• Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
HALMASHAURI YA MJI WA MAKAMBAKO
HALMASHAURI YA MJI WA MAKAMBAKO

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA HALMASHAURI YA MJI WA MAKAMBAKO

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Ardhi na maliasili
      • Raslimali watu na Utawala
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Usafi na mazingira
      • Elimu ya Msingi
      • Ujenzi na Uokoaji
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Elimu ya Sekondari
      • Kilimo, Ushirika na umwagiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maji
    • Vitengo
      • Sheria
      • ICT and Public relations
      • Ugavi na Manunuzi
      • Mkaguzi wa ndani
      • Ufugaji Nyuki
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma ya Afya
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Huduma za Jamii
      • Kamati ya Maadili
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Mipango Miji na Mazingira
    • Ratiba
      • Ratiba ya kumwona Mwenyekiti wa Halmashauri
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
  • Miradi
    • Miradi iliyo kwenye Mpango
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Ripoti mbalimbali
    • Mikataba
    • Mpango Mkakati
    • Hatua
    • Fomu za maombi
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Hotuba
    • Habari Mpya
    • Matukio
    • jarida la mji

Mama Samia awatua wanafunzi wa shule ya Msingi Magegele vidumu vya maji,sasa maji yatiririka shuleni

Tarehe iliyowekwa: July 15th, 2022

Na. Lina Sanga

Wanafunzi wa shule ya Msingi Magegele wamemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Mhe Samia Suluhu Hassan kwa Fedha zilizotolewa kwa ajili ya Ujenzi wa Kisima kirefu cha Maji shuleni hapo na kuwasaidia kutobeba  vidumu vya maji kutoka nyumbani kwa ajili ya  matumizi ya vyooni,kudekia, kumwagilia maua na bustani za mboga.

Hayo yamebainishwa na wananafunzi wa shule hiyo wakati wakizungumza na Mbunge wa jimbo la Makambako,Mhe. Deo Kasenyenda Sanga maarufu kama Jah people alipotembelea shule hiyo leo kwa  ajili ya ukaguzi wa ujenzi wa madarasa mawili yaliyojengwa na Asas.

Akizungumza na wanafunzi hao Mhe. Sanga amesema kuwa kama mwakilishi wa wananchi wa jimbo la makambako,alifikisha ujumbe kwa Mhe. Samia ili kuwasaidia wanafunzi kutobeba maji kutoka nyumbani maji yatoke shuleni na suala hilo limefanikiwa.

"Zamani mlikua mnabeba vidumu vya maji kutoka nyumbani kila siku,lakini Mhe. Samia aliposikia ombi langu la kuchimbwa kisima cha maji hapa shuleni ili kuwapunguzia mzigo wa kubeba maji kila siku alilipokea na ametuletea fedha na sasa maji yanatoka shuleni hapa vidumu sasa basi",alisema Mhe. Sanga.

Ametoa wito kwa wanafunzi kulinda miundombinu ya madarasa na vitu vilivyopo  katika shule hiyo,na kila mmoja kuwa mlinzi wa mwenzie na watoe taarifa endapo kuna mtu anataka kuharibu miundombinu ya shule.

Pia amewataka wanafunzi wa kike kusoma kwa bidii kwa kuiga mfano wa Mama samia kwani wakifaulu vizuri , watapata nafasi ya kushika nyadhifa mbalimbali   kwani sasa hivi viongozi wakubwa wengi ni wanawake.

Jumla ya shilingi mil. 32.8 zilipokelewa kwa ajili ya uchimbaji wa kisima kirefu pamoja na uwekaji wa miundombinu ya maji katika shule ya Msingi Magegele,ikiwa ni moja ya miradi iliyotekelezwa kwa fedha za ustawi wa Taifa na Mapambano dhidi ya Uviko 19 kwa mwaka wa fedha 2021/2022 .

Matangazo

  • Ujio wa Mwenge wa Uhuru 2025, bado siku 13 April 19, 2025
  • Ujio wa Mwenge wa Uhuru 2025, bado siku 12. April 20, 2025
  • Ujio wa Mwenge wa Uhuru 2025, bado siku 11. April 21, 2025
  • Ujio wa Mwenge wa Uhuru 2025, bado siku 10. April 22, 2025
  • Fungua

Habari Mpya

  • Wataalamu na viongozi watakiwa kusimamia upatikanaji na utoaji wa huduma za chanjo.

    April 25, 2025
  • Makambako yang'ara katika tuzo za Afya ya Usafi wa Mazingira ngazi ya Halmashauri za Miji.

    April 09, 2025
  • Jumla ya Miti 15,000 kupandwa Halmashauri ya Mji Makambako kuelekea siku ya Miti duniani mwaka 2025.

    March 15, 2025
  • Maadhimisho ya siku ya wanawake duniani 2025 Mkoa wa Njombe, Mila kandamizi zaelezwa kuwa kikwazo cha ustawi na uwezeshaji

    March 09, 2025
  • Fungua

Video

Shule mpya ya Mbugani Kitandililo sekondari kupitia mradi wa SEQUIP
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Fursa za Usafirishaji
  • Orodha ya Madiwani
  • Uzalishaji wa Umeme wa Upepo
  • Organisation Structure
  • Fursa za Biashara
  • By Laws
  • Permanent Committee

Tovuti Mashuhuri

  • Tovuti ya Ikulu ya Rais
  • Tovuti ya Ofisi ya Utumishi
  • Tovuti ya TAMISEMI
  • Tovuti ya Ofisi ya Takwimu ya Taifa (NBS)
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Open Data Tanzania

Wasomaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Makambako Town Council

    Anuani ya Posta: P.O.BOX 405 Makambako

    Simu ya mezani: 026-2730044

    Simu ya Kiganjani: 0785635383

    Barua pepe: td@makambakotc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Haki miliki ©2017 Halmashauri ya Mji Makambako. Haki zote zimehifadhiwa