• Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
HALMASHAURI YA MJI WA MAKAMBAKO
HALMASHAURI YA MJI WA MAKAMBAKO

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA HALMASHAURI YA MJI WA MAKAMBAKO

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Ardhi na maliasili
      • Raslimali watu na Utawala
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Usafi na mazingira
      • Elimu ya Msingi
      • Ujenzi na Uokoaji
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Elimu ya Sekondari
      • Kilimo, Ushirika na umwagiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maji
    • Vitengo
      • Sheria
      • ICT and Public relations
      • Ugavi na Manunuzi
      • Mkaguzi wa ndani
      • Ufugaji Nyuki
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma ya Afya
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Huduma za Jamii
      • Kamati ya Maadili
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Mipango Miji na Mazingira
    • Ratiba
      • Ratiba ya kumwona Mwenyekiti wa Halmashauri
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
  • Miradi
    • Miradi iliyo kwenye Mpango
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Ripoti mbalimbali
    • Mikataba
    • Mpango Mkakati
    • Hatua
    • Fomu za maombi
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Hotuba
    • Habari Mpya
    • Matukio
    • jarida la mji

Kikao cha Kamati ya Lishe cha Tarehe 24.03.2020

Tarehe iliyowekwa: March 24th, 2020

Halmashauri ya Mji wa Makambako inatekeleza afua mbali mbali za lishe kwa kuzingatia viashiria vilivyomo katika mkataba wa lishe, Lengo  ni kuhakikisha huduma bora za Lishe zinatolewa kwa walengwa/jamii  ili kuondokana na matatizo ya  utapiamlo hususani udumavu .

Mkoa wa Njombe unaongoza kwa kuwa na watoto wengi wenye ukosefu wa Lishe bora (Udumavu, ukondefu, uzito pungufu, n.k.)  Kikao cha Kamati ya Lishe  cha tarehe 24/03/2020 kilijadili : Taarifa ya utekelezaji wa Maazimio ya kikao cha Kamati ya Lishe ya Halmashauri kilichofanyika tarehe 29/11/2019, Taarifa ya utekelezaji wa shughuli  za lishe kwa kipindi cha robo ya pili Oktoba - Disemba 2019/2020,Taarifa ya utekelezaji wa viashiria vya mkataba wa lishe kipindi cha pili Oktoba - Disemba 2019/2020.

Taarifa ya utekelezaji wa Maazimio ya kikao cha Kamati ya Lishe ya Halmashauri kilichofanyika tarehe 29/11/2019

Utekelezaji wa maazimio ya Kikao cha Kamati ya Lishe kilichofanyika tarehe 29/11/2019, ulifanyika kama ifuatavyo: 

1. Kuhakikisha akina mama wajawazito wanapata kiwango sahihi cha madini chuma na asidi ya foliki: Idara ya afya kuendelea kuhamasisha jamii kuhusu umuhimu wa akina mama wajawazito kuwahi kuanza/kuhudhuria kliniki ili kuweza kupata nyongeza ya madini chuma na asidi ya foliki kwa kiwango sahihi kupitia wahudumu wa vituo vya kutolea huduma za afya,wahudumu ngazi ya jamii; kupitia mikutano ya vijiji/mitaa na kwenye nyumba za ibada na Radio(ICE FM).

2. Kuhakikisha watoto wenye utapiamlo mkali wanatambuliwa  mapema na kupatiwa matibabu: Kuendelea kushirikiana na serikali ya Vijiji/Mitaa pamoja na wahudumu wa afya ngazi ya jamii ili kuweza kuwabaini mapema watoto wote wenye utapiamlo na kupewa rufaa katika vituo vya kutolea huduma za afya kwa ajili ya kupata matibabu.

3. Idara ya elimu kushirikiana na afisa lishe watoe elimu katika shule za msingi kuhusu mpangilio wa vyakula ili kukidhi mahitaji ya lishe kwa wanafunzi: Elimu ilitolewa katika shule 14 kati ya 42 za Msingi kipindi cha robo ya pili 2019/2020(Ibatu,Mlenga,Kitandililo,Nyamande,Usetule,Mahongole,Manga,Kifumbe,Kahawa,Mashujaa,Juhudu,Nyambogo,Ikelu na Mtanga) Aidha shughuli ni endelevu.

4. Kuhakikisha kila idara imetenga fedha za utekelezaji wa afua za lishe kwa  mwaka  wa fedha 2020/2021 kwa kuzingatia miongozo iliyotolewa katika kikao cha maandalizi ya awali ya mipango na bajeti za afua za lishe kwani suala la lishe ni mtambuka: Idara husika zimezingatia agizo hilo ambapo jumla ya fedha zimetengwa  kwa utekelezaji wa afua za lishe kwa mwaka 2020/2021.

