• Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
HALMASHAURI YA MJI WA MAKAMBAKO
HALMASHAURI YA MJI WA MAKAMBAKO

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA HALMASHAURI YA MJI WA MAKAMBAKO

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Ardhi na maliasili
      • Raslimali watu na Utawala
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Usafi na mazingira
      • Elimu ya Msingi
      • Ujenzi na Uokoaji
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Elimu ya Sekondari
      • Kilimo, Ushirika na umwagiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maji
    • Vitengo
      • Sheria
      • ICT and Public relations
      • Ugavi na Manunuzi
      • Mkaguzi wa ndani
      • Ufugaji Nyuki
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma ya Afya
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Huduma za Jamii
      • Kamati ya Maadili
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Mipango Miji na Mazingira
    • Ratiba
      • Ratiba ya kumwona Mwenyekiti wa Halmashauri
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
  • Miradi
    • Miradi iliyo kwenye Mpango
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Ripoti mbalimbali
    • Mikataba
    • Mpango Mkakati
    • Hatua
    • Fomu za maombi
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Hotuba
    • Habari Mpya
    • Matukio
    • jarida la mji

Meneja NMB Makambako: Tutashirikiana na halmashauri utoaji wa mikopo ya 10%

Tarehe iliyowekwa: June 16th, 2022

Na. Lina Sanga

Kufuatia agizo la Mkuu wa Mkoa wa Njombe,Mhe. Waziri Kindamba kwa Mkurugenzi wa halmashauri ya Mji Makambako,Bw. Kenneth Haule kutumia utaratibu wa benki katika utoaji na ufuatiliaji wa mikopo ya asilimia kumi kwa vikundi vya wanawake,vijana na watu wenye ulemavu inayotolewa na halmashauri kupitia idara ya maendeleo ya jamii,benki ya NMB tawi la makambako  wamepokea agizo hilo na wameahidi kushirikiana na halmashauri  katika utekelezaji wa agizo hilo.

Mhe. Kindamba alitoa agizo hilo katika mkutano maalumu wa baraza la Madiwani la kuwasilisha mpango kazi na majibu ya menejimenti kwa ajili ya utekelezaji wa hoja za Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa hesabu za Serikali (CAG) kuishia Juni 30,2021,lililofanyika Juni 14,2022 katika ukumbi wa mikutano wa halmashauri ya Mji Makambako.

Akizungumza na wakuu wa idara na vitengo wa halmashauri ya Mji Makambako leo,Meneja wa benki ya NMB tawi la Makambako Bi. Olipa Hebel amesema kuwa,wapo tayari kushirikiana katika utoaji wa elimu ya matumizi ya fedha kwa wanufaika wa Mikopo hiyo,ili kuwasaidia wanufaika hao kutumia fedha hizo katika malengo yaliyokusudiwa na kurejesha kwa muda uliopangwa.

“Sisi NMB Makambako tuna afisa ambaye amehudhuria mafunzo ya utoaji wa mikopo ya vikundi,na yupo tayari kushirikiana na halmashauri katika utoaji wa elimu ya fedha na mikopo,ili kuwajengea uwezo wanufaika wa mikopo ya asilimia kumi kupata manufaa kupitia mikopo hiyo na kurejesha kwa wakati,ili na wengine waweze kunufaika kupitia mikopo hiyo”,alisema Olipa.

Olipa amesema kuwa mbali na utoaji wa elimu ya fedha na mikopo kwa wanufaika hao,pia watashiriki katika zoezi la utoaji wa mikopo hiyo ili kurahisisha zoezi la ufuatiliaji wa madeni kwa vikundi ambavyo havijafanya marejesho kwa wakati.

Pia Olipa pamoja na Maafisa wa benki alioongozana nao walitoa elimu mbalimbali kuhusu huduma zinazotolewa na benki ya NMB,kwa wakuu wa idara na vitengo ikiwa ni pamoja na huduma ya Malipo ya kabla,Mkopo kadi na NMB mkononi.

Naye Bi. Zuena Ungele Mkuu wa idara ya Maendeleo ya Jamii katika halmashauri ya Mji Makambako, kwa niaba ya Mkurugenzi ametoa shukrani kwa Uongozi wa benki ya NMB,kwa kujitoa kushiriki katika zoezi zima la utoaji mikopo ya asilimia kumi kwa vikundi vya Wanawake ,Vijana na Watu wa wenye Ulemavu na kuahidi kushirikiana na afisa aliyeteuliwa kutoka benki hiyo bega kwa bega ili kutekeleza agizo la Mkuu wa Mkoa.

Zaidi ya vikundi 30 vya Wanawake,Vijana na Watu wenye ulemavu katika halmashauri ya Mji Makambako vilivyonufaika na mkopo huo, havijafanya marejesho ya mikopo yao, hali inayokwamisha jitihada za Serikali za kuwawezesha wanawake,vijana na watu wenye ulemavu kuinuka kiuchumi na kufanya mabadiliko ya kiuchumi kuanzia ngazi ya familia,jamii na Taifa kwa ujumla.

Matangazo

  • Ujio wa Mwenge wa Uhuru 2025, bado siku 13 April 19, 2025
  • Ujio wa Mwenge wa Uhuru 2025, bado siku 12. April 20, 2025
  • Ujio wa Mwenge wa Uhuru 2025, bado siku 11. April 21, 2025
  • Ujio wa Mwenge wa Uhuru 2025, bado siku 10. April 22, 2025
  • Fungua

Habari Mpya

  • Wataalamu na viongozi watakiwa kusimamia upatikanaji na utoaji wa huduma za chanjo.

    April 25, 2025
  • Makambako yang'ara katika tuzo za Afya ya Usafi wa Mazingira ngazi ya Halmashauri za Miji.

    April 09, 2025
  • Jumla ya Miti 15,000 kupandwa Halmashauri ya Mji Makambako kuelekea siku ya Miti duniani mwaka 2025.

    March 15, 2025
  • Maadhimisho ya siku ya wanawake duniani 2025 Mkoa wa Njombe, Mila kandamizi zaelezwa kuwa kikwazo cha ustawi na uwezeshaji

    March 09, 2025
  • Fungua

Video

Shule mpya ya Mbugani Kitandililo sekondari kupitia mradi wa SEQUIP
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Fursa za Usafirishaji
  • Orodha ya Madiwani
  • Uzalishaji wa Umeme wa Upepo
  • Organisation Structure
  • Fursa za Biashara
  • By Laws
  • Permanent Committee

Tovuti Mashuhuri

  • Tovuti ya Ikulu ya Rais
  • Tovuti ya Ofisi ya Utumishi
  • Tovuti ya TAMISEMI
  • Tovuti ya Ofisi ya Takwimu ya Taifa (NBS)
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Open Data Tanzania

Wasomaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Makambako Town Council

    Anuani ya Posta: P.O.BOX 405 Makambako

    Simu ya mezani: 026-2730044

    Simu ya Kiganjani: 0785635383

    Barua pepe: td@makambakotc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Haki miliki ©2017 Halmashauri ya Mji Makambako. Haki zote zimehifadhiwa