• Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
HALMASHAURI YA MJI WA MAKAMBAKO
HALMASHAURI YA MJI WA MAKAMBAKO

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA HALMASHAURI YA MJI WA MAKAMBAKO

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Ardhi na maliasili
      • Raslimali watu na Utawala
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Usafi na mazingira
      • Elimu ya Msingi
      • Ujenzi na Uokoaji
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Elimu ya Sekondari
      • Kilimo, Ushirika na umwagiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maji
    • Vitengo
      • Sheria
      • ICT and Public relations
      • Ugavi na Manunuzi
      • Mkaguzi wa ndani
      • Ufugaji Nyuki
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma ya Afya
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Huduma za Jamii
      • Kamati ya Maadili
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Mipango Miji na Mazingira
    • Ratiba
      • Ratiba ya kumwona Mwenyekiti wa Halmashauri
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
  • Miradi
    • Miradi iliyo kwenye Mpango
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Ripoti mbalimbali
    • Mikataba
    • Mpango Mkakati
    • Hatua
    • Fomu za maombi
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Hotuba
    • Habari Mpya
    • Matukio
    • jarida la mji

Kila Mkulima kupata mbolea ya ruzuku

Tarehe iliyowekwa: July 18th, 2022

Na. Lina Sanga

Kutokana na kupanda bei ya pembejeo za kilimo hususani mbolea,Serikali imeanza kusajili wafanyabiashara wa mbolea na wakulima ili kila mkulima aweze kupata mbolea yenye ruzuku.

Hayo yameelezwa na Mbunge wa Jimbo la Makmbako, Mhe. Deo Sanga leo katika mkutano wa hadhara kwenye vijiji vitatu vilivyopo Kata ya Utengule katika Halmashauri ya Mji Makmbako ikiwa ni ziara yake ya kijiji kwa kijiji,Mtaa kwa Mtaa ili kuongea na wananchi,kusikiliza kero zao na kutoa jumbe mbalimbali za Serikali ikiwa ni pamoja na Ujumbe wa Sensa ya watu na Makazi 2022,Mbolea ya ruzuku na bajeti ya Serikali.

Mhe. Sanga amesema kuwa,mfumo wa uuzaji wa mbolea ya ruzuku ya sasa ni tofauti na uliopita,kwani ruzuku zilizopita walipata wakulima wachache lakini kwa sasa Wizara ya kilimo watawatembelea wakulima katika mashamba yao na kupitia idara ya kilimo watawasajili wakulima kupitia Mwenyekiti wa eneo husika ili kupata idadi kamili za ekari za shamba kwa kila mkulima na kila mkulima atapata kulingana na ukubwa wa shamba lake aliloandikishwa.

Amesema kuwa kupitia takwimu hizo zitazopatikana kupitia Mwenyekiti Serikali itazitumia kuleta ruzuku katika maduka ambayo wakulima wa maeneo hayo wataenda kununua,hivyo mkulima atapata mbolea kwa bei ya punguzo.

“Endapo imetambulika kuwa kuna ekari 300 za watu zinazohitaji UREA kadhaa na DAP kadhaa,kwa hiyo Serikali itatoa ruzuku  kule unakokwenda kununua,ukienda kununua hapo bei inakuwa imeshapunguzwa Mama Samia ameshaweka hela yake pale”,alisema Mhe. Sanga.

Ameongeza pia Serikali kupitia Mama Samia Suluhu Hassan,Rais wa Jmahuri ya Muungano wa Tanzania imeleta mwekezaji,ambaye ameshajenga kiwanda jijini Dodoma cha kutengeneza Mbolea ya UREA,DAP,CAN na aina nyingine na ujenzi wa kiwanda hicho umekamilika kwa asilimia 98 na kinatarajiwa kuanza uzalishaji mwezi Agosti mwaka huu,hivyo bei ya mbolea itapungua zaidi.

Mhe. Sanga ametoa wito kwa wakulima wote kutoa taarifa sahihi za mashamba wanayolima na kujiandikisha ili waweze kupata mbolea za ruzuku.

 

Matangazo

  • Ujio wa Madaktari bingwa Hospitali ya Mji Makambako (Mlowa) September 17, 2025
  • Tangazo la kazi 2024 March 11, 2024
  • Mkutano wa uhamasishaji zoezi la urasimishaji Kata ya Kitisi na Majengo juni 27 - 29,2024 May 28, 2024
  • Mkutano wa uhamasishaji zoezi la urasimishaji Kata ya Mjimwema May 28, 2024
  • Fungua

Habari Mpya

  • Mil. 350.8 za Mikopo ya 10% zimetolewa kwa vikundi 30 Halmashauri ya Mji Makambako,DC aagiza mikopo hiyo kuwa chanzo cha utajiri.

    August 14, 2025
  • MIL 350.8 ZA MIKOPO YA 10% ZATOLEWA KWA AWAMU YA PILI KWA MWAKA 2024/2025.

    August 01, 2025
  • Wataalamu na viongozi watakiwa kusimamia upatikanaji na utoaji wa huduma za chanjo.

    April 25, 2025
  • Makambako yang'ara katika tuzo za Afya ya Usafi wa Mazingira ngazi ya Halmashauri za Miji.

    April 09, 2025
  • Fungua

Video

Shule mpya ya Mbugani Kitandililo sekondari kupitia mradi wa SEQUIP
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Fursa za Usafirishaji
  • Orodha ya Madiwani
  • Uzalishaji wa Umeme wa Upepo
  • Organisation Structure
  • Fursa za Biashara
  • By Laws
  • Permanent Committee

Tovuti Mashuhuri

  • Tovuti ya Ikulu ya Rais
  • Tovuti ya Ofisi ya Utumishi
  • Tovuti ya TAMISEMI
  • Tovuti ya Ofisi ya Takwimu ya Taifa (NBS)
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Open Data Tanzania

Wasomaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Makambako Town Council

    Anuani ya Posta: P.O.BOX 405 Makambako

    Simu ya mezani: 026-2730044

    Simu ya Kiganjani: 0785635383

    Barua pepe: td@makambakotc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Haki miliki ©2017 Halmashauri ya Mji Makambako. Haki zote zimehifadhiwa