• Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
HALMASHAURI YA MJI WA MAKAMBAKO
HALMASHAURI YA MJI WA MAKAMBAKO

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA HALMASHAURI YA MJI WA MAKAMBAKO

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Ardhi na maliasili
      • Raslimali watu na Utawala
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Usafi na mazingira
      • Elimu ya Msingi
      • Ujenzi na Uokoaji
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Elimu ya Sekondari
      • Kilimo, Ushirika na umwagiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maji
    • Vitengo
      • Sheria
      • ICT and Public relations
      • Ugavi na Manunuzi
      • Mkaguzi wa ndani
      • Ufugaji Nyuki
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma ya Afya
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Huduma za Jamii
      • Kamati ya Maadili
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Mipango Miji na Mazingira
    • Ratiba
      • Ratiba ya kumwona Mwenyekiti wa Halmashauri
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
  • Miradi
    • Miradi iliyo kwenye Mpango
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Ripoti mbalimbali
    • Mikataba
    • Mpango Mkakati
    • Hatua
    • Fomu za maombi
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Hotuba
    • Habari Mpya
    • Matukio
    • jarida la mji

Miaka 61 ya Uhuru wa Tanzania Bara, Uchumi wa Njombe wafikia Uchumi wa Kati.

Tarehe iliyowekwa: December 9th, 2022

Na. Lina Sanga

Njombe

Kauli hiyo imetolewa leo na Katibu Tawala Mkoa wa Njombe,Bi. Judica Omari katika kilele cha maadhimisho ya miaka 61 ya uhuru wa Tanzania Bara katika Wilaya ya Njombe,yaliyofanyika katika ukumbi wa Njombe Sekondari.

Bi. Judica amebainisha kuwa,katika miaka 61 ya uhuru maisha ya wananchi wa Mkoa wa Njombe yamezidi kuimarika siku hadi siku,kwa kuishi katika nyumba bora na kufanya shughuli mbalimbali za kiuchumi na kuongeza kasi ya ukuaji wa pato la Mkoa kutoka Mil. 5.69 Njombe ilivyokuwa Wilaya chini ya Mkoa wa Iringa hadi kufikia trillion 3.2 kwa mwaka  na pato la kila mwananchi kupanda  kutoka shilingi 103 Njombe ilivyokuwa Wilaya na kufikia Mil. 3.8 kwa mwaka baada ya kupandishwa hadhi na kuwa Mkoa mwaka 2012.

Amesema kuwa kwa upande wa sekta ya elimu,tangu mwaka 1961 Njombe ilikuwa na jumla ya shule za msingi 90 na sekondari 6,shule 3 za Serikali na 3 za watu binafsi na hadi kufikia mwaka huu 2022,Mkoa wa Njombe una jumla ya shule za msingi 544 na shule za sekondari 139,ambapo shule 99 zinamilikiwa na Serikali na shule 40 ni shule binafsi hali inayochangia ukuaji wa sekta ya elimu kwani kila mwanafunzi anapata nafasi ya kujiunga na shule bila ubaguzi kama ilivyokuwa miaka ya ukoloni.

Katika sekta ya afya,Mwaka 1961 Njombe ilikuwa na Zahanati 22 na Hospitali 3 na hakukuwa na vituo vya afya kabisa,tofauti na sasa ambapo  kuna jumla ya vituo vya kutolea huduma za Afya 337,Hospitali 22,Vituo vya afya 44 ngazi ya Kata na Zahanati 271 kwa mujibu wa Sensa ya watu na makazi ya mwaka 2022.

Aidha katika sekta ya barabara, Bi. Judica amebainisha kuwa mwaka 1961 Njombe haikuwa na barabara ya lami na mtandao wa barabara ulikuwa na urefu wa  1,209KM kati ya hizo 76KM zilikuwa barabara za vumbi na 1,133KM kiwango cha changarawe na Udogo, kwa sasa mabadiliko makubwa yametokea ambapo Wakala wa barabara nchini  (TANROADS) hadi mwaka huu anahudumia matengenezo ya barabara zenye jumla ya urefu wa 1,188KM kati ya hizo 251KM zina kiwango cha lami na 937KM zina kiwango cha chanagarawe na udongo.

