wa Wafanyabiashara,Mwakilishi wa Wataalamu wa tiba asili pamoja na wataalamu wa Idara mbalimbali katika  Halmashauri ya Mji Makambako.

Mwisho.

Matangazo

  • Ujio wa Mwenge wa Uhuru 2025, bado siku 13 April 19, 2025
  • Ujio wa Mwenge wa Uhuru 2025, bado siku 12. April 20, 2025
  • Ujio wa Mwenge wa Uhuru 2025, bado siku 11. April 21, 2025
  • Ujio wa Mwenge wa Uhuru 2025, bado siku 10. April 22, 2025
  • Fungua

Habari Mpya

  • Wataalamu na viongozi watakiwa kusimamia upatikanaji na utoaji wa huduma za chanjo.

    April 25, 2025
  • Makambako yang'ara katika tuzo za Afya ya Usafi wa Mazingira ngazi ya Halmashauri za Miji.

    April 09, 2025
  • Jumla ya Miti 15,000 kupandwa Halmashauri ya Mji Makambako kuelekea siku ya Miti duniani mwaka 2025.

    March 15, 2025
  • Maadhimisho ya siku ya wanawake duniani 2025 Mkoa wa Njombe, Mila kandamizi zaelezwa kuwa kikwazo cha ustawi na uwezeshaji

    March 09, 2025
  • Fungua

Video

Shule mpya ya Mbugani Kitandililo sekondari kupitia mradi wa SEQUIP
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Fursa za Usafirishaji
  • Orodha ya Madiwani
  • Uzalishaji wa Umeme wa Upepo
  • Organisation Structure
  • Fursa za Biashara
  • By Laws
  • Permanent Committee

Tovuti Mashuhuri

  • Tovuti ya Ikulu ya Rais
  • Tovuti ya Ofisi ya Utumishi
  • Tovuti ya TAMISEMI
  • Tovuti ya Ofisi ya Takwimu ya Taifa (NBS)
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Open Data Tanzania

Wasomaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Makambako Town Council

    Anuani ya Posta: P.O.BOX 405 Makambako

    Simu ya mezani: 026-2730044

    Simu ya Kiganjani: 0785635383

    Barua pepe: td@makambakotc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Haki miliki ©2017 Halmashauri ya Mji Makambako. Haki zote zimehifadhiwa