• Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
HALMASHAURI YA MJI WA MAKAMBAKO
HALMASHAURI YA MJI WA MAKAMBAKO

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA HALMASHAURI YA MJI WA MAKAMBAKO

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Ardhi na maliasili
      • Raslimali watu na Utawala
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Usafi na mazingira
      • Elimu ya Msingi
      • Ujenzi na Uokoaji
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Elimu ya Sekondari
      • Kilimo, Ushirika na umwagiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maji
    • Vitengo
      • Sheria
      • ICT and Public relations
      • Ugavi na Manunuzi
      • Mkaguzi wa ndani
      • Ufugaji Nyuki
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma ya Afya
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Huduma za Jamii
      • Kamati ya Maadili
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Mipango Miji na Mazingira
    • Ratiba
      • Ratiba ya kumwona Mwenyekiti wa Halmashauri
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
  • Miradi
    • Miradi iliyo kwenye Mpango
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Ripoti mbalimbali
    • Mikataba
    • Mpango Mkakati
    • Hatua
    • Fomu za maombi
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Hotuba
    • Habari Mpya
    • Matukio
    • jarida la mji

KATA YA LYAMKENA YAIBUKA KINARA CHANJO YA UVIKO 19

Tarehe iliyowekwa: November 9th, 2021

Kata ya lyamkena iliyopo katika halmashauri ya Mji Makambako,imeibuka kinara katika zoezi la utoaji chanjo ya UVIKO 19, ya  J&J kwa kuvuka lengo la utoaji chanjo kama  ilivyokadiliwa kutoa chanjo 126, zilizotolewa kwa  kila kata  katika halmashauri ya Mji makambako ,kutokana na mwamko Mdogo wa wananchi waliokuwa wanajitokeza kupata chanjo.

Hayo yamebainishwa na Mganga Mkuu wa Halmashauri ya Mji Makambako, Dkt. Alexander Mchome katika kikao cha tathmini ya zoezi la utoaji chanjo ya UVIKO 19 ,katika halmashauri ya Mji Makambako na utambulisho wa chanjo ya Sinopharm.

Dkt. Mchome amesema kuwa kata ya Lyamkena imefanikiwa kuchanja jumla ya watu 185, na kufuatiwa na kata ya Mlowa ambayo imetoa chanjo 169 na kata ya Kitandililo imetoa chanjo 113 kati ya chanjo 126 ambazo zilitolewa kwa kila kata.

Akielezea jitihada zilizofanyika na kusaidia kutoa chanjo hizo,Diwani wa kata ya Lyamkena,Mhe. Salumu Mlumbe amesema kuwa kuitisha mikutano ya hadhara katika mitaa na kuwapa elimu wananchi kuhusu chanjo na viongozi wa kata kupata chanjo imesaidia kuwaaminisha wananchi kuwa chanjo hiyo ni salama na kuamua kuchanja baada ya kuona viongozi wao wanaowaongoza wamechanja  na hawajapata madhara yoyote.

Dkt. Mchome ametoa wito kwa wakazi wa Halmashauri ya Mji Makambako,kujitokeza  katika vituo vya kutolea chanjo ili kupata chanjo badala ya kusubiri kufuatwa kwenye makazi yao,kwani kwa kufika kituoni ni rahisi zaidi katika kufanikisha zoezi hilo tofauti na kumfuata mtu mmoja mmoja,lakini inapobidi kuwafuata watu kwenye maeneo ya wataalamu wa afya watafanya hivyo.

Aidha amewataka wananchi ambao hawajapata chanjo ya J&J kujitokeza kupata  chanjo ya sinopharm, ambayo imeletwa Nchini kutoka Nchini China baada ya chanjo ya J&J kuisha.