Ameongeza kuwa Mkoa wa Njombe una mtandao wa barabara wenye urefu wa  5,208KM zinazohudumiwa na Wakala wa barabara vijijini na Mijini (TARURA) ,ambapo jumla ya  42KM zina kiwango cha lami, 1,293KM kiwango cha changarawe na 3,873KM zenye kiwango cha udongo.

Kwa upande wa sekta ya maji katika Mkoa wa Njombe amesema kuwa ,huduma ya maji safi na salama Inapatikana kwa asilimia 73 maeneo ya Mijini na asilimia 83 katika maeneo ya vijijini na jitihada mbalimbali zinaendelea kufanyika ili huduma ya maji ifikie asilimia za kitaifa.

Upande wa nishati,imeelezwa kuwa kati ya Vijiji 381 vya Mkoa wa Njombe Vijiji 298 vina huduma ya umeme na Vijiji 83 vinaendelea kuunganishiwa huduma ya umeme chini ya mradi wa REA III mzunguko wa pili, ambao ulizinduliwa mwezi septemba,2021 na mwishoni  mwa mwaka huu wa fedha 2022/2023 Serikali inategemea Vijiji vyote vya Mkoa wa Njombe kupata huduma ya  umeme na kuanza mradi mpya wa kufanya ujazilizo wa umeme ngazi ya Vitongoji ambapo kwa sasa huduma ya umeme katika ngazi ya Vitongoji ni asilimia 50.

Mkoa wa Njombe una jumla ya wilaya 4,Halmashauri 6,tarafa 18,Kata 107,Mitaa 82,Vijiji 381,Vitongoji 1,839 ambapo Halmashauri ya Mji Makambako ina  Kata 12,Mitaa 54,Vijiji 14,Vitongoji 67,Shule za sekondari 15,binafsi 5 na shule za Serikali 10 na shule za Msingi 51,shule za Serikali 45 na binafsi 6 barabara za mitaa za kiwango cha lami kilomita 12,Vituo vya kutolea huduma za afya vya Serikali 3,Zahanati 7 na Hospitali 1.

"Amani na Umoja ni Nguzo ya Maendeleo Yetu"

Matangazo

  • Ujio wa Mwenge wa Uhuru 2025, bado siku 13 April 19, 2025
  • Ujio wa Mwenge wa Uhuru 2025, bado siku 12. April 20, 2025
  • Ujio wa Mwenge wa Uhuru 2025, bado siku 11. April 21, 2025
  • Ujio wa Mwenge wa Uhuru 2025, bado siku 10. April 22, 2025
  • Fungua

Habari Mpya

  • Wataalamu na viongozi watakiwa kusimamia upatikanaji na utoaji wa huduma za chanjo.

    April 25, 2025
  • Makambako yang'ara katika tuzo za Afya ya Usafi wa Mazingira ngazi ya Halmashauri za Miji.

    April 09, 2025
  • Jumla ya Miti 15,000 kupandwa Halmashauri ya Mji Makambako kuelekea siku ya Miti duniani mwaka 2025.

    March 15, 2025
  • Maadhimisho ya siku ya wanawake duniani 2025 Mkoa wa Njombe, Mila kandamizi zaelezwa kuwa kikwazo cha ustawi na uwezeshaji

    March 09, 2025
  • Fungua

Video

Shule mpya ya Mbugani Kitandililo sekondari kupitia mradi wa SEQUIP
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Fursa za Usafirishaji
  • Orodha ya Madiwani
  • Uzalishaji wa Umeme wa Upepo
  • Organisation Structure
  • Fursa za Biashara
  • By Laws
  • Permanent Committee

Tovuti Mashuhuri

  • Tovuti ya Ikulu ya Rais
  • Tovuti ya Ofisi ya Utumishi
  • Tovuti ya TAMISEMI
  • Tovuti ya Ofisi ya Takwimu ya Taifa (NBS)
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Open Data Tanzania

Wasomaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Makambako Town Council

    Anuani ya Posta: P.O.BOX 405 Makambako

    Simu ya mezani: 026-2730044

    Simu ya Kiganjani: 0785635383

    Barua pepe: td@makambakotc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Haki miliki ©2017 Halmashauri ya Mji Makambako. Haki zote zimehifadhiwa