• Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
HALMASHAURI YA MJI WA MAKAMBAKO
HALMASHAURI YA MJI WA MAKAMBAKO

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA HALMASHAURI YA MJI WA MAKAMBAKO

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Ardhi na maliasili
      • Raslimali watu na Utawala
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Usafi na mazingira
      • Elimu ya Msingi
      • Ujenzi na Uokoaji
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Elimu ya Sekondari
      • Kilimo, Ushirika na umwagiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maji
    • Vitengo
      • Sheria
      • ICT and Public relations
      • Ugavi na Manunuzi
      • Mkaguzi wa ndani
      • Ufugaji Nyuki
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma ya Afya
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Huduma za Jamii
      • Kamati ya Maadili
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Mipango Miji na Mazingira
    • Ratiba
      • Ratiba ya kumwona Mwenyekiti wa Halmashauri
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
  • Miradi
    • Miradi iliyo kwenye Mpango
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Ripoti mbalimbali
    • Mikataba
    • Mpango Mkakati
    • Hatua
    • Fomu za maombi
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Hotuba
    • Habari Mpya
    • Matukio
    • jarida la mji

Mbunge kuishauri Bodi ya Maji MAKUWASA kuhusu gharama ya Maji.

Tarehe iliyowekwa: August 15th, 2023

Na. Lina Sanga

Mbunge wa jimbo la Makambako,Mhe. Deo Kasenyenda Sanga amesema ataishauri bodi ya Maji ya Mamlaka ya Maji safi na Usafi wa Mazingira Makambako (MAKUWASA),juu ya gharama za maji kwa matumizi nje ya matumizi ya nyumbani ikiwa ni pamoja na ufyatuaji wa tofali.

Mhe. Sanga ameyasema hayo leo katika Mtaa wa Kilimahewa,wakati akijibu maswali na changamoto mbalimbali wanazokabiliana nazo wananchi hususani katika Sekta ya Maji.

Amesema kuwa,kutokana na sheria za maji na gharama  za utoaji wa huduma za maji majumbani,ni vema bodi ya maji ione namna ya kuwasaidia wananchi pindi wanapotaka kufyatua tofali 200 hadi 1,000 kwa ajili ya kuongeza kibanda  wasibadilishiwe gharama ya maji kutoka gharama ya maji ya nyumbani hadi gharama ya kiwanda au biashara.

Awali akitoa ufafanuzi juu ya malalamiko ya moja kati ya wananchi kuhusu  kupandishiwa gharama ya maji baada ya kufyatua tofali,Winfred Mahali,Mkuu wa kitengo cha huduma kwa wateja MAKUWASA ,amesema kuwa  mteja anatakiwa kutoa taarifa kabla ya kubadili matumizi ya maji ambayo yanatofautiana na usajili wa awali, na pindi ikigundulika maji yametumika kinyume na usajili wa mteja Mamlaka itambadilisha mteja  bila kumpa taarifa kwani ni kosa kubadili matumizi.

Amesema kuwa,wateja wa huduma ya maji wamegawanyika kwenye makundi matano,wateja wa majumbani, taasisi, ujenzi,biashara na viwanda na bei zake zinatofautiana kwani matumizi ya nyumbani hayafanani na matumizi katika nyumba ya biashara na kiwanda.

Ameongeza kuwa uniti Moja ya maji ni sawa na lita 1,000 za maji ambazo ni sawa na ndoo 50 za lita 20,na gharama ya maji kwa wateja wa majumbani uniti moja ni 1,500 na biashara uniti moja inauzwa shilingi 3,000.

Pia,amesema kuwa MAKUWASA kwa sasa ipo kwenye mpango  wa kufunga mita za kulipia kabla ya matumizi, ambapo mteja atalipia uniti za maji anazohitaji  na bei za uniti hazitabadilika ila mfumo wa ulipaji maji ndiyo utakaobadilika ambapo kwa sasa mteja anatumia ndipo analipia na mfumo mpya utamtaka mteja kulipia ndipo atumie kama ilivyo kwenye umeme wa luku.

Matangazo

  • Ujio wa Madaktari bingwa Hospitali ya Mji Makambako (Mlowa) September 17, 2025
  • Tangazo la kazi 2024 March 11, 2024
  • Mkutano wa uhamasishaji zoezi la urasimishaji Kata ya Kitisi na Majengo juni 27 - 29,2024 May 28, 2024
  • Mkutano wa uhamasishaji zoezi la urasimishaji Kata ya Mjimwema May 28, 2024
  • Fungua

Habari Mpya

  • Mil. 350.8 za Mikopo ya 10% zimetolewa kwa vikundi 30 Halmashauri ya Mji Makambako,DC aagiza mikopo hiyo kuwa chanzo cha utajiri.

    August 14, 2025
  • MIL 350.8 ZA MIKOPO YA 10% ZATOLEWA KWA AWAMU YA PILI KWA MWAKA 2024/2025.

    August 01, 2025
  • Wataalamu na viongozi watakiwa kusimamia upatikanaji na utoaji wa huduma za chanjo.

    April 25, 2025
  • Makambako yang'ara katika tuzo za Afya ya Usafi wa Mazingira ngazi ya Halmashauri za Miji.

    April 09, 2025
  • Fungua

Video

Shule mpya ya Mbugani Kitandililo sekondari kupitia mradi wa SEQUIP
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Fursa za Usafirishaji
  • Orodha ya Madiwani
  • Uzalishaji wa Umeme wa Upepo
  • Organisation Structure
  • Fursa za Biashara
  • By Laws
  • Permanent Committee

Tovuti Mashuhuri

  • Tovuti ya Ikulu ya Rais
  • Tovuti ya Ofisi ya Utumishi
  • Tovuti ya TAMISEMI
  • Tovuti ya Ofisi ya Takwimu ya Taifa (NBS)
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Open Data Tanzania

Wasomaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Makambako Town Council

    Anuani ya Posta: P.O.BOX 405 Makambako

    Simu ya mezani: 026-2730044

    Simu ya Kiganjani: 0785635383

    Barua pepe: td@makambakotc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Haki miliki ©2017 Halmashauri ya Mji Makambako. Haki zote zimehifadhiwa