• Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
HALMASHAURI YA MJI WA MAKAMBAKO
HALMASHAURI YA MJI WA MAKAMBAKO

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA HALMASHAURI YA MJI WA MAKAMBAKO

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Ardhi na maliasili
      • Raslimali watu na Utawala
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Usafi na mazingira
      • Elimu ya Msingi
      • Ujenzi na Uokoaji
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Elimu ya Sekondari
      • Kilimo, Ushirika na umwagiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maji
    • Vitengo
      • Sheria
      • ICT and Public relations
      • Ugavi na Manunuzi
      • Mkaguzi wa ndani
      • Ufugaji Nyuki
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma ya Afya
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Huduma za Jamii
      • Kamati ya Maadili
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Mipango Miji na Mazingira
    • Ratiba
      • Ratiba ya kumwona Mwenyekiti wa Halmashauri
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
  • Miradi
    • Miradi iliyo kwenye Mpango
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Ripoti mbalimbali
    • Mikataba
    • Mpango Mkakati
    • Hatua
    • Fomu za maombi
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Hotuba
    • Habari Mpya
    • Matukio
    • jarida la mji

Maafisa lishe tumieni mbinu mbadala kutoa elimu ya lishe na unyonyehaji,athari za matumizi ya dawa za kuongeza nguvu za kiume na uzazi wa mpangoRC Mtaka.

Tarehe iliyowekwa: October 20th, 2022

Na. Lina Sanga

Njombe

Maafisa lishe Mkoa wa Njombe wametakiwa kutumia Mbinu mbadala kutoa elimu kwa wanawake,Vijana na watoto  kuhusu masuala ya Unyonyeshaji,afya ya uzazi na matumizi sahihi ya dawa za uzazi wa mpango na dawa za kuongeza nguvu za kiume na athari za matumizi holela ya dawa hizo katika umri mdogo.

Agizo hilo limetolewa na Mkuu wa Mkoa wa Njombe,Mhe. Anthony Mtaka katika kikao cha utiaji saini mikataba ya lishe kilichofanyika leo katika Ukumbi wa Halmashauri ya Mji Njombe,ambapo imedaiwa kuwa Mkoa wa Njombe unakabiliwa na lishe duni kwa watoto hali inayopelekea watoto kupata udumavu.

Mhe. Mtaka amesema kuwa,ipo haja ya maafisa lishe kutoa elimu ya lishe kwa jamii hasa kwa wanawake juu ya faida ya unyonyeshaji,kwa kubuni mbinu mbadala ya kuwapata wanawake na kina mama wanao nyonyesha ili kuwapa elimu hiyo, kwa kuwafata kwenye makongamano ya dini na shuleni kwa ajili ya kuwapa elimu ya lishe wanafunzi ikiwa ni pamoja na athari za matumizi holela ya madawa ya kuongeza nguvu za kiume kwa vijana wa kiume na dawa za kuzuia ujauzito (P2) kwa watoto wa kike.

Amesema kuwa,matumizi ya madawa hayo kwa sasa yamekithiri kwa watoto wadogo bila kufikiria athari wanazoweza kuzipata baada ya miaka kadhaa,hali hii inaweza kuleta kizazi cha ajabu miaka ijayo.

“Kijana ana miaka 15 anatumia dawa za kuongeza nguvu za kiume mara vumbi la kongo ili kumuonyesha ufundi rafiki yake wa kike wala sio mke,kijana akifika miaka 35 amechoka na huenda akapata madhara hadi kwenye ubongo,binti wa miaka 15 anatumia dawa za kuzuia mimba akifika umri wa kuzaa nini kitatokea?ipo haja ya elimu hii kuwafikishia walipo”,alisema Mhe. Mtaka.

Ametoa wito kwa wazazi na walezi kuzungumza na watoto wao juu ya matumizi ya dawa za kuzuia mimba na dawa za kuongeza nguvu za kiume, pamoja na athari zake kwa kutambua wakati sahihi wa kuzungumza na watoto kuhusiana masuala ya afya ya uzazi na kuwataka wanawake kuacha tabia ya kutonyonyesha watoto kwa kuepuka ulaji wa vyakula vyenye afya kwa mtoto kwa kuhofia kunenepa au kuongeza uzito,hali inayosababisha mtoto kupata lishe duni.

Matangazo

  • Ujio wa Mwenge wa Uhuru 2025, bado siku 13 April 19, 2025
  • Ujio wa Mwenge wa Uhuru 2025, bado siku 12. April 20, 2025
  • Ujio wa Mwenge wa Uhuru 2025, bado siku 11. April 21, 2025
  • Ujio wa Mwenge wa Uhuru 2025, bado siku 10. April 22, 2025
  • Fungua

Habari Mpya

  • Wataalamu na viongozi watakiwa kusimamia upatikanaji na utoaji wa huduma za chanjo.

    April 25, 2025
  • Makambako yang'ara katika tuzo za Afya ya Usafi wa Mazingira ngazi ya Halmashauri za Miji.

    April 09, 2025
  • Jumla ya Miti 15,000 kupandwa Halmashauri ya Mji Makambako kuelekea siku ya Miti duniani mwaka 2025.

    March 15, 2025
  • Maadhimisho ya siku ya wanawake duniani 2025 Mkoa wa Njombe, Mila kandamizi zaelezwa kuwa kikwazo cha ustawi na uwezeshaji

    March 09, 2025
  • Fungua

Video

Shule mpya ya Mbugani Kitandililo sekondari kupitia mradi wa SEQUIP
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Fursa za Usafirishaji
  • Orodha ya Madiwani
  • Uzalishaji wa Umeme wa Upepo
  • Organisation Structure
  • Fursa za Biashara
  • By Laws
  • Permanent Committee

Tovuti Mashuhuri

  • Tovuti ya Ikulu ya Rais
  • Tovuti ya Ofisi ya Utumishi
  • Tovuti ya TAMISEMI
  • Tovuti ya Ofisi ya Takwimu ya Taifa (NBS)
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Open Data Tanzania

Wasomaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Makambako Town Council

    Anuani ya Posta: P.O.BOX 405 Makambako

    Simu ya mezani: 026-2730044

    Simu ya Kiganjani: 0785635383

    Barua pepe: td@makambakotc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Haki miliki ©2017 Halmashauri ya Mji Makambako. Haki zote zimehifadhiwa