Akitolea ufafanuzi wa chanjo hiyo,Dkt Mchome amesema kuwa Chanjo ya sinopharm na J&J zote zinafanya kazi moja ya kuzalisha kinga dhidi ya kirusi cha UVIKO 19,tofauti yake ni utaalamu namna ya utengenezaji,ndio maana sinopharm ili mtu apate kinga kamili ni lazima apate dozi mbili za chanjo ambapo dozi ya pili itatolewa baada ya siku ishirini na nane tofauti na J&J ambayo inatolewa dozi moja tu.

“Chanjo ya sinopharm imetengenezwa na kirusi kilichouliwa kwa kemikali na kuondolewa uwezo wa kuambukiza ugonjwa wa UVIKO 19 kwa binadamu,na endapo mtu huyo akipata maambukizi ya UVIKO 19,mwili unakuwa salama kwa sababu chanjo aliyopata inatengeneza kinga za kuulinda mwili dhidi ya ugonjwa huo,na baada ya kuchoma chanjo ya sinopharm basi mtu huyo hatakiwi kuchoma chanjo ya aina yoyote hadi siku 14 tangu kuchoma chanjo ”alisema Dkt. Mchome.

Halmashauri ya Mji Makambako imepokea jumla ya chanjo 2100 za sinopharm,ambazo zitatolewa kwa watu wenye umri kuanzia miaka kumi na nane,kina mama wajawazito,wazee na hata watu wenye magonjwa mengine kwani wapo kwenye hatari ya kupata maambukizi ya UVIKO 19 kama watu wenye  magonjwa ya moyo,kisukari,figo,shinikizo la damu na Upungufu wa Kinga Mwilini (UKIMWI).

Watu wenye mzio na baadhi ya vitu  vilivyotumika kutengeneza chanjo ya sinopharm hawatapata chanjo hii pamoja na watu ambao watagundulika kuwa na maambukizi ya UVIKO 19 hawatapata chanjo ya sinopharm hadi  miezi sita baada ya kupata matibabu na kupona ugonjwa wa korona.

MWISHO.

 

Matangazo

  • Ujio wa Mwenge wa Uhuru 2025, bado siku 13 April 19, 2025
  • Ujio wa Mwenge wa Uhuru 2025, bado siku 12. April 20, 2025
  • Ujio wa Mwenge wa Uhuru 2025, bado siku 11. April 21, 2025
  • Ujio wa Mwenge wa Uhuru 2025, bado siku 10. April 22, 2025
  • Fungua

Habari Mpya

  • Wataalamu na viongozi watakiwa kusimamia upatikanaji na utoaji wa huduma za chanjo.

    April 25, 2025
  • Makambako yang'ara katika tuzo za Afya ya Usafi wa Mazingira ngazi ya Halmashauri za Miji.

    April 09, 2025
  • Jumla ya Miti 15,000 kupandwa Halmashauri ya Mji Makambako kuelekea siku ya Miti duniani mwaka 2025.

    March 15, 2025
  • Maadhimisho ya siku ya wanawake duniani 2025 Mkoa wa Njombe, Mila kandamizi zaelezwa kuwa kikwazo cha ustawi na uwezeshaji

    March 09, 2025
  • Fungua

Video

Shule mpya ya Mbugani Kitandililo sekondari kupitia mradi wa SEQUIP
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Fursa za Usafirishaji
  • Orodha ya Madiwani
  • Uzalishaji wa Umeme wa Upepo
  • Organisation Structure
  • Fursa za Biashara
  • By Laws
  • Permanent Committee

Tovuti Mashuhuri

  • Tovuti ya Ikulu ya Rais
  • Tovuti ya Ofisi ya Utumishi
  • Tovuti ya TAMISEMI
  • Tovuti ya Ofisi ya Takwimu ya Taifa (NBS)
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Open Data Tanzania

Wasomaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Makambako Town Council

    Anuani ya Posta: P.O.BOX 405 Makambako

    Simu ya mezani: 026-2730044

    Simu ya Kiganjani: 0785635383

    Barua pepe: td@makambakotc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Haki miliki ©2017 Halmashauri ya Mji Makambako. Haki zote zimehifadhiwa