• Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
HALMASHAURI YA MJI WA MAKAMBAKO
HALMASHAURI YA MJI WA MAKAMBAKO

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA HALMASHAURI YA MJI WA MAKAMBAKO

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Ardhi na maliasili
      • Raslimali watu na Utawala
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Usafi na mazingira
      • Elimu ya Msingi
      • Ujenzi na Uokoaji
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Elimu ya Sekondari
      • Kilimo, Ushirika na umwagiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maji
    • Vitengo
      • Sheria
      • ICT and Public relations
      • Ugavi na Manunuzi
      • Mkaguzi wa ndani
      • Ufugaji Nyuki
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma ya Afya
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Huduma za Jamii
      • Kamati ya Maadili
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Mipango Miji na Mazingira
    • Ratiba
      • Ratiba ya kumwona Mwenyekiti wa Halmashauri
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
  • Miradi
    • Miradi iliyo kwenye Mpango
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Ripoti mbalimbali
    • Mikataba
    • Mpango Mkakati
    • Hatua
    • Fomu za maombi
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Hotuba
    • Habari Mpya
    • Matukio
    • jarida la mji

Mamlaka ya Udhibiti wa Mbolea Tanzania- TFRA yashauriwa kufidia wakulima waliopata hasara.

Tarehe iliyowekwa: June 1st, 2023

Na. Lina Sanga

Njombe

Mamlaka ya Udhibiti wa Mbolea Tanzania (TFRA) imeshauriwa kutafuta namna ya kuwafidia wakulima waliouziwa mbolea zilizochakachuliwa katika msimu wa kilimo wa 2022/2023, kutokana na hasara walizosababishiwa na wauzaji wa mbolea wasio waaminifu,kufanya marekebisho ya sheria ya mbolea,pamoja na kuwezesha matumizi ya teknolojia ya kisasa ya ukaguzi wa mbolea kabla ya kufika shambani.

Rai hiyo imetolewa jana na Mkuu wa Wilaya ya Njombe,Mhe. Kissa Gwakisa Kasongwa katika kikao  na Mkurugenzi Mkuu wa TFRA,Dkt. Stephan Ngailo,kilichofanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Halmashauri ya Mji Njombe na kuhudhuriwa na Viongozi na wataalamu wa Halmashauri za Wilaya ya Njombe.

Mhe. Kissa amesema kuwa, njia ya ukaguzi wa mbolea inayotumika kwa sasa na Maafisa Kilimo ya kutumia kifaa chenye ncha kutoboa mfuko,imepitwa na wakati na baadhi ya Mawakala hukataa kutobolewa kwa mifuko , hali inayotoa mwanya kwa wachakachuaji kukamilisha adhma yao.

Dkt. Stephan Ngailo,Mkurugenzi Mkuu wa TFRA amesema kuwa, marekebisho ya sheria ya mbolea yanaenda kufanyika ili kuhakikisha usalama wa mbolea na kuongeza adhabu kwa wakiukaji wa sheria hiyo ambao kwa sasa walikuwa wanafutiwa leseni na kulipa faini isiyopungua Mil. 100.

Aidha, amesema kuwa usajili wa wakulima ambao hawakujisajili msimu uliopita umeanza pamoja na kuhuisha taarifa za usajili wa wakulima wote, ili kupata taarifa sahihi pamoja na usajili wa vyama vya ushirika vinavyoaminika ili vitumike kusambaza mbolea ifikapo Julai 1,2023.

Ametoa wito kwa wakulima kuanza kujisajili mapema kwa kutoa taarifa sahihi ,ikiwa ni pamoja na idadi ya ekari za mashamba wanazolima pasipo kuogopa,idadi ya misimu wanayolima kama ni miwili au mmoja, ili wapate mbolea wanazohitaji mapema kabla ya msimu wa kilimo haujanzaa na kuwatoa hofu wakulima wadogo hususani wa bustani kuwa, mbolea zitapatikana kwa ujazo wa kuanzia kilo 5 na kuendelea ili hata wakulima wadogo waweze kununua.

Amezitaka Halmashauri kuainisha vituo vya kusambazia mbolea pamoja na maghala ya Serikali ,ambayo hayatumiki ili mwezi Julai mbolea zianze kutolewa na kuwafikia wakulima kwa wakati na kuwataka wataalamu wa Kilimo kuendelea kutoa elimu ya matumizi sahihi ya mbolea kwa wananchi ili kuondoa dhana potofu kuwa kuwa mbolea inaharibu ardhi.

Matangazo

  • Ujio wa Mwenge wa Uhuru 2025, bado siku 13 April 19, 2025
  • Ujio wa Mwenge wa Uhuru 2025, bado siku 12. April 20, 2025
  • Ujio wa Mwenge wa Uhuru 2025, bado siku 11. April 21, 2025
  • Ujio wa Mwenge wa Uhuru 2025, bado siku 10. April 22, 2025
  • Fungua

Habari Mpya

  • Wataalamu na viongozi watakiwa kusimamia upatikanaji na utoaji wa huduma za chanjo.

    April 25, 2025
  • Makambako yang'ara katika tuzo za Afya ya Usafi wa Mazingira ngazi ya Halmashauri za Miji.

    April 09, 2025
  • Jumla ya Miti 15,000 kupandwa Halmashauri ya Mji Makambako kuelekea siku ya Miti duniani mwaka 2025.

    March 15, 2025
  • Maadhimisho ya siku ya wanawake duniani 2025 Mkoa wa Njombe, Mila kandamizi zaelezwa kuwa kikwazo cha ustawi na uwezeshaji

    March 09, 2025
  • Fungua

Video

Shule mpya ya Mbugani Kitandililo sekondari kupitia mradi wa SEQUIP
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Fursa za Usafirishaji
  • Orodha ya Madiwani
  • Uzalishaji wa Umeme wa Upepo
  • Organisation Structure
  • Fursa za Biashara
  • By Laws
  • Permanent Committee

Tovuti Mashuhuri

  • Tovuti ya Ikulu ya Rais
  • Tovuti ya Ofisi ya Utumishi
  • Tovuti ya TAMISEMI
  • Tovuti ya Ofisi ya Takwimu ya Taifa (NBS)
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Open Data Tanzania

Wasomaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Makambako Town Council

    Anuani ya Posta: P.O.BOX 405 Makambako

    Simu ya mezani: 026-2730044

    Simu ya Kiganjani: 0785635383

    Barua pepe: td@makambakotc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Haki miliki ©2017 Halmashauri ya Mji Makambako. Haki zote zimehifadhiwa