Taarifa ya utekelezaji wa shughuli  za lishe kwa kipindi cha robo ya pili Oktoba - Disemba 2019/2020

Utekelezwaji wa shughuli za lishe kwa kipindi cha robo ya pili Oktoba-Disemba 2019/2020 ulifanyika kama ifuatavyo:

1. Kufanya maadhimisho ya mwezi wa afya na lishe ya mtoto kwa kutoa matone ya Vitamin A na dawa za minyoo na upimaji wa hali ya lishe kwa watoto wa miezi 6-59: Jumla ya watoto 14,675 wenye umri miezi 6-59 walipata matone ya Vitamini A, ambapo walengwa walikuwa 13,682(107%). Watoto 11887 kati ya 12057(98%)walipewa dawa za  minyoo na kupimwa hali za lishe.

2. Kufanya kikao cha maandalizi ya awali ya  mipango na bajeti za afua za lishe: Wajumbe wa kamati ya lishe 22 walijengewa uwezo na wataalam kutoka OR-TAMISEMI namna sahihi ya kuandaa mipango na bajeti za afua za lishe ili kukabiliana na matatizo ya lishe duni kwa jamii.

3. Kufanya maadhimisho ya siku ya afya na lishe ya kijiji/mtaa: Siku za afya na lishe ya kijiji zilifanyika katika mitaa 3(Magegele,Kilimahewa, na vijiji 2(Ibatu na Utengule) ambapo jumla ya watoto

359 walipimwa urefu ili kubaini kiwango cha udumavu ambapo watoto 13 (3.6%)wamedumaa.

4. Kufanya ufuatiliaji wa huduma za lishe katika vituo 11 vinavyotoa huduma za afya ya uzazi na mtoto ifikapo Juni 2020: Watoa huduma za afya 16 kutoka vituo 7 walijengewa uwezo kwenye ujazaji wa takwimu za lishe,ufuatiliaji wa ukuaji na maendeleo ya mtoto na unasihi wa lishe ili kuboresha huduma.

5. Kufanya kikao cha kamati ya lishe ya Halmashauri kwa kipindi cha robo ya pili mwaka2019/2020: Kikao kimefanyika.

Changamoto 

Uhaba wa vidonge vya kuongeza wekundu wa damu kwa akina mama wajawazito katika vituo vya kutolea huduma za afya zinazomilikiwa na taasisi za dini na vituo binafsi hivyo kupelekea halmashauri kuwa na kiwango kidogo cha utoaji wahuduma hiyo.


Maazimio yaliyotolewa na wajumbe kwenye Kikao  cha Kamati ya Lishe cha Tarehe 24/03/2020

1. Kuendelea kutoa elimu ya Lishe bora kuanzia wanafunzi wa shule za misingi mpaka sekondari ili kupunguza tatizo la utapiamlo linalosababisha udumavu wa watoto.

2. Afisa Lishe wa halmashauri ashirikishwe katika kila kikao cha walimu na wazazi ili awe anatoa elimu ya Lishe bora.

3. Maafisa Elimu msingi na Sekondari kwa kushirikiana na Afisa Lishe waandae mpango kazi wa kwenda kuwafundisha wanafunzi(Msingi na Sekondari) Elimu ya Lishe bora.

4. Jamii iendelee kupata Elimu ya Lishe bora kupitia maafisa Lishe waliopo kwenye maeneo yao.


Matangazo

  • Ujio wa Mwenge wa Uhuru 2025, bado siku 13 April 19, 2025
  • Ujio wa Mwenge wa Uhuru 2025, bado siku 12. April 20, 2025
  • Ujio wa Mwenge wa Uhuru 2025, bado siku 11. April 21, 2025
  • Ujio wa Mwenge wa Uhuru 2025, bado siku 10. April 22, 2025
  • Fungua

Habari Mpya

  • Wataalamu na viongozi watakiwa kusimamia upatikanaji na utoaji wa huduma za chanjo.

    April 25, 2025
  • Makambako yang'ara katika tuzo za Afya ya Usafi wa Mazingira ngazi ya Halmashauri za Miji.

    April 09, 2025
  • Jumla ya Miti 15,000 kupandwa Halmashauri ya Mji Makambako kuelekea siku ya Miti duniani mwaka 2025.

    March 15, 2025
  • Maadhimisho ya siku ya wanawake duniani 2025 Mkoa wa Njombe, Mila kandamizi zaelezwa kuwa kikwazo cha ustawi na uwezeshaji

    March 09, 2025
  • Fungua

Video

Shule mpya ya Mbugani Kitandililo sekondari kupitia mradi wa SEQUIP
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Fursa za Usafirishaji
  • Orodha ya Madiwani
  • Uzalishaji wa Umeme wa Upepo
  • Organisation Structure
  • Fursa za Biashara
  • By Laws
  • Permanent Committee

Tovuti Mashuhuri

  • Tovuti ya Ikulu ya Rais
  • Tovuti ya Ofisi ya Utumishi
  • Tovuti ya TAMISEMI
  • Tovuti ya Ofisi ya Takwimu ya Taifa (NBS)
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Open Data Tanzania

Wasomaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Makambako Town Council

    Anuani ya Posta: P.O.BOX 405 Makambako

    Simu ya mezani: 026-2730044

    Simu ya Kiganjani: 0785635383

    Barua pepe: td@makambakotc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Haki miliki ©2017 Halmashauri ya Mji Makambako. Haki zote zimehifadhiwa