• Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
HALMASHAURI YA MJI WA MAKAMBAKO
HALMASHAURI YA MJI WA MAKAMBAKO

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA HALMASHAURI YA MJI WA MAKAMBAKO

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Ardhi na maliasili
      • Raslimali watu na Utawala
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Usafi na mazingira
      • Elimu ya Msingi
      • Ujenzi na Uokoaji
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Elimu ya Sekondari
      • Kilimo, Ushirika na umwagiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maji
    • Vitengo
      • Sheria
      • ICT and Public relations
      • Ugavi na Manunuzi
      • Mkaguzi wa ndani
      • Ufugaji Nyuki
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma ya Afya
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Huduma za Jamii
      • Kamati ya Maadili
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Mipango Miji na Mazingira
    • Ratiba
      • Ratiba ya kumwona Mwenyekiti wa Halmashauri
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
  • Miradi
    • Miradi iliyo kwenye Mpango
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Ripoti mbalimbali
    • Mikataba
    • Mpango Mkakati
    • Hatua
    • Fomu za maombi
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Hotuba
    • Habari Mpya
    • Matukio
    • jarida la mji

Karibuni kuwekeza kilimo cha maua Mkoani Njombe - RC Mtaka

Tarehe iliyowekwa: September 26th, 2022


Na. Lina Sanga

Njombe

Mkuu wa Mkoa wa Njombe,Mhe. Anthony Mtaka ametoa wito kwa watu binafsi kufungua kampuni za utalii katika Mikoa ya Kusini,na kufanya shughuli za utalii katika mkoa wa Njombe pamoja na wawekezaji katika kilimo cha maua kwani hali ya hewa ya mkoa wa Njombe na Miundombinu inaruhusu.

Mhe. Mtaka ametoa wito huo leo katika hafla ya uzinduzi wa mikakati ya kutangaza utalii kusini mwa Tanzania,iliyofanyika leo katika Ukumbi wa mikutano wa Halmashauri ya Mji Njombe.

Amesema kuwa,Mkoa wa Njombe una hifadhi ya kitulo yenye maua mazuri,na kwa sasa soko la maua limekuwa hafifu na wawekezaji wa maua wameanza kwenda Nairobi kununua Maua.

Ametoa wito kwa wawekezaji wa kilimo cha maua kuwekeza Njombe kwani hali ya hewa ni rafiki,pia kuna vivutio vingi ikiwemo hifadhi ya kitulo na safu ya milima kipengere.

Ameongeza kuwa,utalii uliopo mikoa ya Kaskazini haukujiumba bali umejengwa na watu binafsi,hivyo utalii unajengwa na sekta binafsi ,Serikali  ina jukumu la kuweka  miundombinu na mazingira wezeshi.

Aidha amewataka wananchi wa Mkoa wa Njombe kuchangamkia fursa mbalimbali za utalii na kujipatia kipato,kwani baada ya miaka mitatu Mkoa wa Njombe hautarajii kuwa na wanufaika wa Tasaf  wanaotokana na uzembe.

“Mhe. Pindi Chana anakuja anakwambia  kilimo cha miti hulimi,,utalii hufanyi,viazi tunalima siku sitini hulimi,ngano siku sitini na tano hulimi,mchicha siku ishirini na moja hulimi,tunajenga shule usome bure husomi unakaa unasubiri Rais awape hela kutoka mbinguni,umezeeka nipo Tasaf kwa uzembe,kizazi hichi cha Tasaf ni cha mwisho hakuna hela ya Tasaf atayopewa mzembe labda kwa mlemavu wa viungo na tunaanza kutunza kumbukumbu kwenye mfumo wa kidigitali ”, alisema Mhe. Mtaka.

Amemuomba Waziri wa Maliasili na utalii kuziruhusu bodi kutembelea vivutio mbalimbali vya utalii vilivyopo katika Mkoa wa Njombe,ili kusaidia kuvitangaza vivutio hivyo,pamoja na kujifunza masuala mbalimbali ya utaliii kama vile nyumbu wanaohama kutoka Kenya kuja Tanzania pamoja na ndege wanaotoka Ulaya kuja hifadhi ya Kitulo iliyopo Makete.


Matangazo

  • Ujio wa Mwenge wa Uhuru 2025, bado siku 13 April 19, 2025
  • Ujio wa Mwenge wa Uhuru 2025, bado siku 12. April 20, 2025
  • Ujio wa Mwenge wa Uhuru 2025, bado siku 11. April 21, 2025
  • Ujio wa Mwenge wa Uhuru 2025, bado siku 10. April 22, 2025
  • Fungua

Habari Mpya

  • Wataalamu na viongozi watakiwa kusimamia upatikanaji na utoaji wa huduma za chanjo.

    April 25, 2025
  • Makambako yang'ara katika tuzo za Afya ya Usafi wa Mazingira ngazi ya Halmashauri za Miji.

    April 09, 2025
  • Jumla ya Miti 15,000 kupandwa Halmashauri ya Mji Makambako kuelekea siku ya Miti duniani mwaka 2025.

    March 15, 2025
  • Maadhimisho ya siku ya wanawake duniani 2025 Mkoa wa Njombe, Mila kandamizi zaelezwa kuwa kikwazo cha ustawi na uwezeshaji

    March 09, 2025
  • Fungua

Video

Shule mpya ya Mbugani Kitandililo sekondari kupitia mradi wa SEQUIP
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Fursa za Usafirishaji
  • Orodha ya Madiwani
  • Uzalishaji wa Umeme wa Upepo
  • Organisation Structure
  • Fursa za Biashara
  • By Laws
  • Permanent Committee

Tovuti Mashuhuri

  • Tovuti ya Ikulu ya Rais
  • Tovuti ya Ofisi ya Utumishi
  • Tovuti ya TAMISEMI
  • Tovuti ya Ofisi ya Takwimu ya Taifa (NBS)
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Open Data Tanzania

Wasomaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Makambako Town Council

    Anuani ya Posta: P.O.BOX 405 Makambako

    Simu ya mezani: 026-2730044

    Simu ya Kiganjani: 0785635383

    Barua pepe: td@makambakotc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Haki miliki ©2017 Halmashauri ya Mji Makambako. Haki zote zimehifadhiwa